Freed Freed
JF-Expert Member
- Jun 27, 2017
- 6,547
- 7,167
Habari JF Siasa,
Humu ndani kumekuwa na maoni au chapuo mbalimbali juu ya wagombea Urais Zanzibar. Kuna mmoja wetu humu jukwaani amekuwa wazi kwa kuwapa chapuo Dr Hussein Mwinyi na Prof Makame Mbarawa.
Naomba nami niseme ama kutoa maoni yangu kutoka moyoni Kama walivyofanya wengine.
Kwanza kabisa, Hamad Yusuf Masauni ni Mhandisi ktk nyanja ya ujenzi. Uhandisi ni taaluma muhimu Sana ktk ujenzi wa jamii imara. Mfano wa majengo, umeme, barabara, Reli nk. Miundo mbinu hii ni muhimu ktk kukuza uchumi katika taifa lolote lile duniani. Huenda Masauni akawa mlevi au akapenda zaidi miundo mbinu mbalimbali na hivyo kuipaisha Zanzibar kiuchumi.
Pili, Mheshimiwa Masauni amehudumu ktk wizara ya mambo ya ndani ya JMT kwa miaka mitano licha ya mawaziri watatu kutumbuliwa. Yeye amekuwa Naibu waziri kwa kipindi chote hicho na huenda akawa anawafundisha kazi mawaziri wapya wajao wizarani.
Tatu, Hamad Y. Masauni ni mtiifu mkubwa kwa Rais Magufuli ambaye ni bosi wake Sasa na hata atakapokuwa Rais ajaye Zanzibar. Inasemekana Masauni anamheshimu na pia kumuogopa Sana Rais Magufuli na hivyo hii itakuwa afya njema kwa Muungano.
Nne, Naibu waziri Masauni ni Mbabe kiasi fulani ikizingatiwa siasa za Zanzibar hazimuhitaji mtu mpole Sana kwani wale kina Yakhee watamnasa kibao usoni. Hata Rais shein ni mpole lakini ni mkali Sana ofisini na ndiyo maana Zanzibar imesonga ktk utawala wake.
Tano, Masauni anatoka Unguja na hivyo ili kuimarisha mashirikiano ya dhati Zanzibar, ni vyema Rais kipindi hiki ataloke Unguja kwa kuwa wa Sasa anatoka Pemba.
Sita, Masauni Yusuf ni kijana buheri wa afya na hivyo atahimili mikiki ya siasa za Sasa ambazo zahitaji vijana huku wazee wakiwa washauri wakuu.
Saba, Masauni Yusuf hana nasaba na familia za viongozi wakubwa huko Zanzibar. Sahivi kuna kelele juu ya kiimarika siasa za usultani au ufalme visiwani Zanzibar. Watu wanadai wanadai kumekuwa na tabia za familia za Marais wa zamani Zanzibar kujiona wao Wana uwezo zaidi ya wanafamilia wengine Wazanzibari ya kuiongoza Zanzibar. Zipo pia familia za mawaziri hapo kale kutoa wagombea wenye ujivuni wa kuiweza Zanzibar na sio wanafamilia wengine. Masauni hana nasaba hizi na atazizima kelele zinazopigwa hivi Sasa na Wazanzibari walio wengi.
Rais ajaye Zanzibar ni Hamad Yusuf Masauni na Zanzibar itashuhudia mabadiliko makubwa Sana kimaendeleo. Naamini muda sio mrefu uzi huu utafufuliwa.
Humu ndani kumekuwa na maoni au chapuo mbalimbali juu ya wagombea Urais Zanzibar. Kuna mmoja wetu humu jukwaani amekuwa wazi kwa kuwapa chapuo Dr Hussein Mwinyi na Prof Makame Mbarawa.
Naomba nami niseme ama kutoa maoni yangu kutoka moyoni Kama walivyofanya wengine.
Kwanza kabisa, Hamad Yusuf Masauni ni Mhandisi ktk nyanja ya ujenzi. Uhandisi ni taaluma muhimu Sana ktk ujenzi wa jamii imara. Mfano wa majengo, umeme, barabara, Reli nk. Miundo mbinu hii ni muhimu ktk kukuza uchumi katika taifa lolote lile duniani. Huenda Masauni akawa mlevi au akapenda zaidi miundo mbinu mbalimbali na hivyo kuipaisha Zanzibar kiuchumi.
Pili, Mheshimiwa Masauni amehudumu ktk wizara ya mambo ya ndani ya JMT kwa miaka mitano licha ya mawaziri watatu kutumbuliwa. Yeye amekuwa Naibu waziri kwa kipindi chote hicho na huenda akawa anawafundisha kazi mawaziri wapya wajao wizarani.
Tatu, Hamad Y. Masauni ni mtiifu mkubwa kwa Rais Magufuli ambaye ni bosi wake Sasa na hata atakapokuwa Rais ajaye Zanzibar. Inasemekana Masauni anamheshimu na pia kumuogopa Sana Rais Magufuli na hivyo hii itakuwa afya njema kwa Muungano.
Nne, Naibu waziri Masauni ni Mbabe kiasi fulani ikizingatiwa siasa za Zanzibar hazimuhitaji mtu mpole Sana kwani wale kina Yakhee watamnasa kibao usoni. Hata Rais shein ni mpole lakini ni mkali Sana ofisini na ndiyo maana Zanzibar imesonga ktk utawala wake.
Tano, Masauni anatoka Unguja na hivyo ili kuimarisha mashirikiano ya dhati Zanzibar, ni vyema Rais kipindi hiki ataloke Unguja kwa kuwa wa Sasa anatoka Pemba.
Sita, Masauni Yusuf ni kijana buheri wa afya na hivyo atahimili mikiki ya siasa za Sasa ambazo zahitaji vijana huku wazee wakiwa washauri wakuu.
Saba, Masauni Yusuf hana nasaba na familia za viongozi wakubwa huko Zanzibar. Sahivi kuna kelele juu ya kiimarika siasa za usultani au ufalme visiwani Zanzibar. Watu wanadai wanadai kumekuwa na tabia za familia za Marais wa zamani Zanzibar kujiona wao Wana uwezo zaidi ya wanafamilia wengine Wazanzibari ya kuiongoza Zanzibar. Zipo pia familia za mawaziri hapo kale kutoa wagombea wenye ujivuni wa kuiweza Zanzibar na sio wanafamilia wengine. Masauni hana nasaba hizi na atazizima kelele zinazopigwa hivi Sasa na Wazanzibari walio wengi.
Rais ajaye Zanzibar ni Hamad Yusuf Masauni na Zanzibar itashuhudia mabadiliko makubwa Sana kimaendeleo. Naamini muda sio mrefu uzi huu utafufuliwa.