Uchaguzi 2020 Upinzani bado sana kuiangusha CCM, Magufuli atashinda kiurahisi sana

we subiri teuzi, maadam umeshaonekana kule Kawe plus kabila linakubeba kuwa na uhakika mkuu
 
Kwahiyo umefikia hitimisho kwa maono tu ya bibi yako ambaye ana IQ ndogo kuliko hata ya hao wajukuu zake wanaosoma elimu bure.
 
Uwanja upi huo uwekwe sawa ndugu yangu?

Mbona barua mnazo zote Amsterdam ameaandika weee mpaka kachoka sasa anatweet, watu wanapanda jukwaani wanaropoka kadri wanavyojisikia.

Lakini ukweli ni kwamba CCM imejiimarisha sana huu ndio ukweli mchungu na watu hawataki kuusikia.

Tarehe 28/10/2020 mapema watu watakuwa wamesharejea Brussels wanakunywa juice wewe umebakia flyover ya ubungo.

Mwisho na kwa umuhimu fanya kazi hakuna mtu atakuletea chakula mezani.
 
Niko Moshi kaka! Acha kudanganya watu.
Watu wanaonewa tu na kuvamiwa waunge mkono ccm.Yapo baadhi ya majimbo ccm ina nguvu lkn sio kihivyo.

Naondoka Mwanga nitakuwa Machame/Umbwe kama saa 5.00 asubuhi Jumamosi.

Nitakutafuta angalia inbox namba ya simu.
 
Kwa jinsi Jiwe alivyowatukana wana Kagera, hakuna mhaya anayeweza mpa kura hata kwa utani, ndiyo mana walimzomea. Bibi yako kama ni kweli aliyasema hayo basi atakuwa na tatizo la msingi kama wewe au ndiyo sababu uko kama ulivyo.
 
Kwa jinsi Jiwe alivyowatukana wana Kagera, hakuna mhaya anayeweza mpa kura hata kwa utani, ndiyo mana walimzomea. Bibi yaki kama ni kweli aliyasema hayo basi atakuwa na tatizo la msingi kama wewe au ndiyo sababu uko kama ulivyo.
Hauwajui wahaya wewe unasimuliwa tuu, subiria tarehe 28/10/2020 uone kama hawatamchagua JPM nani asiyetaka maendeleo akachague watu wa kususa susa bungeni ?
 
Hizi ni zile post za kuandikiwa hapo Lumumba ..zinakuwa ndefu halafu mode of writing haibadiliki
Kwa hiyo unafikiri ushindi mtaupata maeneo gani kwa mfano hapa tanzania, ambayo mnafikiri mtashinda?
 
Hauwajui wahaya wewe unasimuliwa tuu, subiria tarehe 28/10/2020 uone kama hawatamchagua JPM nani asiyetaka maendeleo akachague watu wa kususa susa bungeni ?
Yani nisimuliwe kuhusu wahaya?
Nasema kura zikihesabiwa kwa haki Jiwe hata 30% hapati. Kuwa mkweli kundi gani katika jamii (Wanafunzi,Wakulima, Wafanyakazi,Wafanyabiashara)wanaweza kumpa kura jiwe? Naomba usikimbie swali
 
Hayo mengine pia umeambiwa na bibi yako au ni kwa akili zako mwenyewe? Ok si vibaya kama umepata chochote kitu.
 
Hayo mengine pia umeambiwa na bibi yako au ni kwa akili zako mwenyewe? Ok si vibaya kama umepata chochote kitu. View attachment 1574074
Bibi hapo ametumika kuonesha ni kwa jinsi gani vijijini wanavyoikubali CCM haya mengine kama ndege nimeyaishi mwenyewe
 
Subiri watakuja kukujibu, kwa sasa bado wako busy ku edit picha za 2015.
 
Hakuna wakumuondoa Magufuli hapo ni Vibendera tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…