Upishi wa Biskuti za Tangawizi

Upishi wa Biskuti za Tangawizi

Jade_

Senior Member
Joined
Apr 19, 2015
Posts
122
Reaction score
214
Habari zenu wakuu, natumai mnaendelea vizuri. Jumamosi iliyopita niliwaletea mapishi ya wali, samaki wa nazi na mboga. Wiki hii nitapika Biskuti za Tangawizi.

Biskuti hizi zinaweza kuliwa na maji, chai, maziwa, kahawa, juisi nk. Usipomaliza kuzila muda huo unaweza kuzihifadhi kwenye kontena sehemu isiyo na jua.

Ukipenda kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.



Mahitaji ya Biskuti za Tangawizi
350g Unga wa Ngano
1 tsp (kijiko cha chai) Magadi Soda
2 tsp tangawizi ya unga
115g siagi
175g sukari
4 tbsp (kijiko cha chakula) Golden Syrup
1 yai lililopigwa

Tunaanza kwa kuchekecha unga, magadi soda na tangawizi kwenye bakuli.

Pic 01.jpg

Unga wa ngano

Pic 02.jpg
Magadi Soda

Pic 03.jpg

Tangawizi

Pic 04.jpg

Nikichekecha unga, magadi na tangawizi

Baada ya hapo unaweka siagi iliyolainika, na kuichanganya mpaka mchanganyiko ufanane na chenga za mkate. Tunamalizia mahitaji makavu kwa kuchanganyia sukari.
Pic 05.jpg

Siagi laini

Pic 06.jpg

Nikichanganyia siagi

Pic 07.jpg

Nikiweka sukari

Tunaweka Golden Syrup (hii nilinunua supermarket) na yai liliopigwa na kuukanda mchanganyiko wetu kwa muda kidogo.
Pic 08.jpg

Golden Syrup

Pic 09.jpg

Nikipiga yai

Pic 10.jpg

Nikikanda unga


Baada ya kukanda unga wetu, tunausukuma kama chapati na kukata vipande kwa maumbo mbalimbali.
Pic 11.jpg

Nikisukuma mchanganyiko wetu

Pic 12.jpg

Nikitumia kikombe cha bati kukata vipande

Pic 13.jpg

Maumbo ya duara

Pic 15.jpg

Nikikata umbo kama mtu

Baada ya hapo, tunachukua vipande vyetu na kuviweka kwenye tray lililopakwa mafuta au siagi kwa ajili ya kuoka.
Pic 14.jpg

Nikiweka vipande kwenye tray

Pic 16.jpg

Vipande vikiwa kwenye tray tayari kwa kuoka

Ukioka kwenye oven, biskuti zitatumia dakika 10-12 hadi ziive kwenye joto la 190 C. Muda utakaotumia kuoka utalingana na namna unavyopenda biskuti zako ziive. Mimi nimependa zangu ziive zaidi na zitakaa muda mrefu zaidi.
Pic 17.jpg

Biskuti zikiwa kwenye oven

Pic 18.jpg

Biskuti zikiwa zimeiva

Pic 19.jpg

Biskuti za tangawizi

Pic 20.jpg

Biskuti za Tangawizi kwa ukaribu

Pic 21.jpg

Biskuti ya tangawizi kwa ndani
 

Attachments

  • Pic 04.jpg
    Pic 04.jpg
    84.8 KB · Views: 74
Mimi huku Maneromango nazipataje?Nataka za 10 elfu
 
Aisee!? Ipo vizuri
Nanikitaka vibiskuti lain kama vya etisamo naviandaeje
 
Iyo mikono yako ilivyo misafi nimetamani kula ivyo vidude
 
Back
Top Bottom