Urusi yatangaza kuharibiwa kwa makombora ya Marekani nchini Ukraine

Urusi yatangaza kuharibiwa kwa makombora ya Marekani nchini Ukraine

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2018
Posts
21,711
Reaction score
35,644
Wizara ya Ulinzi ya Urusi siku ya Jumatano imetangaza uharibifu uliofanywa na wanajeshi wa Urusi wa makombora mawili ya HIMARS MLRS ya Marekani huko Donbass.

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi Luteni-Jenerali Igor Konashenkov alisema makombora hayo yaliyotengenezwa na Marekani ya HIMARS na maghala mawili ya risasi yaliharibiwa na ‘’makombora yenye usahihi wa hali ya juu’’ ya Urusi karibu na kijiji cha Malotaranovka katika Jamhuri ya Watu wa Donetsk kama ilivyojiita.

Hata hivyo, mshauri wa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ukraine, Anton Gerashchenko, anakataa taarifa za jeshi la Urusi kuhusu madai ya uharibifu wa makombora ya HIMARS yaliyopelekwa Ukraine kutoka Marekani.

Data ya jeshi la Urusi pia imekataliwa na mbunge wa Ukraine, ambaye pia ni mwanachama wa kundi la Umoja wa Ulaya Oleksiy Goncharenko.
 

Attachments

  • Screenshot_20220706-162115_Facebook.jpg
    Screenshot_20220706-162115_Facebook.jpg
    181.9 KB · Views: 14
Nani anaweza kuchukulia seriously kauli za viongozi wa jeshi la Ukraine pamoja na Zelensky - wote wasanii.

Hapa wanaona aibu kukubali kwamba jeshi la Russia limefanikiwa kuharibu/kuteketeza makombora ya Kimerikani - wasi wasi wa Viongozi wa Ukraine ni kwamba wakikubali wataonekana wazembe na hiyo. itawafanya Wamerikani na Nchi za Ulaya kupunguza au sitisha msaada wa silaha zinazo pelekwa huko Ukraine.
 
... Ukraine wakanushe kwa kuleta picha ya kombora lisiloharibiwa au? Jukumu la kuthibitisha ni la mleta madai.
Kwani propaganda ngapi za mainstream media za west zimetangaza wakati vita inaanza ila cha kushangaza kila leo Russia anasonga mbele kimyakimya, hadi kelele zimewaisha wanaokoteza vijitaarifa halafu Putin anasonga kimyakimya kana anakimbiza mwizi
 
Wapigane, Ila wasisahau uku Ndio kipindi cha bajeti kwa nchi yetu ya Tanzania. Kwa iyo wajue kibajeti tunawategemea kwa iyo wabakishe pesa za kutupa misaada.
Acha wapigane maana ndio wanyonyaji wetu halafu wanaturudishia bakishishi tu
 
Iran and Russia have reached an agreement on working to expand their financial and banking cooperation and remove the obstacles in the way of their ties under tough American sanctions.
 
Back
Top Bottom