Uponyaji wa Msongo wa Mawazo na Upweke au Kukata Tamaa

Uponyaji wa Msongo wa Mawazo na Upweke au Kukata Tamaa

Gwappo Mwakatobe

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2019
Posts
1,730
Reaction score
2,230
Natoa ushauri kwa mtu yeyote aliye katika hali ya kupitia machungu (bitterness), kutelekezwa au kukataliwa (rejection), msongo wa mawazo (stress) au mfadhaiko/upweke (depression), aanze kufanya au kufikiria lolote lililo zuri, lolote lililo safi, lolote lenye haki, lolote lenye staha, lolote lenye sifa njema, lolote lenye ukweli, lolote lenye kupendeza na lolote lenye heshima.

Inaweza kuwa ni kufanya usafi, kusikiliza nyimbo au muziki aupendao, kufanya mazoezi au kutembelea mandhari nzuri kama milima, misitu au fukwe. Aidha, atazame picha, michezo au filamu anazopenda, au aangalie ndege na wanyama wampendezao. Ila yote hayo yanatuliza tu machungu kwa muda mfupi sana. Ni suluhisho la muda mfupi.

Kwa suluhisho la kudumu, anza kumshukuru Mungu kwa kukupa uhai na uzima ulionao sasa, ambapo unapumua vizuri wakati wengine wamelazwa hospitalini au wameishakufa. Mungu kakuongezea siku ya leo ili utimize kusudi lake alilokuleta duniani, ikiwemo kumwabudu Yeye pekee katika roho na kweli.

Baada ya hapo, tubu kwa Mungu makosa yako na tubu kwa uliowakosea kama wapo karibu au unaoweza kuwasiliana nao. Aidha, malizia kwa kuwasamehe wote waliokukosea.

Kisha, kwa kumaanisha moyoni mwako popote ulipo sema hivi: "Yesu Kristo karibu moyoni mwangu uniokoe niwe mwana wa Mungu kwa kuzaliwa upya rohoni na kuongozwa na Roho Mtakatifu." Amani utakayoipata moyoni mwako ni ya pekee sana! Mpe Mungu utukufu, sifa, heshima na shukrani.
 
Kisha, kwa kumaanisha moyoni mwako popote ulipo sema hivi: "Yesu Kristo karibu moyoni mwangu uniokoe niwe mwana wa Mungu kwa kuzaliwa upya rohoni na kuongozwa na Roho Mtakatifu." Amani utakayoipata moyoni mwako ni ya pekee sana! Mpe Mungu utukufu, sifa, heshima na shukrani.[emoji1545][emoji817][emoji818][emoji1752]
 
Kisha, kwa kumaanisha moyoni mwako popote ulipo sema hivi: "Yesu Kristo karibu moyoni mwangu uniokoe niwe mwana wa Mungu kwa kuzaliwa upya rohoni na kuongozwa na Roho Mtakatifu." Amani utakayoipata moyoni mwako ni ya pekee sana! Mpe Mungu utukufu, sifa, heshima na shukrani.[emoji1545][emoji817][emoji818][emoji1752]
Natamani sana wenye matatizo kama haya watembelee kule kwetu milimani Lushoto, Amani na/au Magoloto (Muheza). Pia waangalie picha zako za maeneo ya asili unazopost humu. Mpaka miti inapeana busu! Raha kabisa, japo ni suluhisho la muda mfupi.
 
Natamani sana wenye matatizo kama haya watembelee kule kwetu milimani Lushoto, Amani na/au Magoloto (Muheza). Pia waangalie picha zako za maeneo ya asili unazopost humu. Mpaka miti inapeana busu! Raha kabisa, japo ni suluhisho la muda mfupi.
Natamani pia bro! Kuna hijja pia milima ya Same ni sehemu nzuri sana za kufanya tafakuri
 
The following are the techniques

Cooperative techniques

Guidance and Cancelling (this proved to be more effective)

Working hard as you said

Reading Books
[Guidance and Cancelling (this proved to be more effective).
Working hard as you said.
Reading Books]

Truly said, thanks!
 
Yesu Kristo karibu moyoni mwangu uniokoe niwe mwana wa Mungu kwa kuzaliwa upya rohoni na kuongozwa na Roho Mtakatifu."🙏🙏😔
 
Natamani pia bro! Kuna hijja pia milima ya Same ni sehemu nzuri sana za kufanya tafakuri
Haswaaah! Ukitoka kule unarudi mpya uliyejaa furaha tele na amani ya ajabu. Kwenye uasili (nature) kuna Uponyaji wa ajabu. Unatamani usirudi tena mijini!
 
Back
Top Bottom