Sexer
JF-Expert Member
- Oct 22, 2014
- 8,440
- 8,149
Urusi inapambana kudumisha kampeni yake ya kijeshi na Ukraine na inaweza kuwa na uwezo wa kujibu mashambulizi, mkuu wa idara ya kijasusi ya kigeni ya Uingereza amesema.
Mkuu wa MI6 Richard Moore alisema Urusi imeshuhudia"anguko la kihistoria" katika malengo yake ya awali ya kumwondoa rais wa Ukraine, kuichukua Kyiv na kuweka mgawanyiko katika nchi za Magharibi.
Ameyasema hayo wakati akizungumza katika Jukwaa la Usalama la Aspen, ambapo ni nadra sana kuonekana hadharani.
Aliita uvamizi huo "kitendo cha wazi zaidi cha uchokozi. kwa Ulaya tangu Vita vya Pili vya Dunia."
Alisema mafanikio ya hivi karibuni ya Urusi yalikuwa "madogo" na kwamba Urusi "inakaribia kuishiwa nguvu".
"Tathmini yetu ni kwamba Warusi watazidi kupata ugumu wa kupata nguvukazi na nyenzo katika wiki chache zijazo," Bw Moore alisema katikaa mkutano huko Colorado. "Watalazimika kusimama kwa namna fulani na hiyo itawapa Waukraine fursa ya kurudisha mashambulio."
Mtazamo huo unaweza kuonekana kuwa wa matumaini na uwezo wa Ukraine wa kukabiliana na mashambulizi unaweza kutegemea usambazaji mkubwa wa silaha za Magharibi ambazo maafisa wake wanasema mara nyingi umekuwa wa polepole sana kufika.
Mkuu wa MI6 alisema aina fulani ya mafanikio katika uwanja wa vita yatakuwa "ukumbusho muhimu kwa Ulaya yote kwamba hii ni kampeni ya kushinda" haswa kabla ya msimu wa baridi ambao kuna uwezekano wa kuona shinikizo kwenye usambazaji wa gesi.
"Tuko kwenye wakati mgumu," alisema. Sababu zaidi ya kudumisha uungwaji mkono kusaidia Waukraine kushinda au "angalau kujadiliana kuhusu nafasi yenye nguvu kubwa", alisema, ni kwa sababu kiongozi wa China Xi Jinping "alikuwa akitazama kama mwewe (kwa umakini)".
"Hakuna ushahidi kwamba [Rais Vladimir] Putin anasumbuliwa na tatizo la kiafya," alijibu alipoulizwa, akirejea maoni ya Mkurugenzi wa CIA William Burns katika Jukwaa hilo jana.
Takriban maafisa 400 wa ujasusi wa Urusi wanaofanya kazi kwa siri wamefukuzwa kote Ulaya, alisema, na kupunguza nusu ya uwezo wa Urusi wa kufanya ujasusi katika bara hilo.
"Mlango wetu uko wazi kila wakati," alisema linapokuja suala la kuajiri maafisa wa Urusi waliojitenga ili kupeleleza kwa ajili ya Uingereza.
NB: Katika kujifariji sisi warusi wa malinyi tucomment "Propaganda" sawa tumeelewana ee.
Mkuu wa MI6 Richard Moore alisema Urusi imeshuhudia"anguko la kihistoria" katika malengo yake ya awali ya kumwondoa rais wa Ukraine, kuichukua Kyiv na kuweka mgawanyiko katika nchi za Magharibi.
Ameyasema hayo wakati akizungumza katika Jukwaa la Usalama la Aspen, ambapo ni nadra sana kuonekana hadharani.
Aliita uvamizi huo "kitendo cha wazi zaidi cha uchokozi. kwa Ulaya tangu Vita vya Pili vya Dunia."
Alisema mafanikio ya hivi karibuni ya Urusi yalikuwa "madogo" na kwamba Urusi "inakaribia kuishiwa nguvu".
"Tathmini yetu ni kwamba Warusi watazidi kupata ugumu wa kupata nguvukazi na nyenzo katika wiki chache zijazo," Bw Moore alisema katikaa mkutano huko Colorado. "Watalazimika kusimama kwa namna fulani na hiyo itawapa Waukraine fursa ya kurudisha mashambulio."
Mtazamo huo unaweza kuonekana kuwa wa matumaini na uwezo wa Ukraine wa kukabiliana na mashambulizi unaweza kutegemea usambazaji mkubwa wa silaha za Magharibi ambazo maafisa wake wanasema mara nyingi umekuwa wa polepole sana kufika.
Mkuu wa MI6 alisema aina fulani ya mafanikio katika uwanja wa vita yatakuwa "ukumbusho muhimu kwa Ulaya yote kwamba hii ni kampeni ya kushinda" haswa kabla ya msimu wa baridi ambao kuna uwezekano wa kuona shinikizo kwenye usambazaji wa gesi.
"Tuko kwenye wakati mgumu," alisema. Sababu zaidi ya kudumisha uungwaji mkono kusaidia Waukraine kushinda au "angalau kujadiliana kuhusu nafasi yenye nguvu kubwa", alisema, ni kwa sababu kiongozi wa China Xi Jinping "alikuwa akitazama kama mwewe (kwa umakini)".
"Hakuna ushahidi kwamba [Rais Vladimir] Putin anasumbuliwa na tatizo la kiafya," alijibu alipoulizwa, akirejea maoni ya Mkurugenzi wa CIA William Burns katika Jukwaa hilo jana.
Takriban maafisa 400 wa ujasusi wa Urusi wanaofanya kazi kwa siri wamefukuzwa kote Ulaya, alisema, na kupunguza nusu ya uwezo wa Urusi wa kufanya ujasusi katika bara hilo.
"Mlango wetu uko wazi kila wakati," alisema linapokuja suala la kuajiri maafisa wa Urusi waliojitenga ili kupeleleza kwa ajili ya Uingereza.
NB: Katika kujifariji sisi warusi wa malinyi tucomment "Propaganda" sawa tumeelewana ee.