FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,500
- 8,060
Habari!
Hali si hali kwa rais Donald Trump, wapenzi na wafuasi wa Chama cha Republican kwa ujumla wakati ambapo tukielekea katika Uchaguzi wa Rais panapo mwezi Novemba mwaka huu.
Hii ni kulingana na matokeo ya hivi karibuni ya kura mpya za maoni za kitaifa za jarida la New York Times pamoja na Taasisi ya Utafiti ya Chuo cha Siena ambapo mgombea mteule wa Chama cha Democratic Joe Biden anaongoza kwa alama 14 dhidi ya mpinzani wake Donald Trump.
Trump amejipatia asilimia 36 ya kura huku Biden akiongoza kwa asilimia 50 ya kura za washiriki wote.
Biden amejipatia faida ya uungwaji mkono kutoka katika makundi ya wanawake na jamii za watu wasio weupe huku kukiwa na uwiano sawa wa kura kutoka kwa wapiga kura wa kiume, Wamarekani weupe pamoja na wapiga kura wenye umri wa kati na kuendelea.
Huu ni mwanzo tu kuelekea Uchaguzi wa Novemba na pengine ni kidogo tu ya kile kilichopo mbele. Muda utaweka bayana kile kilichobaki!
Hali si hali kwa rais Donald Trump, wapenzi na wafuasi wa Chama cha Republican kwa ujumla wakati ambapo tukielekea katika Uchaguzi wa Rais panapo mwezi Novemba mwaka huu.
Hii ni kulingana na matokeo ya hivi karibuni ya kura mpya za maoni za kitaifa za jarida la New York Times pamoja na Taasisi ya Utafiti ya Chuo cha Siena ambapo mgombea mteule wa Chama cha Democratic Joe Biden anaongoza kwa alama 14 dhidi ya mpinzani wake Donald Trump.
Trump amejipatia asilimia 36 ya kura huku Biden akiongoza kwa asilimia 50 ya kura za washiriki wote.
Biden amejipatia faida ya uungwaji mkono kutoka katika makundi ya wanawake na jamii za watu wasio weupe huku kukiwa na uwiano sawa wa kura kutoka kwa wapiga kura wa kiume, Wamarekani weupe pamoja na wapiga kura wenye umri wa kati na kuendelea.
Huu ni mwanzo tu kuelekea Uchaguzi wa Novemba na pengine ni kidogo tu ya kile kilichopo mbele. Muda utaweka bayana kile kilichobaki!