Uchaguzi 2020 Upinzani, mnafanya vizuri wenzenu mchecheto

Uchaguzi 2020 Upinzani, mnafanya vizuri wenzenu mchecheto

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana heshima kwenu.

Tunapoendelea kusonga mbele na jitihada za kuleta mabadiliko ambayo kila aliye mzalendo angeyapenda, wenye mawazo mgando wanazidi kuingiwa mchecheto.

Hofu imewatanda hawakumbuki jana walisema nini, leo wasemeje wala kesho watasema je.

Palikuwa na hadithi, Lissu harudi. Mbowe hatamwachia Lissu kugombea urais. Lissu akirudi atakamatiwa JNIA. CHADEMA mgombea atakuwa Nyalandu. Lissu hatapata uteuzi wa tume.

Mara oh, Lissu atashikiliwa na mahakama kwa ajili ya kesi zake ambazo nazo ni za kubumba bumba tu nk, nk.

Yakawepo, Membe anakuja kuvuruga upinzani. Membe ni pandikizi lao yupo kwenye kazi maalum, nk, nk.

Ambayo hawakuyataka ndiyo yanakuwa. Wameshikwa pabaya wao na wapambe wao. Kote nchale. Wakisimama nchale, wakikakaa na hata wakichuchumaa nchale.

Wamepagawa na wanaweweseka. Kwa hakika wamechachawa hawajui washike wapi.

"Wenzangu mliwapa miaka kumi kumi mbona miye mnipe mitano tu?"

Aku! Kwani ni zawadi tu bila wajibu?

CHADEMA na ACT hongereni kwa kuzitambua zilizo kelele za vyura na kuzipuuza vilivyo. Mmethubutu Ila safari bado. Tungali tunasubiri ile ahadi yenu kuu:

"Msipokuwa na mgombea mmoja wa upinzani Watanzania hawatawaelewa."

Wako wapi NCCR na mzee wa SMS za usiku kwa Mzee baba? Haiyumkiniki angali anaendeleza libeneke lake!

Yuko wapi yule propesa libumba na CUF aliyoachiwa? Atavuna wabunge na madiwani wangapi Zanzibar 2020? Kusoma hujui hata picha kuangalia wajameni?

Yuko wapi Spunda na bwabwa lake na ndizi mbivu za kushushia? Pamoja na yote mkuu Spunda umetikisa Ila hawa wenye mawazo mgando. Tuwatoe kwanza, ubwabwa tutakula tu tukishamalizana nao.

Wako wapi hawa wengine ambao hata majina yao tu wapiga kura walio wengi hawayajui?

Tanzania ya leo inahitaji haki, uhuru na maendeleo au bata kama wengine wanavyoita. Maendeleo ya watu kabla ya maendeleo ya vitu. Haki na uhuru wetu haviwezi kuwekwa daraja la pili dhidi ya vitu.

Wanayo haki wenye mawazo mgando kuingiwa mchecheto.

Na bado!

Hadi sasa hawajatamka uhuru wala haki popote pale. Kwao wao uhuru na haki zetu si suala bali madege yasiyokuwa na cha kufanya na zaidi ya 95% ya watanzania.

Kwamba kwani hata ni miundo mbinu basi? Labda kama ni Dar, Dodoma na Chato. Kwa maana kwingine kupo hivi:

Ukarabati kichekesho Rusahunga - Rusumo

Lissu tembelea Rusahunga - Rusumo haraka iwezekanavyo

Wakati Chatto kupo hivi:

Chato kupo hivi. Je, hii ngozi haivutwi mno?

Ajisifuye, kwa miundo mbinu ipi?
 
Mabibi na mabwana heshima kwenu.

Tunapoendelea kusonga mbele na jitihada za kuleta mabadiliko ambayo kila aliye mzalendo angeyapenda, wenye mawazo mgando wanazidi kuingiwa mchecheto...
Hivi kwa nini wanachadema wakiongozwa na Tundulisu, wamekubali kuua watu dhidi ya korona? Angalia tundulisu anavyopita kila siku kwenye misururu ya watu wengi watanzania bila hata kuchukua tahadhali yoyote ya kuenea kwa ugonjwa was korona, ambao chadema walikua mstari wa mbele kuilazimisha serikali ya JPM, iweke rock down, na kuitaka kuzuia misongamano pamoja na makongamano mbalimbali ilikujikinga na korona.

Kwa nini chadema na tundu lisu nao wameshindwa kuwalinda na kuwaweka mazingira hatarishi watanzania dhidi ya maambukizi ya gonjwa Kali la korona?

Kuwaweka watu kila siku kwenye misururu na mirundikano bila kujali tahadhali zidi ya korona hamuoni kama huo ni uuaji wa watanzania??
AU NA NYIE MUMEUNGA JUHUDI KWA MAGUFULI AMBAYE YEYE ANAAAMINI NA KUTANGAZA KORONA HAIPO TANZANIA?

Nikimuangalia tundulisu kwa Mara ya mwisho alivaaa barakoa akiwa uberigiji, lakini alipofika terminal3, gafla barakoa ikavaliwa shingonii, huku akijua korona ipo, na anapokelewa na misuru ya watu,kuanzia pale tundulisu sijamuona akiwa amevaaa barakoa ipasavyo.
JE NA NYIE CHADEMA MUMEUNGA JUHUDI KWA MAGUFULI?
 
Hivi kwa nini wanachadema wakiongozwa na Tundulisu, wamekubali kuua watu dhidi ya korona?

Angalia tundulisu anavyopita kila siku kwenye misururu ya watu wengi watanzania bila hata kuchukua tahadhali yoyote ya kuenea kwa ugonjwa was korona, ambao chadema walikua mstari wa mbele kuilazimisha serikali ya JPM, iweke rock down, na kuitaka kuzuia misongamano pamoja na makongamano mbalimbali ilikujikinga na korona...
Chadema ni Wapigaji balaa!!
 
Mabibi na mabwana heshima kwenu.

Tunapoendelea kusonga mbele na jitihada za kuleta mabadiliko ambayo kila aliye mzalendo angeyapenda, wenye mawazo mgando wanazidi kuingiwa mchecheto....
Eti Jafo anatangaza ajira za walimu baada ya kuona hali imekuwa tete, kwa taarifa yenu waliokosa ajira ni wengi na watakaopata hawatoshi kuwapumbaza watakaobaki kiasi cha kuwashawishi wawapigie kura majambazi ya fisiemu.
 
Hivi kwa nini wanachadema wakiongozwa na Tundulisu, wamekubali kuua watu dhidi ya korona? Angalia tundulisu anavyopita kila siku kwenye misururu ya watu wengi watanzania bila hata kuchukua tahadhali yoyote ya kuenea kwa ugonjwa was korona, ambao chadema walikua mstari wa mbele kuilazimisha serikali ya JPM, iweke rock down, na kuitaka kuzuia misongamano pamoja na makongamano mbalimbali ilikujikinga na korona...

Habari za Corona zitakusaidia nn... Kwamba fulani kasema hivi na fulani hivi... Hayo ya Kenya yaache.
 
Hivi kwa nini wanachadema wakiongozwa na Tundulisu, wamekubali kuua watu dhidi ya korona? Angalia tundulisu anavyopita kila siku kwenye misururu ya watu wengi watanzania bila hata kuchukua tahadhali yoyote ya kuenea kwa ugonjwa was korona, ambao chadema walikua mstari wa mbele kuilazimisha serikali ya JPM, iweke rock down, na kuitaka kuzuia misongamano pamoja na makongamano mbalimbali ilikujikinga na korona...
Kwani corona ilikuwepo kwenye ilani ya ccm 2015? Magufuli aliahidi kupambana na corona? Yaani mmedakia corona na kuifanya agenda ya uchaguzi? Aisee ndo maana mnatiatia huruma daily
 
Eti kijafo kinatangaza ajira za walimu baada ya kuona hali imekuwa tete, kwa taarifa yenu waliokosa ajira ni wengi na watakaopata hawatoshi kuwapumbaza watakaobaki kiasi cha kuwashawishi wawapigie kura majambazi ya fisiemu.

Na bado.

Hivi mawaziri nao bado ni mawaziri hata bwana kyembe pia?
 
Kwani corona ilikuwepo kwenye ilani ya ccm 2015? Magufuli aliahidi kupambana na corona? Yaani mmedakia corona na kuifanya agenda ya uchaguzi? Aisee ndo maana mnatiatia huruma daily
Mimi nimewauliza chadema na tundulisu, kuendeleza misongamano na huku wakijua korona ipoo
Jee na nyie chadema kwa sasa mnakubaliana korona imeisha?
Mbina hamchukuitahadhari kama ilivyokuwa mwanzoniii?
 
Mimi nimewauliza chadema na tundulisu, kuendeleza misongamano na huku wakijua korona ipoo
Jee na nyie chadema kwa sasa mnakubaliana korona imeisha?
Mbina hamchukuitahadhari kama ilivyokuwa mwanzoniii?

Ungesema "nyomi" za hatari zinazowatia mburura nyie mchecheto haswaa, ungeeleweka tu mkuu.

Suala ni kuwa nyomi zile ni za wa watu wanaotaka haki na uhuru wao wa kuishi. Wanataka kumtoa jahili kutoka madarakani kikatiba. Kisha wake na serikali yenye kutambua haki za raia zikiwamo za kuishi dhidi ya yote ikiwamo Corona pia.

Nyomi hizi kama za Dodoma jana ndiyo zinazowatia mchecheto vilivyo.

Na bado!

Si mlisema harudi? Si mlisema ataenguliwa? Membe naye si mlidai bado ni wenu?

Mtajichetua sana.
 
Ungesema "nyomi" za hatari zinazowatia mburura nyie mchecheto haswaa, ungeeleweka tu mkuu.

Suala ni kuwa nyomi zile ni za wa watu wanaotaka haki na uhuru wao wa kuishi. Wanataka kumtoa jahili kutoka madarakani kikatiba. Kisha wake na serikali yenye kutambua haki za raia zikiwamo za kuishi dhidi ya yote ikiwamo Corona pia...
Korona imeisha?
 
Back
Top Bottom