Uchaguzi 2020 Upinzani kujitoa kushiriki Uchaguzi Mkuu 2020 siyo uoga wala ujinga, kitakuwa ni kitendo cha ushujaa na uzalendo

Uchaguzi 2020 Upinzani kujitoa kushiriki Uchaguzi Mkuu 2020 siyo uoga wala ujinga, kitakuwa ni kitendo cha ushujaa na uzalendo

Nasema itakuwa ni ushujaa na kutanguliza maslahi ya taifa, itakuwa ni njia pekee sahihi na muafaka ya kuonesha kutokubaliana na uchaguzi huu batili uliojaa hila, fitina na nia ovu.

Kama tume itakataa kuwarudisha wagombea ubunge zaidi ya 150 wa upinzani hususani ACT na CHADEMA waliowaengua kwa sababu moja ama nyingine basi upinzani ukubali tu kuwa kujitoa kushiriki uchaguzi ndiyo njia pekee sahihi na muafaka.

Mpaka sasa kwa mujibu wa Zitto Kabwe wagombea ubunge wa chama hicho zaidi ya majimbo 45 Tanzania bara na Zanzibar wameenguliwa. CHADEMA mpaka sasa ni karibia majimbo 25 kwa Tanzania Bara sijajua huko Zanzibar na bado uenguaji unaendelea. Na hapo kuna wagombea pia wa CUF, NCCR wameenguliwa, ukijumlisha unapata idadi ya wagombea wasiopungua 150 kwa vyama vyote vya upinzani nchi hii.

Hapo bado sijazungumzia udiwani, majimbo ambayo wagombea ubunge wa upinzani wameondolewa kuna wagombea udiwani at least wasiopungua 10 wanaondolewa. Sasa idadi ya madiwani ni makumi kwa mamia wanaondolewa.

Je upinzani bado unaamini una haja ya kuendelea kushiriki uchaguzi huu? Je upinzani utaendelea kujilisha upepo mpaka lini?

Upinzani kuendelea kushiriki uchaguzi huu ni kujiaibisha wenyewe. Sisi sote ni watu wazima na wenye uelewa. Hatutakiwi kujidanganya, kujipa matumaini hewa na kujilisha upepo. Kusema eti watanzania watakubali kuandamana kupinga udhalimu huu ni uongo, watanzania ni waoga sana, hivyo mwitikio mdogo wa hayo maandamano utapelekea hao wachache watakaoitikia kuumia na hiyo itawavunja moyo na kuendelea kuwaogopesha wengi.

NI ATHARI ZA KUENDELEA KUSHIRIKI HUU UCHAGUZI?

Ni kuwasindikiza CCM, kuendelea kubariki uhuni wanaoufanya, kuendelea kushiriki dhuluma yao na najisi kwa umma.

Kushiriki huu uchaguzi na wakati unajua mwenzako ana majimbo 25 Zanzibar na 30 bara ambayo amejitwalia mezani. Halafu unaenda kugombania majimbo 200 ambayo pia uhakika wa kutangazwa hauna ni kujidanganya big time.

Ishu isiwe Lissu tu, hapo ndipo tunapodanganywa tunang'ang'ana na Lissu huku wenzetu wanajizolea ubunge na udiwani wa dezo mpaka ikifika siku ya uchaguzi na huyo Lissu naye wanamuibia kura tunabaki na kitu gani?

Tujitoe mapema sana kabla hatujafika hata mwisho mwa kampeni. Najua watasema tunamwachia fisi bucha ni heri tuonekane tulimwachia fisi bucha kuliko tukaonekana tulishiriki pamoja na fisi kula nyama buchani kumbe tuliambulia mifupa michache tu.

Magufuli anataka kuthibitisha ile kauli yake kwamba ameufuta upinzani na hapo anajiona mjanja sana maana aliteua wana ccm kwenye ukurugenzi makusudi na matokeo yake yanaonekana sasa hivi. Sasa sisi tusiwe sehemu ya kumsindikiza Magufuli kwenye hiyo project yake.

Narudia tena utakuwa uzalendo na ushujaa kususia uchaguzi huu kuliko kujidanganya na kujilisha upepo kuwa tutashinda pamoja na mwenendo mzima unavyoonekana katika hizi hatua za mwanzo.
Zanzibar watu waliacha kuzikana, kuoleana hata kununuliana kwa upumbavu kama huuhuu unaofanyika sasa.
 
Wewe jamaa ni mnafiki sana unaongea kama ni mgeni kutoka Toronto hujui kwamba upinzani ulikatazwa kufanya siasa kwa miaka mitano? Unaongea kama vile hujui kwamba walipothubutu kuongea tu kesi za uchochezi ziliwahusu? Eti wakimya sana daaa!
Kawaida yao ni KUJISAHAULISHA NA WANADHANI WATANZANIA WOTE NI MAZWAZWA KAMA WAO!!!
 
Nasema itakuwa ni ushujaa na kutanguliza maslahi ya taifa, itakuwa ni njia pekee sahihi na muafaka ya kuonesha kutokubaliana na uchaguzi huu batili uliojaa hila, fitina na nia ovu.

Kama tume itakataa kuwarudisha wagombea ubunge zaidi ya 150 wa upinzani hususani ACT na CHADEMA waliowaengua kwa sababu moja ama nyingine basi upinzani ukubali tu kuwa kujitoa kushiriki uchaguzi ndiyo njia pekee sahihi na muafaka.

Mpaka sasa kwa mujibu wa Zitto Kabwe wagombea ubunge wa chama hicho zaidi ya majimbo 45 Tanzania bara na Zanzibar wameenguliwa. CHADEMA mpaka sasa ni karibia majimbo 25 kwa Tanzania Bara sijajua huko Zanzibar na bado uenguaji unaendelea. Na hapo kuna wagombea pia wa CUF, NCCR wameenguliwa, ukijumlisha unapata idadi ya wagombea wasiopungua 150 kwa vyama vyote vya upinzani nchi hii.

Hapo bado sijazungumzia udiwani, majimbo ambayo wagombea ubunge wa upinzani wameondolewa kuna wagombea udiwani at least wasiopungua 10 wanaondolewa. Sasa idadi ya madiwani ni makumi kwa mamia wanaondolewa.

Je upinzani bado unaamini una haja ya kuendelea kushiriki uchaguzi huu? Je upinzani utaendelea kujilisha upepo mpaka lini?

Upinzani kuendelea kushiriki uchaguzi huu ni kujiaibisha wenyewe. Sisi sote ni watu wazima na wenye uelewa. Hatutakiwi kujidanganya, kujipa matumaini hewa na kujilisha upepo. Kusema eti watanzania watakubali kuandamana kupinga udhalimu huu ni uongo, watanzania ni waoga sana, hivyo mwitikio mdogo wa hayo maandamano utapelekea hao wachache watakaoitikia kuumia na hiyo itawavunja moyo na kuendelea kuwaogopesha wengi.

NI ATHARI ZA KUENDELEA KUSHIRIKI HUU UCHAGUZI?

Ni kuwasindikiza CCM, kuendelea kubariki uhuni wanaoufanya, kuendelea kushiriki dhuluma yao na najisi kwa umma.

Kushiriki huu uchaguzi na wakati unajua mwenzako ana majimbo 25 Zanzibar na 30 bara ambayo amejitwalia mezani. Halafu unaenda kugombania majimbo 200 ambayo pia uhakika wa kutangazwa hauna ni kujidanganya big time.

Ishu isiwe Lissu tu, hapo ndipo tunapodanganywa tunang'ang'ana na Lissu huku wenzetu wanajizolea ubunge na udiwani wa dezo mpaka ikifika siku ya uchaguzi na huyo Lissu naye wanamuibia kura tunabaki na kitu gani?

Tujitoe mapema sana kabla hatujafika hata mwisho mwa kampeni. Najua watasema tunamwachia fisi bucha ni heri tuonekane tulimwachia fisi bucha kuliko tukaonekana tulishiriki pamoja na fisi kula nyama buchani kumbe tuliambulia mifupa michache tu.

Magufuli anataka kuthibitisha ile kauli yake kwamba ameufuta upinzani na hapo anajiona mjanja sana maana aliteua wana ccm kwenye ukurugenzi makusudi na matokeo yake yanaonekana sasa hivi. Sasa sisi tusiwe sehemu ya kumsindikiza Magufuli kwenye hiyo project yake.

Narudia tena utakuwa uzalendo na ushujaa kususia uchaguzi huu kuliko kujidanganya na kujilisha upepo kuwa tutashinda pamoja na mwenendo mzima unavyoonekana katika hizi hatua za mwanzo.
Usichanganye mambo ,sema chadema kujitoa ,usisemee upinzani wote
 
Chadema sidhani kama watajitoa ila ushindi wa mezani sio tija. Nguvu ya wananchi imepokwa na Serikali very sad.
 
Na wale wa sisiem walio katwa unasema je? Ina maana hawa watu ndo wanatuchagulia wananchi kuwa nani ni mgombea, uhuni gani huu! Tusisahau kuwa kuna kuchagua what na kunakuchagua chama?! Mfano Lema hapa Arusha kwa miaka 10 aliyoko alifanya nn? Huwezi mchagua mtu kama huyu ambae hata impact yake kwenye jamii haupo licha ya blah blah! Sasa kwa hali hii wananchi wakimchagua Gambo je tutasema kapendelewa? Same applies pia kwa wegombea wengine hata kama ni sisiem je ulipochaguliwa ulifanya nn jimboni mwako licha ya kupiga meza na kelele na kusema ndio bungeni, umefanya nn?? Ni wakati watanzania tuache siasa za mikumbo, siasa za hisia, tunataka siasa za kiutendaji haijalishi upo chama gani ukishindwa kudeliver ww ni wa kuktwa tu!

Mkuu jitahidi sana ujifunze ili usirudie tena kukosea kazi za udiwani, ubunge, na uraisi nenda kwenye ktb
 
Back
Top Bottom