Usafi wa kila Jumamosi ulichangia vipi kushuka kwa mapato Dar?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Nani ana takwimu za kiasi gani cha mapato kilipotea kwa maduka na biashara kufunguliwa saa 4 asubuhi kila Jumamosi Dar es Salaam kwa miaka 2?

Nini adhali za kiuchumi kwa wafanyabiashara wakubwa Dar kuchanganyishwa kwenye utekelezaji na ufanikishaji wa shughuli za kimaendeleo Dar?
 
Kilikuwa ni kipindi cha mgomo uliosimamiwa na serikali.

Biashara nyingi zinafunguliwa kuanzia saa 12 asubuhi. Siku za jumamosi mgomo ulikuwa ni wa masaa 4 ambapo kwa mwezi yalipotea masaa 16 ya kazi.

Hasara ilikuwa ni kubwa kwa wafanyabiashara na wateja wao.
 
Tamko lilitolewa kumfurahisha mtukufu ambae sasa anauliza mapato
 
Ila ukiangalia ni kweli,hata ishu ya baadhi ya biashara kutokuruhusiwa kukesha
 
Kufungua bar saa kumi na kufunga saa tano kamili usiku pia Yana punguza mapato!
Maana hapo hapo unataka mmiliki wa bar alipie leseni ya vinywaji,leseni ya afya,leseni ya biashara,bado hajalipa mishahara,umeme,maji etc
Kuna biashara hapo

Ova
 
Tatizo letu hao jamaa wanajua kudai tu hawangali upande wa pili ukoje

Ova
 
Kufungua bar saa kumi na kufunga saa tano kamili usiku pia Yana punguza mapato!
Maana hapo hapo unataka mmiliki wa bar alipie leseni ya vinywaji,leseni ya afya,leseni ya biashara,bado hajalipa mishahara,umeme,maji etc
Kuna biashara hapo

Ova
Ukizuia watu kunywa ni sawa na kuwaambia brewery walipe kodi kidogo.
 
Nilitafakari kwa makini ule mda wa kufunga biashara kila jumamosi mpaka saa nne nikakosa jibu, kufanya usafi ukiwa kwenye biashara yako kuna kosa gani?masaa manne kupotea ni pesa nyingi. Mama ntilie wengi walifunga biashara zao jumamosi kwani mpaka saa nne umeshapoteza wateja.
 
Ndio maana nchi zingine kazi ni 24/7
Halafu nimeipenda hii kampuni ya japan
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…