Urusi: Twitter yapigwa faini kwa kuweka maudhui yasiyoendana na Maadili ya Nchi hiyo

Urusi: Twitter yapigwa faini kwa kuweka maudhui yasiyoendana na Maadili ya Nchi hiyo

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mahakama ya mji mkuu wa Moscow nchini Urusi, imeitoza Twitter faini ya fedha ruble milioni 3.2 kwa ukiukaji wa kiutawala.

Kesi iliyowasilishwa na Idara ya Teknolojia ya Habari ya Serikali ya Urusi na Mamlaka ya Usimamizi wa Mawasiliano ya Umma (Roskomnadzor) dhidi ya Twitter ilisikilizwa katika Mahakama ya Taganskiy mjini Moscow.

Mahakama iliamua kuwa kampuni ya Twitter haikutii sheria kwa sababu ya kupatikana kwa machapisho yaliyopigwa marufuku nchini Urusi kwenye jukwaa hilo la mtandao wa kijamii, na kusababishwa kutozwa faini ya fedha ruble milioni 3.2 (takriban dola elfu 42).

Pamoja na uamuzi huo, idara ya Roskomnadzor ilipunguza kasi ya Twitter kwa asilimia 50 kwenye vifaa vya rununu kwa madai kuwa maudhui ya kujitoa uhai, yenye uchafu na utangazaji wa dawa za kulevya hayakuondolewa kwenye mtandao huo wa kijamii.


TRT
 
I like this.

They must abide and comply to the laws of the country they operate.

But NOT think that countries should obey the Twitter rules.
 
Enh urusi si walisema watajitegemea kwa kila kitu.. internet hadi social media???
 
Twitter wanapaswa kuwa makini mno kwa sababu mtandao wao wapo tayari kuzuia maneno ya Trump na kuona ni hatari zaidi kuliko picha za ngono,madawa ya kulevya, ushoga n.k.

Hauwezi amini kwamba Maneno ya Trump Twitter waliona ni hatari zaidi ya haya mauchafu yao
 
Yaani urusi yote hiyo inapigwa faini 42,000 tu au kuna mtu anaitwa urusi
 
Yaani urusi yote hiyo inapigwa faini 42,000 tu au kuna mtu anaitwa urusi
 
Mahakama ya mji mkuu wa Moscow nchini Urusi, imeitoza Twitter faini ya fedha ruble milioni 3.2 kwa ukiukaji wa kiutawala.

Kesi iliyowasilishwa na Idara ya Teknolojia ya Habari ya Serikali ya Urusi na Mamlaka ya Usimamizi wa Mawasiliano ya Umma (Roskomnadzor) dhidi ya Twitter ilisikilizwa katika Mahakama ya Taganskiy mjini Moscow.

Mahakama iliamua kuwa kampuni ya Twitter haikutii sheria kwa sababu ya kupatikana kwa machapisho yaliyopigwa marufuku nchini Urusi kwenye jukwaa hilo la mtandao wa kijamii, na kusababishwa kutozwa faini ya fedha ruble milioni 3.2 (takriban dola elfu 42).

Pamoja na uamuzi huo, idara ya Roskomnadzor ilipunguza kasi ya Twitter kwa asilimia 50 kwenye vifaa vya rununu kwa madai kuwa maudhui ya kujitoa uhai, yenye uchafu na utangazaji wa dawa za kulevya hayakuondolewa kwenye mtandao huo wa kijamii.


TRT
Safi sana wameshtakiwa huko huku wakahukumiwa huko huko amna mambo ya MIGA huko au ICSd
 
Urusi lazima wawabane Twitter watu wanajiachia huko wapinzani wa putini mitandao mingine ikibanwa huko wanatumia kuwasiliana kama kawaida...Putin anatanani malaika washuke wafunge mitandao...
 
Back
Top Bottom