Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Jambo Sana!
Wakati wengine wakibadilisha Maisha Yao Kwa dakika tano Kwa kubet, Mimi nilikuwa napiga doria katika account za mitandao ya kijamii huko Pm na inbobo nikivizia mawindo. Wengine wengi wakijaribu kuyabadilisha Maisha Yao Kwa kulima Kilimo cha machenza, Mimi nilikuwa nachenza na michenzo ya kuchenzea mafutunzo. Doooh! Samaleko!
Upwiru wenye kunyima Uhuru. Ukanifanya nikakufuru. Ila ni tamu! Tena inanoga! Raha yake macho kufumba. Anyway let me now tell you what that face me tit4tat.
Upwiru haukuwa na adabu. Ukanikaba bila sababu. Huyo kiguu na njia, nikatokea labda useme Amazonia, Huko kwenye soko la Makedonia, naambiwa ni mtandao pendwa wa wenye upwiru. Huko ndiko niliko kutana na mrembo ambaye Sifa zake ziliandikwa katika vitabu vya Peponi.
Tena katika Sura ya ashura katika kitabu kile kilimchora Mwanamke mmoja mwenye umbo la namba kamilifu yenye kugawanyika Kwa mbili katika kila namba. Mimi nilisoma zamani kidogo, zipo namba shufwa, witiri na tasa. Tena nikaambiwa kuwa zipo namba zisizogawanyika Kwa mbili na kama zingegawanyika basi ingebaki moja. Lakini umbo la Yule Mwanamke lilibeba namba kamilifu ambayo hata ingegawanywa Kwa witiri au tasa bado ingegawanyika bila utata.
Akitembea akitisa moja itatikisika Kwa namba shufwa. Tikisa moja tikisika mara mbili au nne. Yaani ndii! Kisha ndindindindi! Kudadadadeki! Hapo ndipo nilipojichanganya. Si unajua wengine hesabu tulimchukia kama Nduli Idi amini adui yake Baba.
Yule mrembo macho yake yalikuwa yanarembua na kuakisi kama prizimu, alikuwa ananitesa kisayansi na kunimaliza kiteknolojia. Kisha ananikonga kisarufi na kunikoroga kifasihi.
Baada ya kusoma apendex one tukasaini na kukubaliana. Ati tunapendana pasipo kujuana. Upwiru Noma! Nani anataka kumjua Nani hapa! Mimi sio karani.
Nikapiga mbiu, akaitikia la mgambo. Gwanda mwilini, risasi chomboni. Nikamtwanga akatwangika. Alia kama toto, achekelea kama kibiriti Ngoma, macho kayalegeza akiwa kayageuza juu kama yuaaga Dunia. Kumbe madoido ya Binti nyangwena.
Mikunjo anakunjua na kupiga tiktaka kama ibrahimovic, mikato anaikata huku akipiga mikasi duarani Kama C7. Baadaye tukamaliza pigo ungedhani Kiama. Bwi!bwi! Bwi! Mamamamaweee! Anabwinya na kubana kama nisingekufa siku Ile basi siku yangu ya Kufa ili pita kama kile kitabu cha Taikon Master, nina uhakika siku Ile niliponea chupuchupu na ninahakika tena kuwa siku ambayo nitakutana naye tena ndio itakuwa siku ya Mauti yangu.
Mwezi ukapita, kichwa kinagonga kama kengele ya gereza la kuzimu alipofungwa Lusifa na Kaka yake Azazel.
Sijakaa vizuri Yule Mwanamke ananiambia ni mjamzito, nimempa mimba jinni Mimi. Wakwe zangu ni kina Subiani. Mahari yangu ni Damu.
Nikamwambia kichwa kinauma na kugonga Sana. Akanambia Dawa yake ni mpaka tuonane mara ya pili vinginevyo ninaweza kupatwa na makubwa zaidi.
🎶Ooh! Yamenikuta! Ooh! Upwiru umeniponza🎶
🎶 dakika tano tuu zimebadili Maisha yangu eeh🎶 (Sauti ya instrumental inalia parampapapa)
Niko Hapa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Wakati wengine wakibadilisha Maisha Yao Kwa dakika tano Kwa kubet, Mimi nilikuwa napiga doria katika account za mitandao ya kijamii huko Pm na inbobo nikivizia mawindo. Wengine wengi wakijaribu kuyabadilisha Maisha Yao Kwa kulima Kilimo cha machenza, Mimi nilikuwa nachenza na michenzo ya kuchenzea mafutunzo. Doooh! Samaleko!
Upwiru wenye kunyima Uhuru. Ukanifanya nikakufuru. Ila ni tamu! Tena inanoga! Raha yake macho kufumba. Anyway let me now tell you what that face me tit4tat.
Upwiru haukuwa na adabu. Ukanikaba bila sababu. Huyo kiguu na njia, nikatokea labda useme Amazonia, Huko kwenye soko la Makedonia, naambiwa ni mtandao pendwa wa wenye upwiru. Huko ndiko niliko kutana na mrembo ambaye Sifa zake ziliandikwa katika vitabu vya Peponi.
Tena katika Sura ya ashura katika kitabu kile kilimchora Mwanamke mmoja mwenye umbo la namba kamilifu yenye kugawanyika Kwa mbili katika kila namba. Mimi nilisoma zamani kidogo, zipo namba shufwa, witiri na tasa. Tena nikaambiwa kuwa zipo namba zisizogawanyika Kwa mbili na kama zingegawanyika basi ingebaki moja. Lakini umbo la Yule Mwanamke lilibeba namba kamilifu ambayo hata ingegawanywa Kwa witiri au tasa bado ingegawanyika bila utata.
Akitembea akitisa moja itatikisika Kwa namba shufwa. Tikisa moja tikisika mara mbili au nne. Yaani ndii! Kisha ndindindindi! Kudadadadeki! Hapo ndipo nilipojichanganya. Si unajua wengine hesabu tulimchukia kama Nduli Idi amini adui yake Baba.
Yule mrembo macho yake yalikuwa yanarembua na kuakisi kama prizimu, alikuwa ananitesa kisayansi na kunimaliza kiteknolojia. Kisha ananikonga kisarufi na kunikoroga kifasihi.
Baada ya kusoma apendex one tukasaini na kukubaliana. Ati tunapendana pasipo kujuana. Upwiru Noma! Nani anataka kumjua Nani hapa! Mimi sio karani.
Nikapiga mbiu, akaitikia la mgambo. Gwanda mwilini, risasi chomboni. Nikamtwanga akatwangika. Alia kama toto, achekelea kama kibiriti Ngoma, macho kayalegeza akiwa kayageuza juu kama yuaaga Dunia. Kumbe madoido ya Binti nyangwena.
Mikunjo anakunjua na kupiga tiktaka kama ibrahimovic, mikato anaikata huku akipiga mikasi duarani Kama C7. Baadaye tukamaliza pigo ungedhani Kiama. Bwi!bwi! Bwi! Mamamamaweee! Anabwinya na kubana kama nisingekufa siku Ile basi siku yangu ya Kufa ili pita kama kile kitabu cha Taikon Master, nina uhakika siku Ile niliponea chupuchupu na ninahakika tena kuwa siku ambayo nitakutana naye tena ndio itakuwa siku ya Mauti yangu.
Mwezi ukapita, kichwa kinagonga kama kengele ya gereza la kuzimu alipofungwa Lusifa na Kaka yake Azazel.
Sijakaa vizuri Yule Mwanamke ananiambia ni mjamzito, nimempa mimba jinni Mimi. Wakwe zangu ni kina Subiani. Mahari yangu ni Damu.
Nikamwambia kichwa kinauma na kugonga Sana. Akanambia Dawa yake ni mpaka tuonane mara ya pili vinginevyo ninaweza kupatwa na makubwa zaidi.
🎶Ooh! Yamenikuta! Ooh! Upwiru umeniponza🎶
🎶 dakika tano tuu zimebadili Maisha yangu eeh🎶 (Sauti ya instrumental inalia parampapapa)
Niko Hapa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam