ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa kuwa amesema kubwa la wakubwa huenda this time around Wakapata amani ya kudumu.
----
Marekani imehimiza Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Jumanne kuzingatia kuchukua hatua za kukomesha vikosi vya Rwanda na waasi vya M23 kuingia Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo huku mzozo huo ukiendelea kuongezeka.
Kaimu Balozi wa Marekani kwa UN Dorothy Shea hakuelezea kwa Baraza la Wanachama 15 ni hatua gani inaweza kuchukuliwa.
Lakini Baraza hilo lina mamlaka ya kuweka vikwazo.
"Tunataka kusitisha na kumaliza mapigano haraka iwezekanavyo. Rwanda lazima iondoe wanajeshi wake DRC. Rwanda na DRC lazima warudi kwenye meza ya mazungumzo na kushirikiana katika kupatikana kwa suluhisho endelevu na la amani," Shea aliiambia Baraza la Usalama.
Waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda waliandamana hadi Goma, mji mkubwa zaidi mashariki mwa Kongo, siku ya Jumatatu katika hali mbaya zaidi ya mzozo uliodumu kwa muda mrefu katika zaidi ya muongo mmoja.
Kongo iliishutumu Rwanda kwa kutuma wanajeshi wake mpakani, huku Rwanda ikisema mapigano karibu na mpaka yanatishia usalama wake, bila kuzungumzia moja kwa moja iwapo wanajeshi wake wako nchini Kongo.
Katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Kongo Therese Kayikwamba Wagner alitaka vikwazo kuwekwa dhidi ya viongozi wa kijeshi na kisiasa wa Rwanda, kuwekewa vikwazo vya silaha, kupigwa marufuku kwa ununuzi wa maliasili za Rwanda na kuzuiwa kwa wanajeshi wa Rwanda kutoka kwa ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa.
Chanzo: BBC
Pia soma
- Ni wakati muafaka sasa kwa Rwanda kuwekewa vikwazo ili kumaliza vita ya mashariki ya DRC
Amesanda 👇👇
View: https://www.instagram.com/p/DFacNcURuiI/?igsh=cjl3Mjgxc2kxZGoy
Mungu awe na jeshi letu wafanikishe lengo la wao kuwa DRC na warudi salama nyumbani
Uwelewa wako ni mdogo kuhusu walinzi wa amani na kinachoendelea hapo goma Congo DRC.Zipo taarifa kwamba Wanajeshi wote wa kulinda amani kutoka kwa nchi za SADC pia wametekwa na Waasi wa M23.
Wampige chini ameshindwa kazi 👇👇Asipokuwa makini watamuondoa
Jinsi Kagame anavyojibizana na Ramaphosa naona kama anajisahau sana
Jinsi Kagame anavyojibizana na Ramaphosa naona kama anajisahau sana Sidhani kama Rwanda itaiweza South Africa. Hii ni kutoka X (Twitter) I held two conversations this week with President Ramaphosa on the situation in Eastern DRC, including earlier today. What has been said about these...www.jamiiforums.com
Kwa kuwa amesema kubwa la wakubwa huenda this time around Wakapata amani ya kudumu.
----
Marekani imehimiza Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Jumanne kuzingatia kuchukua hatua za kukomesha vikosi vya Rwanda na waasi vya M23 kuingia Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo huku mzozo huo ukiendelea kuongezeka.
Kaimu Balozi wa Marekani kwa UN Dorothy Shea hakuelezea kwa Baraza la Wanachama 15 ni hatua gani inaweza kuchukuliwa.
Lakini Baraza hilo lina mamlaka ya kuweka vikwazo.
"Tunataka kusitisha na kumaliza mapigano haraka iwezekanavyo. Rwanda lazima iondoe wanajeshi wake DRC. Rwanda na DRC lazima warudi kwenye meza ya mazungumzo na kushirikiana katika kupatikana kwa suluhisho endelevu na la amani," Shea aliiambia Baraza la Usalama.
Waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda waliandamana hadi Goma, mji mkubwa zaidi mashariki mwa Kongo, siku ya Jumatatu katika hali mbaya zaidi ya mzozo uliodumu kwa muda mrefu katika zaidi ya muongo mmoja.
Kongo iliishutumu Rwanda kwa kutuma wanajeshi wake mpakani, huku Rwanda ikisema mapigano karibu na mpaka yanatishia usalama wake, bila kuzungumzia moja kwa moja iwapo wanajeshi wake wako nchini Kongo.
Katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Kongo Therese Kayikwamba Wagner alitaka vikwazo kuwekwa dhidi ya viongozi wa kijeshi na kisiasa wa Rwanda, kuwekewa vikwazo vya silaha, kupigwa marufuku kwa ununuzi wa maliasili za Rwanda na kuzuiwa kwa wanajeshi wa Rwanda kutoka kwa ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa.
Chanzo: BBC
Pia soma
- Ni wakati muafaka sasa kwa Rwanda kuwekewa vikwazo ili kumaliza vita ya mashariki ya DRC
Amesanda 👇👇
View: https://www.instagram.com/p/DFacNcURuiI/?igsh=cjl3Mjgxc2kxZGoy
Unajidanganya.Vikwazo vya US havimtishi yoyote yule.
Tanzania katika kumuadabisha Kagame ni afadhali kuliko USA
Unajidanganya.
Watu hawalali usingizi kutokana na Vitisho kutoka kwa Trump wa huko US.