Urusi imezikatia gesi nchi za Poland na Bulgaria. Putin alivyosema walipe kwa ruble hakuwa anatania

Subili utayaona majibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkataba hauainishi namna ya kufanya malipo zaidi ya kusema Euro/dola zitatumika. Muuzaji ndiye mwenye mandate ya kuelekeza mode of payment. Kwa sasa urusi imeelekeza mnunuzi lazima afungue akaunti Gazprombank ambako ataweka hizo dola au Euro zake kama mkataba unavyosema alipe kwa Euro/dola. Baada ya hapo asubiri gesi! Kinachoendelea na dola zake alizoweka hakimhusu! Gazprombank huzitumia hizo dola kununulia ruble kisha kuzituma hizo ruble kwa gazprom ambayo ndiyo huuza gesi. Rais wa EU keshasema huo utaratibu unakubalika na wanunuzi wakubwa wa gesi wa ulaya Ujerumani na Austria wameukubali. Ona hapa:

Austria will pay in rubles for Russian gas – official​

The country has accepted new payment terms and opened a ruble account, Chancellor Karl Nehammer has announced

© Getty Images / ullstein bild
Austria has accepted the new ruble gas payment mechanism, introduced by Russia earlier this month, and will abide by it, Chancellor Karl Nehammer announced on Wednesday.
We, that is, [state energy company] OMV, accepted the terms of payment, as did the German government. They [the terms] were found to be in line with the terms of the sanctions. For us, this was important,” Nehammer said at a press conference.
Wewe ukizira wenzio wala!!
 

Mwaka huu mtanyooka tu,,,
 
Baridi inakaribia kwisha bado kwa wiki 5 hivi.

Huku kwetu (Southern hemisphere)kukiwa msimu wa baridi (winter) huko Ulaya (Northern hemisphere) kunakuwa msimu wa joto (summer).

Kwahiyo, Bara Ulaya wanaingia msimu wa joto ndani ya wiki tano zijazo, wakati sisi tunaingia msimu wa baridi ndani ya kipindi hicho.
 
Sasa kama Poland hawahitaji gesi ya Urusi wanaenda mahakamani kufanya nini tena...

Jibu ni kwamba wanaihitaji gesi ya Urusi tena sana tu....
 
Uko sahihi
Ni kama mfano nina daladala halafu nalazimisha kuwa lazima abiria wa wapande daladala yangu vinginevyo siji hiyo njia!! Na pili abiria waliokataa kupanda nitawaburuza mahakamani! Kwa kupitia hasara !!!
Sasa kama Eu hawana shida ya gesi Mbona wao ndio wanalalamika?
Sijasikia Urusi ikilalamika hata
 
Mbna wamekufa watu kidogo sana hawajafika hata laki [emoji35][emoji35][emoji35][emoji34][emoji34]
 
Putin alichofanya hapa Ni kuwahi TU ili kuogopa fedheha au kuyagawa mataifa ya Ulaya (Divide and Rule)

IKO HIVI

Mkataba wa Poland kununua Gas Urusi unaisha Mwezi Octoba mwaka 2022. Poland imeweka wazi kuwa Baada ya mkataba kuisha haitanunua Gas kutoka Urusi,badala yake itaanza kufungua mabomba ya Gesi ya Kutoka Norway ambayo yalijengwa tangu mwa 2011. Mabomba hayo yalichelewa kufunguliwa kwasababu ya Gharama nafuu ya Gesi ya Urusi dhidi ya Gas ya Norway. Kwahiyo Kitakachobadilika Huko Poland Ni Gharama za Gasi TU na Wala sio kwamba Wataganda kwa kukosa Gasi Kama ninavyoona wengi wakishadidia.

Kuhusu Bulgaria. Hapa Kuna Kichekesho. Bulgaria inaitegemea Gas ya Urusi kwa 97%,Lakini Gasi hiyo inachangia 11% ya vyanzo Vya Nishati nchini Bulgaria. Kila mwaka,Bulgaria Inaagiza kiasi Cha Gasi Cha 111M m^3 kwa Mwaka. Meli kubwa na kubeba LNG inabeba kiasi Cha Gas Cha 260M m^3. Kwamaana hiyo,Bulgaria akipata Oil Tanker Moja ya LNG kutoka Marekani atatumia miaka 2 bila kuhitaji Gasi nyingine. Hapo Ni Bei TU itabadilika na Wala sio kukosekana kwa Gasi.

MAONI YANGU

Tangu tishio la Urusi kukata Gasi kuelekea Ulaya lianze,Mimi niliamua kufuatilia Umuhimu wa Gas ya Urusi barani Ulaya hasa Kiuchumi. Nimekuja Kugundua kwamba,Nchi ya Ujerumani ndio Mateka wa Urusi linapokuja kwenye suala la Gasi. Ujerumani inatumia kiasi kikubwa Cha Gasi kutoka Urusi kuendesha uchumi wake,na mbaya zaidi Hakuna mbadala wa Gasi hiyo. Kwa maana hiyo,Kama Urusi itakata Gasi yake kuelekea Ujerumani,basi hapo Uchumi wa Ujerumani utaingia RECESSION. Na Kwa kuwa Ujerumani ndio yenye Uchumi mkubwa barani Ulaya,Basi Ni wazi Ulaya nzima itayumba Kiuchumi.
 
Putin ni bogus, hakuna popote ambapo mkataba unaongelea hayo madafu yake for the terms of payment, tayari wamemwambia akaye na gesi yake kuna sources nyingi.

Kuanzia mwakani atatembeza hiyo gesi kama karanga.
 
hata Kama yalikuwa ni ya magharibi ,yaliingiaje kufanya biashara urusi!?? walikuwa na mikataba na urusi!! Na walikuwa wanalipa Kodi,hivyo wembe unakata kotekote!! Putin Safi Sana,Katia gesi hao kenge!!! na kipindi Cha kuganda ndo kimeingia,watageuka barafu kenge hao!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…