Mkuu Invicible ni makampuni ya IPP Media yanayoongoza kuandika habari zozote zenye lengo la kumbabua BWM, ushahidi uko wazi na pia hata yale ambayo Mengi ana hisa agenda ni hiyhiyo!!! Soma This day au Kulikoni , Nenda the Guardian, Nipashe,Acha Umbea na hata ya michezo, Ni Lete Raha lililoendesha kampeni ya kupinga Uwanja mpya usiitwe kwa jina la Mkapa mpaka wakathubutu kupendekeza uitwe Jakaya M.Kikwete, tunayaangalia magazeti haya kwa macho ya fadhaa maana sasa hata Pimbi anatambua mchezo unaofanyika.
Ninakutaka ufanye uchunguzi wako, IPP Media wanavyoziripoti habari za viongozi wa Umma wa Tz inapofika Mkapa tatizo kwelikweli na ndio maana kuna siku nilihoji JF iweje hawa jamaa wa IPP Media habari iwe ni Mkapa pale inapozungumzia yale wanayoona na mabaya yake?!! Lakini inapokuja dunia na umma ku acknowledge mchango wako they don't want to be part of it?!!!! Kumbuka kilichotokea National Stadium(The New Arena) , kwa makusudi IPP walianza kampeni za kuwaonyesha viongozi wa sasa kila mara lakini wale wachina wakaamua kuiwasha ile Runinga pale ndani ikimuonyesha Ben Netanyahu Mkapa uwanja uliripuka kama kuna goli limeingia kimiani, wao hawakuonyesha hicho kitu live siku ile mpaka siku ya pili tuliposoma baadhi ya magazeti kuwa wananchi walisahau machungu ya game mara baada ya kuonyeshwa mzee Netanyahu akikagua uwanja wakati wa mapumziko.
Ninaanza kuamini kuwa ushirika wa Msuya na Mengi na harakati za kujipendekeza kwao kwa utawala mpya ni chanzo cha yote yanayompata Mkapa, hakukosea kuwa wagomvi wake ni pamoja na wale aliwanyima mamlaka zama za utawala wake.
Invicible, Mengi anao mkono juu ya haya yanayotendwa na waajiriwa wake dhidi ya Ben Netanyahu, usipoteze muda wako kumtetea huyu tajiri kwani umma unamuangalia kwa jicho la kisirani kwa mahubiri yake na matendo yake, tulisha hoji iweje huyu afananishwe na Martin Luther King Jr, tuliongea mengi humu JF.
Mzee Mramba alichosema ni sahihi kabisa na wala hakulenga kumponda mtu wala chama chake bali ni kujiuliza kama Mtz, ameongea kwa ufasaha ,kwa dhati ya moyo wake na zaidi ametoa changamoto. Muandishi anapoamua kupotosha ,Muhariri anapokubaliana na Mmiliki anapokaa kimya bila kuchukua hatua za makusudi kurejesha imani na heshima ya mali zake unataka tusimuhoji?!!!
Mkuu black and white IPP Media ni tatizo kwa maendeleo ya habari Tz, tunamlaumu sana Rostam why?? Ni pale tunapoona media zake zinapotosha umma, why not Mengi? Ni mungu huyu au?
Alichotaka ktk kipindi cha Mkapa na kukikosa sasa amekipata kwa JK, tunamuona yuko karibu naye sana ingawaje jamii haipendezwi na hali hiyo lakini maamuzi ya Rais na tunayaheshimu, mzee wake Msuya naye kasogezwa basi inatosha kwake ,ajenge nchi na siyo malumbano yaso na hoja.
Hofu yake nini kwa Mkapa ambaye sasa si Rais wa nchi au anataka nini toka kwa huyu mzee? Issue hii Mkuu invisible inawakera wananchi wengi sana na kwa dhati ninaamini inaipotosha nchi maana umma hautaki kukubaliana na huu mchezo na muda unakwenda wakati mambo ya muhimu hayazungumzwi na tunamjadili mtu tena kwa pesa za nchi yetu.
Imetosha wakuu, sasa wahariri jaribuni kuheshimu taaluma zenu na mkumbuke tu kuwa mnayemkejeli aliwashawatabiri kuwa uwezo wenu ni mdogo sana ktk kuchambua mambo na mmeamua kumthibitishia kuwa hamnazo, Shame on you!!!!!!
Mkuu Invicible mpaka sasa ktk ugumu huu wa kipato kuna wakati bado huwa najitahidi kununua Mwanahalisi, Raia Mwema,Rai na Tz Daima Jtano-Jpili maana kidogo hapo ninalo la kujifunza, hata kama wanamuandika Ben Netanyahu hawa jamaa wako reasonable kwa msomaji wao.
Mkuu ni maoni yangu juu ya thread hii na IPP Media, ruksa kupingana kwa hoja.
Mungu awabariki sana.