Jade_
Senior Member
- Apr 19, 2015
- 122
- 214
Habari za Jumamosi wakuu, natumai mpo salama. Leo nawaletea mapishi ya wali, samaki wa nazi na mboga.
Ukipenda kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.
Turudi kwenye mapishi yetu.
Wali
Nimeanza kwa kuchambua na kuosha mchele. Nimetumia mchele wa kawaida, sijatumia basmati kwa sababu siupendi kwa kutokua na harufi wala ladha yake yenyewe.
Kuchambua mchele
Kuosha mchele
Baada ya mchele kuwa safi nimeuweka kwenye sufuria na maji ya wastani. Nimetia mafuta, chumvi, nimekoroga na kuanza kuupika.
Mchanganyiko wa wali ukiwa jikoni
Baada ya muda maji yamekauka na wali wetu umeanza kuiva. Nimeugeuza ili uive kote na nimeongeza maji ya moto kidogo sana ili mvuke uusaidie wali kuiva. Nimefunikia mpaka umeiva kabisa.
Nikigeuza wali wangu
Nikiongeza maji kidogo sana ya moto
Wali ukiwa tayari
Samaki
Samaki aina ya sato
Nimemtayarisha samaki aina ya sato kwa kukwangua magamba yake, kuondoa mapezi (wengine wanayaacha au wanayatoa na kuyakaanga pembeni) na ute kwenye kichwa.
Nikikwangua magamba ya samaki
Nikiondoa mapezi na ute
Samaki akiwa msafi
Baada ya hapo samaki wangu nimempaka chumvi ya kutosha na kumkaanga kwenye mafuta kidogo yaliyopata moto hasa. Baada ya muda nimegeuza vipande vyangu vya samaki mpaka vimeiva vizuri. Nimetoa samaki jikoni na kuweka pembeni
Nikipaka vipande vya samaki chumvi
Naanza kukaanga samaki kwenye mafuta kidogo
Nikigeuza samaki
Samaki zimeiva
Nimeanza maandalizi ya mchuzi wa samaki kwa kukatakata vitunguu na nyanya
Nikikata nyanya na vitunguu
Kwenye kile chombo nilichokaangia samaki nimeanza kukaanga vitunguu. Baada ya kupata rangi kidogo nimeweka chumvi na kitunguu saumu na kukaanga kwa muda kidogo.
Nikikaanga vitunguu
Nikiweka kitunguu saumu
Baada ya hapo nimeweka nyanya na kuziacha mpaka zimelainika kabisa na kuwa mchuzi. Nimehamishia mchuzi wangu kwenye sufuria nyingine ili inirahisishie mapishi.
Nimeongezea nyanya kwenye vitunguu
Mchuzi wangu ukiwa tayari na kwenye sufuria nyingine
Nimekorogea tui la nazi taratibu kwenye mchuzi na nimeendelea kukoroga mpaka umechemka. Ulivyochemka, nimeweka vipande vya samaki nilivyokaanga na nimekamulia limao. Nimeacha imechemka kidogo ndio nikatoa jikoni.
Nikikorogea tui la nazi kwenye mchuzi wangu
Nikiweka vipande vya samaki vilivyokaangwa kwenye mchuzi
Nikikamulia limao
Mchuzi ukiwa tayari
Mboga
Kwa pishi la leo mboga tunazotumia ni mchanganyiko wa “chinese” na “spinach”. Unazikatakata na kuzichanganya kwenye sufuria pamoja na mafuta.
Nikikatakata mboga
Mboga zikiwa jikoni
Zikianza kuiva katia kitunguu na ukorogee kwenye mboga pamoja na chumvi. Acha mchanganyiko ukae jikoni mpaka vitunguu viive kidogo alfu utoe motoni.
Mboga na vitunguu jikoni
Mboga ikiwa tayari
Upakuaji
Nikipakua wali kwenye sahani
Nikiweka samaki na mchuzi wake juu ya wali
Nikiweka mboga kwenye sahani
Ukipenda kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.
Turudi kwenye mapishi yetu.
Wali
Nimeanza kwa kuchambua na kuosha mchele. Nimetumia mchele wa kawaida, sijatumia basmati kwa sababu siupendi kwa kutokua na harufi wala ladha yake yenyewe.
Kuchambua mchele
Kuosha mchele
Baada ya mchele kuwa safi nimeuweka kwenye sufuria na maji ya wastani. Nimetia mafuta, chumvi, nimekoroga na kuanza kuupika.
Mchanganyiko wa wali ukiwa jikoni
Baada ya muda maji yamekauka na wali wetu umeanza kuiva. Nimeugeuza ili uive kote na nimeongeza maji ya moto kidogo sana ili mvuke uusaidie wali kuiva. Nimefunikia mpaka umeiva kabisa.
Nikigeuza wali wangu
Nikiongeza maji kidogo sana ya moto
Wali ukiwa tayari
Samaki
Samaki aina ya sato
Nimemtayarisha samaki aina ya sato kwa kukwangua magamba yake, kuondoa mapezi (wengine wanayaacha au wanayatoa na kuyakaanga pembeni) na ute kwenye kichwa.
Nikikwangua magamba ya samaki
Nikiondoa mapezi na ute
Samaki akiwa msafi
Baada ya hapo samaki wangu nimempaka chumvi ya kutosha na kumkaanga kwenye mafuta kidogo yaliyopata moto hasa. Baada ya muda nimegeuza vipande vyangu vya samaki mpaka vimeiva vizuri. Nimetoa samaki jikoni na kuweka pembeni
Nikipaka vipande vya samaki chumvi
Naanza kukaanga samaki kwenye mafuta kidogo
Nikigeuza samaki
Samaki zimeiva
Nimeanza maandalizi ya mchuzi wa samaki kwa kukatakata vitunguu na nyanya
Nikikata nyanya na vitunguu
Kwenye kile chombo nilichokaangia samaki nimeanza kukaanga vitunguu. Baada ya kupata rangi kidogo nimeweka chumvi na kitunguu saumu na kukaanga kwa muda kidogo.
Nikikaanga vitunguu
Nikiweka kitunguu saumu
Baada ya hapo nimeweka nyanya na kuziacha mpaka zimelainika kabisa na kuwa mchuzi. Nimehamishia mchuzi wangu kwenye sufuria nyingine ili inirahisishie mapishi.
Nimeongezea nyanya kwenye vitunguu
Mchuzi wangu ukiwa tayari na kwenye sufuria nyingine
Nimekorogea tui la nazi taratibu kwenye mchuzi na nimeendelea kukoroga mpaka umechemka. Ulivyochemka, nimeweka vipande vya samaki nilivyokaanga na nimekamulia limao. Nimeacha imechemka kidogo ndio nikatoa jikoni.
Nikikorogea tui la nazi kwenye mchuzi wangu
Nikiweka vipande vya samaki vilivyokaangwa kwenye mchuzi
Nikikamulia limao
Mchuzi ukiwa tayari
Mboga
Kwa pishi la leo mboga tunazotumia ni mchanganyiko wa “chinese” na “spinach”. Unazikatakata na kuzichanganya kwenye sufuria pamoja na mafuta.
Nikikatakata mboga
Mboga zikiwa jikoni
Zikianza kuiva katia kitunguu na ukorogee kwenye mboga pamoja na chumvi. Acha mchanganyiko ukae jikoni mpaka vitunguu viive kidogo alfu utoe motoni.
Mboga na vitunguu jikoni
Mboga ikiwa tayari
Upakuaji
Nikipakua wali kwenye sahani
Nikiweka samaki na mchuzi wake juu ya wali
Nikiweka mboga kwenye sahani