Usafiri wa kutumia ungo upo wa aina nyingi

Usafiri wa kutumia ungo upo wa aina nyingi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
10151259_1558174831086389_6504662339237088119_n.jpg
attachment.php
10689715_1558174864419719_2703376850819588356_n.jpg
10672214_1558174887753050_1745182959163419979_n.jpg


Usafiri wa ungo upo wa aina nyingi, upo usafiri wa ungo unaotumia wanyama, upo usafiri wa kutumia fagio, upo usafiri wa kutumia fimbo, upo usafiri wa kutumia ungo. Wachawi wote wana roho ya uchawi, roho ya uchawi ni roho inayokufanya uweze kupita eneo ngumu na kutokeza upande wa pili, kwa mfano

wachawi wanapowanga usiku roho hizi huwafanya kuingia katika nyumba yoyote na kuwafanyia uchawi usiku watu waliolala ndani ya nyumba hizo bila ya kuonekana. Isipokuwa nyumba za walokole haziingiliki kabisa. Roho za uchawi zinawawezesha wachawi kujibadilisha maumbo yao, kutoka maumbo ya kibinadamu na kugeuka kuwa paka, panya, kunguru n.k.

1. Usafiri wa UNGO
Picha ya wachawi walio dondoka huko mkoani Mwanza. Ungo uliokuwa ukitumiwa na wachawi hawa, ulizidiwa nguvu baada ya wachawi kupita katika anga ambalo chini yake kulikuwa kanisa la kiroho. Wachawi hawa walitumwa kutoka mkoani Kigoma, kwenda mkoani Mwanza kuchukua roho za watu wawili. Wachawi hawa walikuwa wamepewa maagizo na mkuu wa wachawi katika madhabau yao ya kichawi.

Askari polisi na watu mbalimbali wakiwashangaa wachawi hawa walio anguka na ungo wao wa kichawi katika eneo la Butimba jijini Mwanza. Wanapotaka kusafiri anakuwa na vifaa vyake vya kichawi, kisha huomba dua akinuizia majini yampeleke sehemu fulani, roho yake ya uchawi na majini humuinua juu angani kwa kasi hadi eneo alilokusudia. Usafiri wa aina hii ni hatari kwani unaweza kutunguliwa kirahizi ukiwa angani.

2. USAFIRI WA KUTUMIA WANYAMA KAMA FISI.
Usafiri wa kutumia wanyama kama fisi, hutumika kwa nchi kavu tu, hawawezi kuvuka bahari kwenda visiwani au nchi za mbali. Fisi ni mnyama anayetumiwa sana na wachawi wa nchi katika usafiri. Usafiri huu hutumika katika maeneo ya nchi kavu tu, hauvuki bahari.

Uchawi wa kusafiri na fisi, unatumiwa sana na wachawi waliopo katika mikoa ya kanda ya ziwa , Mwanza, Shinyanga na Tabora, pamoja na mikoa ya Kigoma, Dodoma, na Singida. Katika makala inayo fuata nitawafahamisha kwanini wachawi wa maeneo tajwa hapo juu hupenda kutumia usafiri wa fisi.

3. USAFIRI WA KUTUMIA FIMBO
Usafiri wa kasi sana ni wa kutumia fimbo, kabla ya kuanza safari, unaomba dua ya manuizo na kukanyanga incha moja ya fimbo, roho ya uchawi na majini hukuinua juu angani, kama unataka kwenda Nigeria kutoka Dar, utaonyeshwa njia yote ilivyo, kama kuna hatari yoyote huonekana, na inabidi uhairishe safari,

kama njia ni nyeupe, unatakiwa ukanyage incha ya pili ya fimbo, na safari huanza kwa kasi ya sauti. Kwa sababu safari ni ya kasi sana na upepo ni mkali sana, kiasi kuwa huwezi kufika ukiwa hai, majini huchomoa roho yako ndani ya mwili wako na roho kukutangulia mbele, mwili wako huikimbiza roho yako ukiwa katika hali ya

umauti, unaweza kutumia sekunde 10 kufika Nigeria, lakini ni usafiri wa hatari kuliko zingine, usafiri huu hujulikana kama usafiri wa kujichinja. Mfano wa picha ya mchawi wa kizungu akisafiri kwa kutumia fimbo.

3. UCHAWI WA KUSAFIRI KWA UFAGIO.
Uchawi huu hutumiwa sana na wachawi waliopo katika nchi ya Romania na Ulaya na Marekani yote kwa ujumla. Barani Afrika, uchawi huu hutumiwa zaidi na wachawi waliopo katika nchi ya Swaziland. Picha ya mfano wa mchawi wa kizungu akisafiri kichawi kwa kutumia ufagio. Usafiri huu ni maarufu sana miongoni mwa wachawi waliopo Ulaya na Marekani na katika nchi ya Swaziland.

Uchawi huu ulianza kutumika katika nchi ya Romania iliyopo Ulaya Mashariki miongo mingi iliyopita. Katika makala yajayo nitaeleza kuhusu usafiri wa fisi. Bunge La Mtandao Usafiri wa ungo upo wa aina nyingi, upo usafiri wa ungo unaotumia wanyama, upo usafiri wa kutumia fagio, upo usafiri wa kutumia fimbo, upo usafiri wa kutumia ungo.

Wachawi wote wana roho ya uchawi, roho ya uchawi ni roho inayokufanya uweze kupita eneo ngumu na kutokeza upande wa pili, kwa mfano wachawi wanapowanga usiku roho hizi huwafanya kuingia katika nyumba yoyote na kuwafanyia uchawi usiku watu waliolala ndani ya nyumba hizo bila ya kuonekana. Isipokuwa

nyumba za walokole haziingiliki kabisa. Roho za uchawi zinawawezesha wachawi kujibadilisha maumbo yao, kutoka maumbo ya kibinadamu na kugeuka kuwa paka, panya, kunguru n.k.

Chanzo: MziziMkavu
 

Attachments

  • wachawi.jpg
    wachawi.jpg
    57.7 KB · Views: 2,958
hua nataman sana japo kwa nia njema kujua namna roho za kichawi na wachawi wanavo fanikisha mambo yao, sasa naanza elewa
 
Mtu na akili zako unafanya ndumba nangae? Huu ni msiba
 
Hivi ikitokea nimeibiwa nauli afu akaja MTU na mfagio akanisafilisha kwa huo mfagio na kwa kichawi hadi nakokwenda kuna ubaya wowote
 
Kazi ya uchawi na uganga wa kienyeji ni mateso ya kujitakia tu;na mwisho wa maisha ni Jehanum ya moto pamoja na shetani.
 
Usafiri wa fimbo unaweza kutufaa ktk uchunguzi wa anga za mbali
 
MziziMkavu nataka fumba na kufumbua niwe amerika.msaada wako mkuu.lol
Tafuta pesa upatiwe Jini likurushe kutoka Bongo mpaka Amerika kadoda11

969917_637254506302937_93078210_n.jpg



993018_636796873015367_763374715_n.jpg


528310_592137330814655_501558711_n.jpg


Kwenye hizo Picha chaguwa Jini mmoja amabayr atakayre kufaa ili akurushe angani.
 

Attachments

  • ghost_of_sparta__kratos__by_huzzain-d6jkl80.jpg
    ghost_of_sparta__kratos__by_huzzain-d6jkl80.jpg
    107.8 KB · Views: 441
Last edited by a moderator:
Niliwahi kusikia kuna wachawi wanatumia Qur'an kusafiri, je hii imekaaje? Wao wanafanyaje?
 
Hivi ni kwa nini wanaotumia ungo na kuruka angan wasiwe wawazi yaan tuwaone live wanavyopaa kama ndege za kawaida tunavyoziona?
 
536628_390412344345009_779945728_n.jpg



JINI CLAUNECK;
Jini huyu ana Nguvu na Mamlaka juu ya Vitu na Utajiri,
Anaweza Kuvumbua Hazina iliyofichwa, kwa yeyote atakayeweka Mkataba nae,
Ana uwezo wa Kumzawadia Mtu Utajiri mkubwa kwani yeye anapendwa sana na Lucifer,
Ana uwezo wa kukuletea Pesa kutoka mbali,
Mtii naye atakutii!

Je unahitaji kuzungumza nae
 
536628_390412344345009_779945728_n.jpg



JINI CLAUNECK;
Jini huyu ana Nguvu na Mamlaka juu ya Vitu na Utajiri,
Anaweza Kuvumbua Hazina iliyofichwa, kwa yeyote atakayeweka Mkataba nae,
Ana uwezo wa Kumzawadia Mtu Utajiri mkubwa kwani yeye anapendwa sana na Lucifer,
Ana uwezo wa kukuletea Pesa kutoka mbali,
Mtii naye atakutii!

Je unahitaji kuzungumza nae

hebu ngoja kwanza.........wakati tunazungumza tunaangaliana uso kwa macho......?.........ooooh puliiz......
 
Back
Top Bottom