Jade_
Senior Member
- Apr 19, 2015
- 122
- 214
Habari zenu wakuu, natumai mnaendelea vizuri. Jumamosi iliyopita niliwaletea mapishi ya wali, samaki wa nazi na mboga. Wiki hii nitapika Biskuti za Tangawizi.
Biskuti hizi zinaweza kuliwa na maji, chai, maziwa, kahawa, juisi nk. Usipomaliza kuzila muda huo unaweza kuzihifadhi kwenye kontena sehemu isiyo na jua.
Ukipenda kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.
Mahitaji ya Biskuti za Tangawizi
350g Unga wa Ngano
1 tsp (kijiko cha chai) Magadi Soda
2 tsp tangawizi ya unga
115g siagi
175g sukari
4 tbsp (kijiko cha chakula) Golden Syrup
1 yai lililopigwa
Tunaanza kwa kuchekecha unga, magadi soda na tangawizi kwenye bakuli.
Unga wa ngano
Magadi Soda
Tangawizi
Nikichekecha unga, magadi na tangawizi
Baada ya hapo unaweka siagi iliyolainika, na kuichanganya mpaka mchanganyiko ufanane na chenga za mkate. Tunamalizia mahitaji makavu kwa kuchanganyia sukari.
Siagi laini
Nikichanganyia siagi
Nikiweka sukari
Tunaweka Golden Syrup (hii nilinunua supermarket) na yai liliopigwa na kuukanda mchanganyiko wetu kwa muda kidogo.
Golden Syrup
Nikipiga yai
Nikikanda unga
Baada ya kukanda unga wetu, tunausukuma kama chapati na kukata vipande kwa maumbo mbalimbali.
Nikisukuma mchanganyiko wetu
Nikitumia kikombe cha bati kukata vipande
Maumbo ya duara
Nikikata umbo kama mtu
Baada ya hapo, tunachukua vipande vyetu na kuviweka kwenye tray lililopakwa mafuta au siagi kwa ajili ya kuoka.
Nikiweka vipande kwenye tray
Vipande vikiwa kwenye tray tayari kwa kuoka
Ukioka kwenye oven, biskuti zitatumia dakika 10-12 hadi ziive kwenye joto la 190 C. Muda utakaotumia kuoka utalingana na namna unavyopenda biskuti zako ziive. Mimi nimependa zangu ziive zaidi na zitakaa muda mrefu zaidi.
Biskuti zikiwa kwenye oven
Biskuti zikiwa zimeiva
Biskuti za tangawizi
Biskuti za Tangawizi kwa ukaribu
Biskuti ya tangawizi kwa ndani
Biskuti hizi zinaweza kuliwa na maji, chai, maziwa, kahawa, juisi nk. Usipomaliza kuzila muda huo unaweza kuzihifadhi kwenye kontena sehemu isiyo na jua.
Ukipenda kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.
Mahitaji ya Biskuti za Tangawizi
350g Unga wa Ngano
1 tsp (kijiko cha chai) Magadi Soda
2 tsp tangawizi ya unga
115g siagi
175g sukari
4 tbsp (kijiko cha chakula) Golden Syrup
1 yai lililopigwa
Tunaanza kwa kuchekecha unga, magadi soda na tangawizi kwenye bakuli.
Unga wa ngano
Tangawizi
Nikichekecha unga, magadi na tangawizi
Baada ya hapo unaweka siagi iliyolainika, na kuichanganya mpaka mchanganyiko ufanane na chenga za mkate. Tunamalizia mahitaji makavu kwa kuchanganyia sukari.
Siagi laini
Nikichanganyia siagi
Nikiweka sukari
Tunaweka Golden Syrup (hii nilinunua supermarket) na yai liliopigwa na kuukanda mchanganyiko wetu kwa muda kidogo.
Golden Syrup
Nikipiga yai
Nikikanda unga
Baada ya kukanda unga wetu, tunausukuma kama chapati na kukata vipande kwa maumbo mbalimbali.
Nikisukuma mchanganyiko wetu
Nikitumia kikombe cha bati kukata vipande
Maumbo ya duara
Nikikata umbo kama mtu
Baada ya hapo, tunachukua vipande vyetu na kuviweka kwenye tray lililopakwa mafuta au siagi kwa ajili ya kuoka.
Nikiweka vipande kwenye tray
Vipande vikiwa kwenye tray tayari kwa kuoka
Ukioka kwenye oven, biskuti zitatumia dakika 10-12 hadi ziive kwenye joto la 190 C. Muda utakaotumia kuoka utalingana na namna unavyopenda biskuti zako ziive. Mimi nimependa zangu ziive zaidi na zitakaa muda mrefu zaidi.
Biskuti zikiwa kwenye oven
Biskuti zikiwa zimeiva
Biskuti za tangawizi
Biskuti za Tangawizi kwa ukaribu
Biskuti ya tangawizi kwa ndani