Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unajua kutengeneza kashata?tuwekee basiThank you.
Yasitokee tu mangumbaru yakaanza kusema eti una mikono mizuri...
Habari zenu wakuu, natumai mnaendelea vizuri. Jumamosi iliyopita niliwaletea mapishi ya wali, samaki wa nazi na mboga. Wiki hii nitapika Biskuti za Tangawizi.
Biskuti hizi zinaweza kuliwa na maji, chai, maziwa, kahawa, juisi nk. Usipomaliza kuzila muda huo unaweza kuzihifadhi kwenye kontena sehemu isiyo na jua.
Ukipenda kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.
Mahitaji ya Biskuti za Tangawizi
350g Unga wa Ngano
1 tsp (kijiko cha chai) Magadi Soda
2 tsp tangawizi ya unga
115g siagi
175g sukari
4 tbsp (kijiko cha chakula) Golden Syrup
1 yai lililopigwa
Tunaanza kwa kuchekecha unga, magadi soda na tangawizi kwenye bakuli.
View attachment 2480746
Unga wa ngano
View attachment 2480747Magadi Soda
View attachment 2480748
Tangawizi
View attachment 2480750
Nikichekecha unga, magadi na tangawizi
Baada ya hapo unaweka siagi iliyolainika, na kuichanganya mpaka mchanganyiko ufanane na chenga za mkate. Tunamalizia mahitaji makavu kwa kuchanganyia sukari.
View attachment 2480751
Siagi laini
View attachment 2480752
Nikichanganyia siagi
View attachment 2480753
Nikiweka sukari
Tunaweka Golden Syrup (hii nilinunua supermarket) na yai liliopigwa na kuukanda mchanganyiko wetu kwa muda kidogo.
View attachment 2480755
Golden Syrup
View attachment 2480758
Nikipiga yai
View attachment 2480759
Nikikanda unga
Baada ya kukanda unga wetu, tunausukuma kama chapati na kukata vipande kwa maumbo mbalimbali.
View attachment 2480760
Nikisukuma mchanganyiko wetu
View attachment 2480762
Nikitumia kikombe cha bati kukata vipande
View attachment 2480765
Maumbo ya duara
View attachment 2480766
Nikikata umbo kama mtu
Baada ya hapo, tunachukua vipande vyetu na kuviweka kwenye tray lililopakwa mafuta au siagi kwa ajili ya kuoka.
View attachment 2480767
Nikiweka vipande kwenye tray
View attachment 2480768
Vipande vikiwa kwenye tray tayari kwa kuoka
Ukioka kwenye oven, biskuti zitatumia dakika 10-12 hadi ziive kwenye joto la 190 C. Muda utakaotumia kuoka utalingana na namna unavyopenda biskuti zako ziive. Mimi nimependa zangu ziive zaidi na zitakaa muda mrefu zaidi.
View attachment 2480769
Biskuti zikiwa kwenye oven
View attachment 2480770
Biskuti zikiwa zimeiva
View attachment 2480771
Biskuti za tangawizi
View attachment 2480772
Biskuti za Tangawizi kwa ukaribu
View attachment 2480773
Biskuti ya tangawizi kwa ndani
Ahsante sana.View attachment 2534998
Mi tayari
Swali zuri. Badala ya kutumia golden syrup, unaweza kuyeyusha sukari na maji kwenye moto.View attachment 2603528
Ni lazima kutumia hiyo golden syrup? na inasaidia nini katika mapishi ya biscuits?