Urinary Tract Infections ( UTIs) Imekuwa Janga

busy bees

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2016
Posts
2,249
Reaction score
1,340
Yawezekana ni tatizo la muda mrefu lakini kwa siku za hivi karibuni UTI imeonekana kuwa ni janga tena kubwa kwa wana wa kike hasahasa walo katika "teen age" ....

Mahali fulani shule ya sekondari .... ilionekana UTI kuwasumbua sana wanafunzi wa kike walokuwa bweni ... ikawa ni frequent routines za hospital .....

Wako wapi wataalamu wa magonjwa haya ya maambukizo ili kutoa angalizo ama maelekezo yatakayowasaidia hawa ndg zetu kuepukana na tatizo hili?

Nngeweza post JF doctor but nmeona ni vyema waso kule nao wapate elimu hii ..
 
Elimu itolewe kwa wananchi jinsi ya kujikinga na huo ugonjwa, tukianzia hapa JF.
JF imesheheni wataalamu na ni imani yangu watakuja na suluhisho la hili tatizo lionekanalo kuwa sugu na lenye kuwasumbua wengi
 
UTI inasababishwa na uchafu wa vyoo. hiyo shule itakuwa haihimizi suala la usafi wa vyoo.

watoto wa kike wanaathirika zaidi kwa kuwa hukojoa wakiwa wamechuchumaa tofauti na watoto wa kiume. hivyo mkojo unapogonga choo kichafu na kurukia sehemu zao za siri.

lkn pia watt wa kike wapewe elimu juu ya kuchamba kinyesi, kwani nacho ni kisababishi kikubwa. wanapochamba wawe wanavuta tissue kwenda nyuma na siyo mbele kwenye tamu.,

kwan kwenye kinyesi kuna vimelea vinavyopatikana kwenye kila tumbo la binadamu na ambavyo husababisha UTI
 
Vyoo vya public vinachangia sana kusambaza ugonjwa huu kwa wanawake. Kunywa maji mengi husaidia sana lakini kama bi dada nao ugonjwa huu na njemba wake ambao hupeana yale mambo matamu basi njemba naye inabidi atibiwe ili kuumaliza ugonjwa vinginevyo utakuwa unajirudia kila mara.

 
Well said mkuu,
 
Naamin wahusika watakuwa wamepata elimu juu ya chanzo na nn kifanyike
 
Reactions: BAK
Kwa sasa ukipereka mtoto Hospitar kupima marelia,lazima atapima na UTI...
 
UTI ni ugonjwa unaowapata watu ambao hawajali miili yao. PERIOD.
 
Wakazi wa Dar es salaam mnabambikwa ugonjwa huu na hasa hizi maabara na hospitali za uchochoroni, kibaya zaidi haohao jamaa wa maabara wanawaandikia na tiba wao wenyewe...."pawasef"(ceftriaxon). Yaani mdada anatibiwa UTI kila mwezi......

Ila pia hii pia inaweza kuwa sababu: jamani na hili joto la Dar MTU amepiga chupi, skin tight, na ka jeans tight na mbanano wa kwenye daladala joto huko ikulu na mijasho inachuruzika na kusomba wadudu kutoka njia ya haja kubwa kwenda njia ya haka ndogo.
 
Vyoo vya kisasa vya kuflash ni sababu ya ongezeko la tatizo la UTI hasa kwa wanawake. Zamani enzi za vyoo vya shimo UTI ilikuwa haijulikani kwani ilitokea kwa nadra sana. Lakini leo tatizo hili ni la kawaida sana. Elimu inahitajika ili kutunza usafi wa vyoo vya marumaru na kutunza sehemu za mwili ambazo zinapata maabukizi.
 
Watoto wa kike na wanawake kwa ujumla ndio wanaonekana hasa kuwa wahanga wa UTI kwa sababu ya maumbile ya sehemu za siri hasa wakati wa kujisaidia haja ndogo.
Katika shule za bording (goverment) na vyoo vya maeneo ya public huwa ni vichafu sana, hivyo kupelekea maambukizi ya gonjwa hili.
Kinachotakiwa kufanyika ili kupunguza maambukizi haya kwa wasichana na wanawake kwa ujumla kama ifuatavyo:
1. Kabla ya kujisaidia haja kubwa au ndogo hakikisha unasafisha choo kwa dawa za chooni au sabuni ya dettol itakayosaidia kuua vijidudu vilivyokuwepo tayari kwenye sinki la choo.
2. Unapomaliza kujisaidia, wakati wa kuchamba unatakiwa kuwa makini, anza kujisafisha ukeni baada ya hapo ndiyo usafishe na sehemu ya haja kubwa. Wengi wao hujiongeza maambukizi wenyewe kwani vijidudu vya UTI hukaa katika haja kubwa, kwa hiyo unapochamba kuanzia sehemu ya haja kubwa na kumalizia sehemu ya haja ndogo unakuwa umewahamisha wadudu hao kutoka kwenye kinyesi na kuwaruhusu waingie kwenye njia ya mkojo.
3. Pia unashauriwa kunywa maji safi na salama kwa wingi kwani kusaidia kuondoa tatizo hili kama halijawa kubwa.
Asanteni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…