Upishi wa Wali, Samaki wa Nazi na Mboga

Upishi wa Wali, Samaki wa Nazi na Mboga

Jade_

Senior Member
Joined
Apr 19, 2015
Posts
122
Reaction score
214
Habari za Jumamosi wakuu, natumai mpo salama. Leo nawaletea mapishi ya wali, samaki wa nazi na mboga.

Ukipenda kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.

Turudi kwenye mapishi yetu.

Wali
Nimeanza kwa kuchambua na kuosha mchele. Nimetumia mchele wa kawaida, sijatumia basmati kwa sababu siupendi kwa kutokua na harufi wala ladha yake yenyewe.

Pic 01.jpg

Kuchambua mchele

Pic 02.jpg

Kuosha mchele


Baada ya mchele kuwa safi nimeuweka kwenye sufuria na maji ya wastani. Nimetia mafuta, chumvi, nimekoroga na kuanza kuupika.

Pic 03.jpg

Mchanganyiko wa wali ukiwa jikoni

Baada ya muda maji yamekauka na wali wetu umeanza kuiva. Nimeugeuza ili uive kote na nimeongeza maji ya moto kidogo sana ili mvuke uusaidie wali kuiva. Nimefunikia mpaka umeiva kabisa.

Pic 04.jpg

Nikigeuza wali wangu

Pic 05.jpg


Nikiongeza maji kidogo sana ya moto

Pic 32.jpg

Wali ukiwa tayari



Samaki
Pic 06.jpg

Samaki aina ya sato


Nimemtayarisha samaki aina ya sato kwa kukwangua magamba yake, kuondoa mapezi (wengine wanayaacha au wanayatoa na kuyakaanga pembeni) na ute kwenye kichwa.

Pic 07.jpg

Nikikwangua magamba ya samaki

Pic 08.jpg

Nikiondoa mapezi na ute

Pic 09.jpg

Samaki akiwa msafi

Baada ya hapo samaki wangu nimempaka chumvi ya kutosha na kumkaanga kwenye mafuta kidogo yaliyopata moto hasa. Baada ya muda nimegeuza vipande vyangu vya samaki mpaka vimeiva vizuri. Nimetoa samaki jikoni na kuweka pembeni

Pic 10.jpg

Nikipaka vipande vya samaki chumvi

Pic 11.jpg

Naanza kukaanga samaki kwenye mafuta kidogo

Pic 12.jpg

Nikigeuza samaki

Pic 13.jpg

Samaki zimeiva


Nimeanza maandalizi ya mchuzi wa samaki kwa kukatakata vitunguu na nyanya
Pic 14.jpg

Nikikata nyanya na vitunguu


Kwenye kile chombo nilichokaangia samaki nimeanza kukaanga vitunguu. Baada ya kupata rangi kidogo nimeweka chumvi na kitunguu saumu na kukaanga kwa muda kidogo.
Pic 15.jpg

Nikikaanga vitunguu

Pic 16.jpg

Nikiweka kitunguu saumu


Baada ya hapo nimeweka nyanya na kuziacha mpaka zimelainika kabisa na kuwa mchuzi. Nimehamishia mchuzi wangu kwenye sufuria nyingine ili inirahisishie mapishi.
Pic 17.jpg

Nimeongezea nyanya kwenye vitunguu

Pic 18.jpg

Mchuzi wangu ukiwa tayari na kwenye sufuria nyingine

Nimekorogea tui la nazi taratibu kwenye mchuzi na nimeendelea kukoroga mpaka umechemka. Ulivyochemka, nimeweka vipande vya samaki nilivyokaanga na nimekamulia limao. Nimeacha imechemka kidogo ndio nikatoa jikoni.
Pic 19.jpg

Nikikorogea tui la nazi kwenye mchuzi wangu

Pic 20.jpg

Nikiweka vipande vya samaki vilivyokaangwa kwenye mchuzi

Pic 21.jpg

Nikikamulia limao

Pic 33.jpg

Mchuzi ukiwa tayari


Mboga

Kwa pishi la leo mboga tunazotumia ni mchanganyiko wa “chinese” na “spinach”. Unazikatakata na kuzichanganya kwenye sufuria pamoja na mafuta.
Pic 22.jpg

Nikikatakata mboga

Pic 23.jpg

Mboga zikiwa jikoni



Zikianza kuiva katia kitunguu na ukorogee kwenye mboga pamoja na chumvi. Acha mchanganyiko ukae jikoni mpaka vitunguu viive kidogo alfu utoe motoni.
Pic 24.jpg

Mboga na vitunguu jikoni

Pic 25.jpg

Mboga ikiwa tayari


Upakuaji
Pic 26.jpg

Nikipakua wali kwenye sahani

Pic 27.jpg

Nikiweka samaki na mchuzi wake juu ya wali

Pic 28.jpg

Nikiweka mboga kwenye sahani
 
Ila lakini anayekata mboga za majani na anayepakua wali ni watu tofauti. How hapo?
Macho yako kama yangu. Nadhani ni bibi na mjukuu wanafanya mapishi.

Kongole kwao
 
All in all chakula kinaonyesha ni kitamu, usafi umezingatiwa...
Binafsi ni mpenzi wa kupikia nazi, hapo umenifikisha.. hongera
 
Kwa huu uzi na mida hii, tayari nishasikia njaa ngoja nitoke sasa nikatafute msosi
 
Hongera sana , nimepata hamu ghafla. Bila shaka faza hausi anafurahia sana mapishi ya nyumbani kwake.
 
Back
Top Bottom