Upekee wa Mlima Kilimanjaro

Upekee wa Mlima Kilimanjaro

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Mlima Kilimanjaro ni miongoni mwa milima yenye vilele virefu zaidi Duniani. Mlima huu una sifa nyingi zinazoutofautisha na milima mingine, sifa hizo ni pamoja na:

1. Ni miongoni mwa milima saba enye vilele virefu zaidi Duniani. Lakini pamoja na kuwa hivyo bado ni mlima rahisi kupandwa ukilinganisha na milima mingine kwa sababu hauhitaji utaalamu mwingi wala vifaa vingi vya kisasa kama kamba, shoka la kujishikiza kwenye barafu n.k. Inawekewa kwenye kundi la milima ya kupanda kwa kutembea.

2. Ni mlima uliojitenga na kusimama wenyewe pasi na safi za milima tofauti kabisa na milima mingine Duniani.

3. Mlima huu upo karibu zaidi na mstari wa Ikweta, Ikweta ni mstari wa kufikikirika wenye nyuzi sifuri unaogawa Dunia katikati katika pande mbili yaani Kaskazini na Kusini.
Mlima huu kulingana na vipimo vya kijiografia upo umbali wa maili mia mbili na tano (205) kutoka ulipo mstari wa Ikweta.

4. Mlima huu una kuni tatu za kivolkano ambazo ni;
(i) Kibo 5895m
(ii) Mawenzi 5149m
(iii) Shira 3962m

5. Mlima huu ni wa kivolcano, volcano tuli.

6. Zaidi ya nusu ya watu wanaojaribu kupanda mlima huu hushindwa kutokana na kupita ruti mbaya au matatizo ya upumuaji kutikana na mwinuko kutoka usawa wa bahari.

7. Watu wenye umri mkubwa na watoto wamefanikiwa kupanda na kufika katika kilele cha mlima huu. Kwa mfano, Mwaka 2019 Mwanamke wa Kimarekani Anne Lorimo aliyekuwa na umri wa miaka 89 alifanikiwa kufika katika kilele cha mlima Kilimanjaro huku mwaka 2018 Mtoto wa Kimarekani wa miaka sita Coaltan Tunner alifanikiwa kufika katika kilele cha mlima huu.

8. Safari ya kupanda mlima huu ni kama kutoka kwenye Ikweta kwenda Antaktika.

Unaweza ukatafakari kupitia picha hizo hapo chini.
Karibu.

download (17).jpeg

images (44).jpeg

download (16).jpeg

download (19).jpeg

download (18).jpeg
 
hii ni kutokana na kihali ya hewa au hebu ni dadavulie kidogo mkuu nashukuru kwa bandiko zuri
Kadiri unavyopanda mlima huu utahisi badiliko la tabia Nchi, ukiwa chini utahisi hali ya Kiikweta ,hata uoto nao utaisadifu hali hiyo lakini ukifika juu utahisi hali ya maeneo baridi kabisa "temperate latitudes" hali hii inaweza kumfanya mtu kuhisi amehama eneo fulani lenye tabia fulani na kuingia eneo jingine kabisa.
 
Kadiri unavyopanda mlima huu utahisi badiliko la tabia Nchi, ukiwa chini utahisi hali ya Kiikweta ,hata uoto nao utaisadifu hali hiyo lakini ukifika juu utahisi hali ya maeneo baridi kabisa "temperate latitudes" hali hii inaweza kumfanya mtu kuhisi amehama eneo fulani lenye tabia fulani na kuingia eneo jingine kabisa.
okay nmekupata ndo nasikia kuna sehem ni nyasi fupi tuu zinasadifu hali ya kisavana kabisaaaaaaaaaaa
 
Mlima Kilimanjaro ni miongoni mwa milima yenye vilele virefu zaidi Duniani. Mlima huu una sifa nyingi zinazoutofautisha na milima mingine, sifa hizo ni pamoja na;
1.Ni miongoni mwa milima saba enye vilele virefu zaidi Duniani. Lakini pamoja na kuwa hivyo bado ni mlima rahisi kupandwa ukilinganisha na milima mingine kwa sababu hauhitaji utaalamu mwingi wala vifaa vingi vya kisasa kama kamba, shoka la kujishikiza kwenye barafu n.k. Inawekewa kwenye kundi la milima ya kupanda kwa kutembea.

2. Ni mlima uliojitenga na kusimama wenyewe pasi na safi za milima tofauti kabisa na milima mingine Duniani.

3. Mlima huu upo karibu zaidi na mstari wa Ikweta, Ikweta ni mstari wa kufikikirika wenye nyuzi sifuri unaogawa Dunia katikati katika pande mbili yaani Kaskazini na Kusini.
Mlima huu kulingana na vipimo vya kijiografia upo umbali wa maili mia mbili na tano (205) kutoka ulipo mstari wa Ikweta.

4. Mlima huu una kuni tatu za kivolkano ambazo ni;
(i) Kibo 5895m
(ii) Mawenzi 5149m
(iii) Ashira
Rekebisha hapo Kwenye Vilele mkuu, ni Shira sio Ashira
 
Bandiko zuri sana hili Mkuu.
Badilisha uelekeo wa mabadiliko ya climatic regions.

Tuseme kupanda Mlima Kilimanjaro ni sawa na Kutoka Ikweta hadi Arctic Circle hii itapendeza zaidi ya kutoka Ikweta hadi Antarctic.

Mlima Kilimanjaro ni mzuri sana.
IT IS THE HIGHEST FREE STANDING MOUNTAIN IN THE WORLD.
 
Bandiko zuri sana hili Mkuu.
Badilisha uelekeo wa mabadiliko ya climatic regions.

Tuseme kupanda Mlima Kilimanjaro ni sawa na Kutoka Ikweta hadi Arctic Circle hii itapendeza zaidi ya kutoka Ikweta hadi Antarctic.

Mlima Kilimanjaro ni mzuri sana.
IT IS THE HIGHEST FREE STANDING MOUNTAIN IN THE WORLD.
Lakini kote huko mkuu Arctic and Antarctic si kuna barafu la kufa mtu?
 
pande zote ukiwa unaelekea kwenye mlima unazidi kuvutia yaani BREATH TAKING scenery!!
ukiwa juu utaona taa za kenya.
ruti za kupandia ni.
machame-6 to 7 days descnd route mweka.

lemosho-hii unapandia upande wa west huchukua siku 8-9 sababu unazunguka mlima wote.

umbwe -hii very short route but very steep.very rare watu kupandia huko sababu ina mawe sana na very slippery!

rongai-hii route inapendwa sababu haina population na very easy ndio wazee sana hupenda kuitumia.hii ni 6days climbing.

Marangu-hii ndio route ya mwanzo kuwa established ni njia kongwe zaidi inayojulikana na iko na HUTS hivyo haina haja ya tents for shelter.

Mweka- hii huwa ni ya kushukia tuu(descendin route)pia ni karibu sana kufika top kwa njia hii.ila hairuhusiwi kupanda ila tu kwa wapagazi kwa ajili ya kupeleka supply of food.
ni hayo tuu machache ngoja niendelee kufturu
 
Urefu ni mlima wa ngapi? Mbona kuna milima mingine mingi mirefu inayozidi Kilimanjaro?
Ni kweli mkuu Kilimanjaro inaweza kuwa kwenye namba 7 kwa urefu.
Kwenye safu za Himalaya na Andes, ndio kuna vilele virefu.

Hivyo vilele viko kwenye Safu.

ukija kwa Kili, yenyewe inasimama alone.
kibo alone(kiboriloni).
Ndio Maana tunasema Highest Free Standing Mountain in the World.

Hata hivyo vilele vingine vyote viko kwenye Fold Mountain.

Hakuna Mlima Volcano 🌋 mkubwa Kama Kilimanjaro Duniani.
so Kili is Number One.
 
pande zote ukiwa unaelekea kwenye mlima unazidi kuvutia yaani BREATH TAKING scenery!!
ukiwa juu utaona taa za kenya.
ruti za kupandia ni.
machame-6 to 7 days descnd route mweka.

lemosho-hii unapandia upande wa west huchukua siku 8-9 sababu unazunguka mlima wote.

umbwe -hii very short route but very steep.very rare watu kupandia huko sababu ina mawe sana na very slippery!

rongai-hii route inapendwa sababu haina population na very easy ndio wazee sana hupenda kuitumia.hii ni 6days climbing.

Marangu-hii ndio route ya mwanzo kuwa established ni njia kongwe zaidi inayojulikana na iko na HUTS hivyo haina haja ya tents for shelter.

Mweka- hii huwa ni ya kushukia tuu(descendin route)pia ni karibu sana kufika top kwa njia hii.ila hairuhusiwi kupanda ila tu kwa wapagazi kwa ajili ya kupeleka supply of food.
ni hayo tuu machache ngoja niendelee kufturu
Ongezea Marangu ndio route pekee inayo panda na kushuka.
 
Back
Top Bottom