Tz boy 4tino
JF-Expert Member
- Sep 14, 2014
- 1,598
- 1,822
Tueleze Kenya wapo mbele kwa kipengele kipi? Mauaji au ?Tanzania tuna chembe za ustaarabu ila sio demokrasia tuache kujipa moyo. We are more of a conservative society , .
Kenya wapo mbali kwenye demokrasia hilo ni swala lisilopingika
Uhuru wa kuandamana, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kuhoji mamlaka.. Bongo tuna mengi ya kujifunza huo ndo ukweliTueleze Kenya wapo mbele kwa kipengele kipi? Mauaji au ?
Kenya ukiandamana ovyo unapigwa risasi, walivyo wahuni zaidi wamewavalishwa Mungiki mavazi ya jeshi, na Mungiki kama wanavyojulikana, kazi yao ni kuua tu.Uhuru wa kuandamana, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kuhoji mamlaka.. Bongo tuna mengi ya kujifunza huo ndo ukweli
MK254 Ninakushangaa sana kulinganisha nchi inayokataza maandamano na nchi inayouwa na kutesa watu kwa sababu tu wameandamana, ama ni uzalendo umekuzidi au unafanya makusudi. Magufuli anahisi kwamba maandamano yataleta uvunjifu wa amani na kupelekea watu kuuliwa, ndicho kinachotokea Kenya, wewe mwenyewe unakiri kwamba wanapoandamana wanafanya uhalifu unaolazimisha polisi kutumia silaha, jambo ambalo sio kweli, watu wameuliwa wakiwa kazini wanachomelea madirisha, yule binti wa miaka 11 alikuwa akicheza, yule mtoto wa miezi sita kule kisumu alikuwa amepakatwa na mama yake wamekaa sebuleni, yule Padre Kisumu, alitekwa njiani kwa sababu tu amemsema Uhuru Kenyatta, sasa kati ya Magufuli ambaye ameona mbali na kuzuia hayo mauaji yasitokee kwa kuzuia maandamano, na uhuru Kenyatta anayeruhusu maandamano, kisha kuyadhibiti kwa kuwapiga watu risasi nani ni mwenye busata?Hehehe huwa nacheka mnavyo andaa hoja zenu na kujiliwaza, mpo mbali sana kujlinganisha na Kenya.
Bora kwetu maandamano yanaruhusiwa, mara nyingi vurugu huibuka pale waandamanaji wanakiuka taratibu na kuanza kujihusisha na mambo yasioruhusiwa. Kama tukio la juzi pale waandamanaji walithubutu kuvamia kituo cha polisi.
Nyie kwenu maandamano hata ya amani hayaruhusiwi, hata wapinzani kuhutubia wananchi ni hatia, kuhoji takwimu za kiuchumi ni hatia, juzi Zitto Kabwe mumemtia ndani.
Mwengine kahoji mambo ya madini, leo hii tunamuuguza Kenya baada ya kupigwa risasi 38, halafu unanichekesha sana ukisema eti Watanzania walipigia kelele tukio za Lissu kupigwa marisasi. Nyie kituko kweli......
Yaani hata nashindwa nianzie wapi kutaja jinsi mlivyo nyuma, nafikiri kitu ambacho huwa kinawasaidia hamuanikwei ni kwasababu mumejifcha nyuma ya Kiswahili. Huwa kinaficha sana matukio yenu hivyo wadau nje wanasubiri kutafsiriwa taarifa zenu.
Una mahaba yanakusumbua.Tanzanian ni nchi inayoongozwa kwa taratibu za kulingana na katiba tuliyonayo,
Kuna watu wanafika hatua wanasema kwamba iko demokrasia ya juu sana nchini Kenya kuliko Tanzania,
1.Kupiga risasi wapinzani na kuwaua ndo demokrasia ya Kenya?
2.Kupiga mtoto wa miaka mitatu risasi kwa masuala ya kisiasa ndo demokrasia?
3. Kuua mwakilishi wa IEBC ndo demokrasia?
4. Kubaguana kikabila ndo demokrasia?
BABA WA DEMOKRASIA AFRIKA NI TANZANIA hakuna nchi nyingine zaidi ya Tanzania,
Upinzani wa Tanzania una mawenge
Madikiteita ndo Wanadhani hivyo.Tanzania hakuna upinzani, kuna kikundi cha wasanii kinachojiita upinzani!
Kenya ukiandamana ovyo unapigwa risasi, walivyo wahuni zaidi wamewavalishwa Mungiki mavazi ya jeshi, na Mungiki kama wanavyojulikana, kazi yao ni kuua tu.
Hata Tz unaruhusiwa kuhoji chochote ili mradi tu usivuke mipaka.
Tz kuna vyombo vya habari vingi zaidi ya Kenya.
Mbona huzungumzii watu kwa mamia waliopotea Mombasa na ukanda mzima wa pwani kwa sababu tu ya kutimiza matakwa ya katiba ya Kenya kutaka Kujitenga? MRC wameuliwa karibu wote walio baki wamekimbilia Somalia. Taja watu 5 Tanzania waliouliwa na vyombo vya ulinzi vya Tanzania, kila jina moja, mimi nitakupa majina kumi ya wakenya waliouliwa na serikali, hapa Tanzania utaishia kuzungumzia Ben Sanane, Mawazo na Mwangosi, tena suala la mwangosi muhusika alihukumiwa kifungo cha miaka 15, tena ni zaidi ya miaka minne sasa tangu tukio hilo litokee, Kenya ndani ya miaka hiyo minne, zaidi ya watu 400 wameuliwa na hakuna hata muhusika mmoja aliyekamatwa, huwezi hata kidogo kulinganisha Kenya na Tanzania katika hili.Wauguzi na madaktari waliandamana kwa muda mrefu na hakuna aliyepigwa risasi, Bongo madaktari walijaribu hicho kitu kuna jamaa anaitwa Ulimboka hana hamu na maandamano tena.
Hayo maandamano yanayoruhusiwa ndio police wanakuja kutandika risasi za moto, mbaya zaidi hadi Mungiki na wao wanavalishwa jezi za police kwenda kuua Jaluo, nyie ni jamii isiyo na huruma kabisa.
Ndio, Tz mikutano ya kisiasa inayoruhusiwa ni viongozi wa sehemu husika, kama wewe ni Mbunge wa Kajiado, fanya mkutano na wananchi wako wa Kajiado, hakuna haja ya kwenda kufanya uchochezi Nairobi. Huo si utaratibu mbaya na unaleta utulivu wa kisiasa.
Tz kuna sheria ya takwimu, mtu akionekana anafanya maksudi kupotosha takwimu ataenda kujielezea mahakamani, wao ndio watamuhukumu na takwimu zake za kupika. Kuruhusu wanasiasa waropoke uongo wowote kwa jina la uhuru si ushujaa, ni ujinga. Mwanasiasa anageuza takwimu kwa maksudi ili tu atengeneza chuki, hii si uhuru wala demokrasia, acha wakufundishwe adabu mahakamani.
Huna maana wewe, mgomo wa manesi Kenya umekaa miezi sasa, hiyo si demokrasia tena ni vurugu. Kuna watu wamepoteza maisha hapo wewe unakuja kujisifia hapa udhaifu wa GoK. Kuacha mgomo kukaa karibu nusu mwaka si ushujaa ni udhaifu na ujinga.Wauguzi na madaktari waliandamana kwa muda mrefu na hakuna aliyepigwa risasi, Bongo madaktari walijaribu hicho kitu kuna jamaa anaitwa Ulimboka hana hamu na maandamano tena.
Kuna tofauti ya kueleza takwimu na kuanza kudanganya kwa maksudi kwa manufaa ya kisiasa. Mtu anajaribu kudanganya hata vitu vilivyo wazi ili mradi apate mileage ya ki siasa. Ku endelea kubishana nae sana ni kuendekeza ujinga, acha akaielekeze mahakama hizo data amepikia wapi.Mtu akieleza takwimu unafaa umjibu kwa hoja sio kumkamata kamata, huo ni udhalimu na ubabaishaji, dah Raila angekua hiyo Tanzania sijui mngekua mshamnyofoa viungo vyote maana yeye hupenda sana haya mambo ya kutoa takwimu.
Magazeti mumeyafungia hata sijui ipi ndio imesalia, dah halafu naskia mumeanza ukabila kabisa, kuna kabila mnaonyesha human face wakati wa ubomoaji.
Hilo la kutokua na ukabila mulikua mumetupiga bao, japo ulikuwepo lakini sio kwa kiwango cha Kenya, ila siku hizi naona mnakuja kwa kasi. Kwenu ubaguzi ulikua tu kwenye dini, lakini duh...
Naona waziri Nyalandu ameshuka basi mwenyewe, ila bado hamuoni kuna tatizo sehemu, mnatunisha misuli na kutumia muda mwingi mkijadili demokrasia ya Kenya.
Ukitaka kumjua muulize Ndugai alimwita kwa makeke mpaka leo kimya hana majibu.Kuna tofauti ya kueleza takwimu na kuanza kudanganya kwa maksudi kwa manufaa ya kisiasa. Mtu anajaribu kudanganya hata vitu vilivyo wazi ili mradi apate mileage ya ki siasa. Ku endelea kubishana nae sana ni kuendekeza ujinga, acha akaielekeze mahakama hizo data amepikia wapi.
Tz kuna magezeti mengi zaidi ya Kenya, na kila siku yanafumuka mapya mengi tu. So usihadaike na magazeti ya chama.
Nyalanda ni mbwa koko, hana madhara na hajawahi kuwa na madhara katika siasa za Tz. Atakumbukwa kwa ufisadi na umalaya tu, hakuna sifa nyingine aliyonayo zaidi ya hizo. Hasira zake ni za kunyimwa uwaziri wala si kingine. Wameondoka wakubwa CCM itakuwa Nyalandu.