Urusi imezikatia gesi nchi za Poland na Bulgaria. Putin alivyosema walipe kwa ruble hakuwa anatania

Putin ni bogus, hakuna popote ambapo mkataba unaongelea hayo madafu yake for the terms of payment, tayari wamemwambia akaye na gesi yake kuna sources nyingi.

Kuanzia mwakani atatembeza hiyo gesi kama karanga.
Acha makasiriko boss ya kwenu mliamua kuigawa kama madalali unaisi urusi inawatu punguani kama kwenu tayri kashapata plani b gesi saivi itakuwa inaenda sana Asia nyie kipindi manaachana na gesi yake moja Kwa moja na yeye anashapata soko kubwa jipya ambalo viwanda vingi saivi vinafunguliwa Asia kuliko ulaaya China kaongeza kutumia gesi,India mafuta na gesi zinaenda snaa kwake basso Indonesia, na Vietnam nazo wataanzza Tumia iyoo gesi kwaiyo kijana wenzetu si kama Sisi
 
Mie naona jamaa anajiweka pabaya kiuhusiano wa kiuchumi.
EU wanatafuta mbadala pa kununulia aina zote za nishati sio gesi tu na mafuta mpk makaa ya mawe.
Na Russia mataifa ya EU ndio wateja wake wakubwa.
Wadhani Russia atakua ktk wakati gani!?
 
Mzee mbona umeongea kidananda sana kusema uchumi wa EU wote utaporomoka Germany akikatiwa gesi!?
Unajua maana ya uchumi wa Ulaya nzima!?
Ni sawa useme China ikiathirika kiuchumi Asia nzima itaathirika.
Ilhali mataifa mengine yanategemea nishati mbadala nyingine kuzalisha.
Mzee hapo umetoa boko kwa hiyo kauli.
Sema Germany ndio itaporomoka kiuchumi sio Ulaya yote.
 
Shida ni kwamba Russia anafanya maamuzi kwa kukurupuka akitaka kujifanya ana nguvu.
Tupo hapa Russia itakuja kuwa km Cuba kiuchumi baadae.
USA na EU waliongea jana na mama Ursula kuwa wanakaribia kupata mbadala wa kununua nishati aina zote mpk makaa ya mawe nje ya Russia na watakata kununua aina zote za nishati Russia.
Unadhani Russia kiuchumi itakua hali gani!?
Kuna pesa zinaandaliwa za ku backup sio tu uchumi wa EU Bali mpk uchumi wa Ukraine.
Kiufupi Ulaya Russia anabaki na mshirika mmoja tu Mr.Lukashenko wa Belarus .
 
Ndio maana hili ni jukwaa la international forum punguza ujuaji
 
Taarifa za hivi punde zinasema nchi za Ulaya zimeshaanza mpasuko kuhusiana na vita vya Ukraine na vikwazo hasa kutokana na gesi. Nchi kadhaa zimeanza kununua gesi kwa sarafu ya Urusi ya Rouble kinyume na misimamo yao ya awali. Kinara wa kutunisha misuli hiyo alikuwa Ujerumani wakijidai watatafuta gesi kutoka kwengine.Mashirika yanayoingiza gesi nchini humo mengi yakiwa yana ubia tu na serikali yametaka yapate ufafanuzi kutoka serikali yao na kutoka umoja wa Ulaya juu ya nini ni kukiuka vikwazo wanaponunua kwa Rouble. Katika janja janja ya Ujerumani kuendelea kupata gesi huku ikitoa kauli mbaya kwa Urusi ilitaka walipe kwa Euro halafu pesa hiyo ikiingia benki ibadilishwa na kampuni ya kuzalisha gesi ya Gazpon kuwa rouble,hata hivyo wazo hilo limepingwa na Urusi na kutaka chenji ifanyike kabla ya kuingizwa kwenye akaunti.
 
Mie naona jamaa anajiweka pabaya kiuhusiano wa kiuchumi.
EU wanatafuta mbadala pa kununulia aina zote za nishati sio gesi tu na mafuta mpk makaa ya mawe.
Na Russia mataifa ya EU ndio wateja wake wakubwa.
Wadhani Russia atakua ktk wakati gani!?
Itachukua si chini ya miaka Saba,na hiyo nishati itakua ghali Mara tano ya urusi
 
Rahisi kusema kuliko kutenda,kampuni za ujerumani bado zinashupaa na gesi ya urusi,zinaangalia namna ya kukwepa vikwazo
 
Msiwe mnatuletea comments za kile umachotamani kichwani kwako kitokee ndiyo una assume kimetokea.Nyinyi mlituaminisha hapa Germany kasalimu amri ananunua gesi kwa Ruble,huyo huyo Germany aliyesalimu amri ndiyo kwanza ameidhinisha kupeleka silaha nzito zaidi Ukraine

Sasa inaingia akilini mtu aliyesalimu amri hapo hapo anakuwa na guts za kupeleka silaha.Na kwanini Russia hajakata gesi kwenda Germany pamoja na kukaidi kote kwa masharti aliyomwekea?
 
Gesi hawajakatiwa kwa sababu kuna makampuni ya Ujerumani yananunua kwa rouble tayari.Wameshindwa kuacha kununua.Na kuhusu kupeleka silaha nzito si dalili ya kuwa mbabe bali hicho ni kiburi zaidi.Hujawahi kuona anapigana na huku analia kwa vile hataki aonekane kashindwa.
 
Itachukua si chini ya miaka Saba,na hiyo nishati itakua ghali Mara tano ya urusi
Embu fikiria kabla ya kuongea.
Ametaftiwa mbadala China sembuse Russia!?
Hata ikichukua miaka 20 hayo mataifa tunayoyazungumzia ndio yanashikilia uchumi wa dunia labda umesahau hilo.
Je Russia akishahamwa atakua na hali gani!?
Ogopa kutishia wenye fedha.
 
Rahisi kusema kuliko kutenda,kampuni za ujerumani bado zinashupaa na gesi ya urusi,zinaangalia namna ya kukwepa vikwazo
Embu fikiria unazungumzia mataifa yepi mzee.
Unazungumzia mataifa yaliyoimarika kiuchumi na kifedha.
Kaa fanya tathmini nani mpk sasa ameumia na kaanguka kiuchumi Kati ya mataifa ya EU na Russia.
NASUBIRI JIBU.
 
Wakipata mbadala ndio uje uchangie
Halafu URUSI kakurupuka alikwambia nani!!?
Upe muda nafasi huku ukiomba UHAI na UZIMA ndio utaelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Embu fikiria unazungumzia mataifa yepi mzee.
Unazungumzia mataifa yaliyoimarika kiuchumi na kifedha.
Kaa fanya tathmini nani mpk sasa ameumia na kaanguka kiuchumi Kati ya mataifa ya EU na Russia.
NASUBIRI JIBU.
Weee fanya tathmini MKUU ukipata majibu uje nayo
Lakwanza angalia uimara wa hizo fedha zao kuanzia mgogoro unaanza mpaka leo hii
Pili angalia mfumko wa bei kwenye hayo mataifa kabla na baada ya huu mgogoro ikiwemo leo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Embu fikiria unazungumzia mataifa yepi mzee.
Unazungumzia mataifa yaliyoimarika kiuchumi na kifedha.
Kaa fanya tathmini nani mpk sasa ameumia na kaanguka kiuchumi Kati ya mataifa ya EU na Russia.
NASUBIRI JIBU.
Raia wa hayo mataifa wakikusikia watakupiga mawe,recession inaingia marekani,mfumuko wa Bei ulaya kote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…