Usafi na mpangilio wa vitu vya ndani ni changamoto kwa watu wengi

Usafi na mpangilio wa vitu vya ndani ni changamoto kwa watu wengi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1615236360921.jpeg

Usafi na mpangilio mzuri wa vitu vya ndani huenda pamoja. Huwezi kuwa msafi lakini ushindwe kupanga vitu vyako vizuri. Wana saikologia husema mpangilio mzuri wa vitu husaidia akili kutulia.

Kuna wanaofikiria usafi huendana na uwezo wa kiuchumi. Hapana kuna watu wanaishi maisha duni lakini akikupa maji ya kunywa kwenye kikombe cha bati kina ng’aa unaweza ujione. Ingawa maziringira huchangia, si rahisi kuishi kwenye chumba kimoja unapikia kuni na moshi unatanda na kuta za nyumba ziwe safi.

Kuna watu mpangilio wa nyumba unamshinda anasingizia watoto. Watoto ukianza kuwafundisha mapema mnaweza kusafisha na kupanga nyumba pamoja. Michezo yao unawaonyesha sehemu ya kuhifadhi.

Wanaume wengine hushindwa kukaa katika mazingira yasiyo na mpangilio. Mtu ametoka kazini na stress za boss, akifika nyumbani anakuta mambo vurumai. Huyu akipata mchepuko unaojua usafi na mpangilio wa vitu andika maumivu.
 
Sijui inawezekana vipi hata, jamaa zangu muda wote ni kuchana karatasi sebleni, kurusha mito ya kochi, sarakasi sasa yani nyumba inakua kama karakana.... ndio maana na akili haitulii kumbe!
 
Mi kwangu ni Kuchafu mazee soksi zimeanzia Sebleni nikirudi nguo huwa nazivua naziweka kitandani vurugu match ngoja nitafute jiko
 
Back
Top Bottom