Muju4
JF-Expert Member
- Oct 27, 2014
- 5,489
- 7,446
Wakuu habari zenu,
Nimeangalia hali ya kampeni inavyokwenda na nikasema ni vyema nilete machache niliyopata kujionea.
1. Upinzani unategemea umaarufu na uwezo wa mtu binafsi na sio kujiimarisha kitaasisi hivyo kujikuta hawana agenda zenye muelekeo wa kuleta maendeleo kwa Taifa na kubakia kupinga na kubeza kila kitu kinachofanywa na serikali na wakati mwingine huwa wanaokoteza wagombea hadi ngazi ya Uraisi ni AIBU.
2. Katika Dunia ya sasa ambayo kila Taifa lipo huru katika kujitawala, wapinzani wanaamini mataifa ya nje ndiyo yatakayowaletea maendeleo na kuwapigia kura za ushindi wanasahau wenzao CCM wamejiimarisha hadi vijijini.
{Mwaka jana nilienda Bukoba kuwasalimia ndugu na jamaa, walifurahi sana kuniona maana ulikuwa ni muda mrefu tokea nimeonana na ndugu na jamaa zangu. Kitu kilichonifanya nifurahi ni maongezi kati yangu na Bibi yangu kuhusu uchaguzi wa 2020-2025 kwakweli Bibi aliniambia uchaguzi huu atamchagua Magufuli kwasababu amepelekewa umeme hadi Kijijini na pia alimsifu kupambana na mafisadi (nilimuuliza kivipi vita na mafisadi imemsaidia,jibu alilonipa akaniambia wajukuu zake wanasoma bure hayo kwake ni mafanikio na pesa zingine zinajenga Barabara ). Mwisho alinisihi na mimi nipigie kura CCM 2020-2025.}
3. Kazi alizozifanya JPM zinajieleza zenyewe yaweza kuwa yanaitwa maendeleo ya vitu lakini tujiulize yafuatayo:-
i/ Ukuta wa Mererani
Tumekuwa tunalalamika madini ya Tanzanite yanatoroshwa na kuuza nchi jirani lakini kwasasa ujenzi wa ukuta huu umeyalinda madini yetu na serikali kupata mapato.
ii/ Ujenzi wa miundo mbinu
Kwasasa tukubaliane sehemu kubwa ya nchi imeunganishwa na barabara za lami zamani kwenda mikoa ya kusini (Lindi na Mtwara) ilikuwa ni kama adhabu ila kwa sasa kama una private car Lindi masaa manne hadi matano unafika kutokea Dar.
Hii pia imechochea kukua kwa biashara kwasababu mzigo husafirishwa na kufika kwa wakati hivyo kufanya mahitaji muhimu ya kibinadamu kupatikana nchi nzima.
iii/ Mikopo Elimu ya juu
Serikali ya awamu ya tano imejitahidi katika kutoa mikopo kwa vijana wa elimu ya juu hasa wanaotoka katika familia maskini ili kuweza kuwasaidia vijana wetu kusoma na hivyo Taifa kutngeneza wataalamu ambao watalitumikia Taifa kwa kuajiriwa katika utumishi wa umma,kuajiriwa na wawekezaji au kuajiri na kutengeneza ajira kwa vijana wengine.
iv/ Umeme vijijini
Kwakweli kama utabisha hapa nenda kamuangalie youtube Bwana Bwege wakati akichangia mchango wake bungeni aliisifu serikali katika kusambaza umeme vijijini. Sote tunaelewa umuhimu wa umeme katika maisha yetu kwa hili tuu JPM anatakiwa apongezwe kwa kupewa miaka mitano mwingine.
v/ Mapambano dhidi ya Covid 19
Hapa alicheza kama Pele wakati mataifa mengine yakiwapiga raia wao wakae ndani sisi Watanzania tulikuwa kama vile hakuna linaloendelea na kazi ziliendelea kufanyika, kwakweli kwa hili wala hakuna ubishi msimamo wake ulileta mafanikio makubwa, tusipolisema hili leo bhasi hata miti itasema anastahili pongezi na maono haya unahitajika 2020-2025.
Yapo mengi sana aliyoyafanya JPM katika kipindi cha miaka mitano kiasi itachukua muda mrefu kuelezea kama:-
a. Ujenzi wa vituo vya afya
b. Ndege
c. Stiglers gorge
d. Standard gauge e.t.c
Maendeleo yanahitaji watu kuchapa kazi kwa bidii hakuna mtu atakayekuletea chakula mezani tunapaswa kupambana kwa kufanya kazi kwa bidii kama ni kilimo tulime kwa bidii na kama ni biashara basi tuzidishe ubunifu kupata masoko, maofisini tuongeze ufanisi tukifanya hivyo tutasonga mbele.
Magufuli 2020-2025 ataenda kufanya makubwa zaidi ni muhimu vijana tukampa support ya kutosha ninaimani atatatuvusha kuelekea kule tunapopatarajia (maisha bora).
Tarehe 28/10/2020 kura zote kwa JPM.
Tanzania itajengwa na Watanzania tuwakatae wazandiki na wafitini.
Viva JPM
Kidumu Chama Cha Mapinduzi
Nimeangalia hali ya kampeni inavyokwenda na nikasema ni vyema nilete machache niliyopata kujionea.
1. Upinzani unategemea umaarufu na uwezo wa mtu binafsi na sio kujiimarisha kitaasisi hivyo kujikuta hawana agenda zenye muelekeo wa kuleta maendeleo kwa Taifa na kubakia kupinga na kubeza kila kitu kinachofanywa na serikali na wakati mwingine huwa wanaokoteza wagombea hadi ngazi ya Uraisi ni AIBU.
2. Katika Dunia ya sasa ambayo kila Taifa lipo huru katika kujitawala, wapinzani wanaamini mataifa ya nje ndiyo yatakayowaletea maendeleo na kuwapigia kura za ushindi wanasahau wenzao CCM wamejiimarisha hadi vijijini.
{Mwaka jana nilienda Bukoba kuwasalimia ndugu na jamaa, walifurahi sana kuniona maana ulikuwa ni muda mrefu tokea nimeonana na ndugu na jamaa zangu. Kitu kilichonifanya nifurahi ni maongezi kati yangu na Bibi yangu kuhusu uchaguzi wa 2020-2025 kwakweli Bibi aliniambia uchaguzi huu atamchagua Magufuli kwasababu amepelekewa umeme hadi Kijijini na pia alimsifu kupambana na mafisadi (nilimuuliza kivipi vita na mafisadi imemsaidia,jibu alilonipa akaniambia wajukuu zake wanasoma bure hayo kwake ni mafanikio na pesa zingine zinajenga Barabara ). Mwisho alinisihi na mimi nipigie kura CCM 2020-2025.}
3. Kazi alizozifanya JPM zinajieleza zenyewe yaweza kuwa yanaitwa maendeleo ya vitu lakini tujiulize yafuatayo:-
i/ Ukuta wa Mererani
Tumekuwa tunalalamika madini ya Tanzanite yanatoroshwa na kuuza nchi jirani lakini kwasasa ujenzi wa ukuta huu umeyalinda madini yetu na serikali kupata mapato.
ii/ Ujenzi wa miundo mbinu
Kwasasa tukubaliane sehemu kubwa ya nchi imeunganishwa na barabara za lami zamani kwenda mikoa ya kusini (Lindi na Mtwara) ilikuwa ni kama adhabu ila kwa sasa kama una private car Lindi masaa manne hadi matano unafika kutokea Dar.
Hii pia imechochea kukua kwa biashara kwasababu mzigo husafirishwa na kufika kwa wakati hivyo kufanya mahitaji muhimu ya kibinadamu kupatikana nchi nzima.
iii/ Mikopo Elimu ya juu
Serikali ya awamu ya tano imejitahidi katika kutoa mikopo kwa vijana wa elimu ya juu hasa wanaotoka katika familia maskini ili kuweza kuwasaidia vijana wetu kusoma na hivyo Taifa kutngeneza wataalamu ambao watalitumikia Taifa kwa kuajiriwa katika utumishi wa umma,kuajiriwa na wawekezaji au kuajiri na kutengeneza ajira kwa vijana wengine.
iv/ Umeme vijijini
Kwakweli kama utabisha hapa nenda kamuangalie youtube Bwana Bwege wakati akichangia mchango wake bungeni aliisifu serikali katika kusambaza umeme vijijini. Sote tunaelewa umuhimu wa umeme katika maisha yetu kwa hili tuu JPM anatakiwa apongezwe kwa kupewa miaka mitano mwingine.
v/ Mapambano dhidi ya Covid 19
Hapa alicheza kama Pele wakati mataifa mengine yakiwapiga raia wao wakae ndani sisi Watanzania tulikuwa kama vile hakuna linaloendelea na kazi ziliendelea kufanyika, kwakweli kwa hili wala hakuna ubishi msimamo wake ulileta mafanikio makubwa, tusipolisema hili leo bhasi hata miti itasema anastahili pongezi na maono haya unahitajika 2020-2025.
Yapo mengi sana aliyoyafanya JPM katika kipindi cha miaka mitano kiasi itachukua muda mrefu kuelezea kama:-
a. Ujenzi wa vituo vya afya
b. Ndege
c. Stiglers gorge
d. Standard gauge e.t.c
Maendeleo yanahitaji watu kuchapa kazi kwa bidii hakuna mtu atakayekuletea chakula mezani tunapaswa kupambana kwa kufanya kazi kwa bidii kama ni kilimo tulime kwa bidii na kama ni biashara basi tuzidishe ubunifu kupata masoko, maofisini tuongeze ufanisi tukifanya hivyo tutasonga mbele.
Magufuli 2020-2025 ataenda kufanya makubwa zaidi ni muhimu vijana tukampa support ya kutosha ninaimani atatatuvusha kuelekea kule tunapopatarajia (maisha bora).
Tarehe 28/10/2020 kura zote kwa JPM.
Tanzania itajengwa na Watanzania tuwakatae wazandiki na wafitini.
Viva JPM
Kidumu Chama Cha Mapinduzi