Urais wa Kasim Majaliwa 2025 umempa Ukatibu Mkuu Kiongozi Dk. Bashiru Ally

Urais wa Kasim Majaliwa 2025 umempa Ukatibu Mkuu Kiongozi Dk. Bashiru Ally

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,377
Wanabodi tuwe tunaweka kumbukumbu pamoja na kusoma "between the lines" anapoandika mtu uzi wake. Tuongeze uwezo wa kutafakari na kudadisi ili kupata faida kuepuka ramli.

Siku za hivi karibuni nikiandika uzi humu ndani nikieleza kuwa Urais wa Kassim Majaliwa unasukwa na SG wa CCM Dk. Bashiru Ally lakini bila baraka za Mkulu ambaye amekuja kustukia. Nikasema kwamba Bashiru ukomo wake ni 2022 kwenye Uchaguzi Mkuu ndani ya Chama wanapopanga safu za uongozi. Nikadhani nilieleweka.

Kifo cha Balozi John Kijazi kikaleta ahueni katika kummaliza kisiasa Bashiru. "Adui msogeze ubavuni". Kwa sasa Bashiru hawezi tena kufanya harakati za siasa za kumwandaa Majaliwa. JPM ana akili sana. Kamtoa kwenye reli pamoja na kwamba aliwahi kusema, "sitogombea nafasi yoyote wala kukubali uteuzi WOWOTE" baada ya huu Ukatibu Mkuu wangu'.

Kifupi ni kwamba vita ya Urais 2025 inarindima ndani ya CCM na Serikali. Mitandao inaundwa kwa gharama kubwa. Yetu macho!!
 
Siasa bhana wengine busy kuandaa mtandao wa 2025, wengine Jpm aongezewe 5 tena. Hapo ataamua mwenyewe
 
Bado mkuu huwa vita za madaraka zinaanza mwaka wa tatu wa awamu ya pili ya Rais aliyepo madarakani.

Uchaguzi wa mwakani wa Chama ndio watu wanaanza kujipanga ndugu.
 
Bado mkuu huwa vita za madaraka zinaanza mwaka wa tatu wa awamu ya pili ya Rais aliyepo madarakani.

Uchaguzi wa mwakani wa Chama ndio watu wanaanza kujipanga ndugu.
Hapo unakosea. Mchakato wa Urais unaanza na kupanga Safu ndani ya Chama. Lengo hapa ni kuhakikisha mtu anapata uteuzi kuwakilisha chama. Ikumbukwe kwamba bado anayeteuliwa kupeperusha bendera ya Chama anauhakiki wa 100%. Hivyo wanapambana kuteuliwa na Chama baada ya hapo Party apparatuses zinatumika kumuingiza madarakani.
 
Wanabodi tuwe tunaweka kumbukumbu pamoja na kusoma "between the lines" anapoandika mtu uzi wake. Tuongeze uwezo wa kutafakari na kudadisi ili kupata faida kuepuka ramli.

Siku za hivi karibuni nikiandika uzi humu ndani nikieleza kuwa Urais wa Kassim Majaliwa unasukwa na SG wa CCM Dk. Bashiru Ally lakini bila baraka za Mkulu ambaye amekuja kustukia. Nikasema kwamba Bashiru ukomo wake ni 2022 kwenye Uchaguzi Mkuu ndani ya Chama wanapopanga safu za uongozi. Nikadhani nilieleweka.

Kifo cha Balozi John Kijazi kikaleta ahueni katika kummaliza kisiasa Bashiru. "Adui msogeze ubavuni". Kwa sasa Bashiru hawezi tena kufanya harakati za siasa za kumwandaa Majaliwa. JPM ana akili sana. Kamtoa kwenye reli pamoja na kwamba aliwahi kusema, "sitogombea nafasi yoyote wala kukubali uteuzi WOWOTE" baada ya huu Ukatibu Mkuu wangu'.

Kifupi ni kwamba vita ya Urais 2025 inarindima ndani ya CCM na Serikali. Mitandao inaundwa kwa gharama kubwa. Yetu macho!!
Kwani kuna shida gani Majaliwa kuwa Rais ?
 
Back
Top Bottom