Usafiri wa meli kutoka Tanzania hadi Brazil

Wapendwa eee hivi Kuna meli inayotoka bandari ya dar es salaam hadi Brazil?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna meli ya abiria inayotoka hapa Tanzania mpaka Brazil.

Kama unataka uende Brazil kwa meli itakubidi uzamie kwenye meli ambayo ilikuja kuleta mzigo wa sukari.

Kufika Huko utatumia muda mrefu sana maana aina ya meli unazozamia hazina ratiba maalumu na zinakaa sana na kupita bandari mbalimbali kubeba mzigo.
 
Write your reply...daah nakumbuka shughuli zangu za uzamiaji sitakaa nisahau nilivyoachwa kisiwa cha Solomon island.

Mkuu kumbe umewahi zamia meli.
Saizi raha sana ukizamiha ukakamatwa na mmetoka nje ya nchi yako. Wafanyakazi was meli hawarusiwi kukusumbua utahudumiwa vizuri mpaka utaposhushwa bandari inayofatwa na kupelekwa ubaloz wa nchi yako.

Na huo ndio muongozo wa international Ship and Port Facility Security Code (ISPS CODE) kwenye kipengele cha stow away.

Kuna kifungu cha kuhusu utu ukikamatwa wakati wa kurudishwa nchini mwako unapewa pesa kiasi kama dola 1000 ya kujikimu ukirudi mtaani.
 
Kama unataka uzamie nikupe escape plan kuanzia bandarini mpaka kuingia kwenye meli.

Hii unaingia bandari yoyote hata iwe na security level one na meli nakusomea ramani yake yote na sehemu salama za kukaa ambazo ni ngumu kufanyiwa inspection kabla ya meli kuondoka bandarini.
 
Ngoja nistoroway aseeh

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama unazamia meli hapa Bongo ili uende ulaya inabidi utulize kichwa. Na meli pekee ni za kontena tena utafute taarifa ya meli iyo na ratiba yake.

Meli nyingine za kontena hazifiki ulaya ni zile meli ambazo zimebeba mzigo kutoka kwenye meli kubwa ambazo haziwezi kuingia bandari zetu(Feeder Vessels) ukizamia hii utajikuta upo Arabuni, Singapore, Thailand au China.
 
Natamani umwage mboga hapa mkuu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ehee endeleen Basi
Haya Mambo bado yapo!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Uzamiaji bado upo sana. Uzamiaji ni moja ya matishio makubwa katika biashara ya meli na bandari.

Mwaka 2004 ilianzishwa code inaitwa ISPS Code ili kuzuia na kuweka usalama kwa bandari na meli dhidi ya uharamia.

Kwa Bongo baada ya ISPS Code kuanza kufanya kazi kwenye bandari yetu uzamiaji umepungua. Hii kwa sababu mzamiaji hawezi kutoboa kuondoka na meli kwa sababu kabla meli haijatoka kuna inspection na bandari in a operate kwa Isps security level 1 ambapo mtu ambaye haijui hii code ni ngumu kupenya.
 
Natamani umwage mboga hapa mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ukizamia meli kwanza jihamini na hakuna mtu yeyote atayekudhuru ukiwa melini wala kukufanyia kitendo kiovu. Endapo hatathubutu kwa sheria za sasa adhabu itakuwa ni kwa nahodha, mhusika mpaka mmiliki wa hiyo kampuni.

Ndio maana ukizamia meli kubwa ukakutwa nahodha atakulinda kama mboni mpaka ukabidhiwe kwenye bandari au balozi ya nchi yako.

Angalizo hizi sheria ni kwa meli za biashara(Mercant ships) meli za kijeshi hazipo chini ya sheria hizi za IMO.
Sije ukazamia meli ya kijeshi kama ile ya India au China, huko utakuwa umeenda choo cha kike.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…