Usafiri wa meli kutoka Tanzania hadi Brazil

Usafiri wa meli kutoka Tanzania hadi Brazil

Thanks kiongozi

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama upo serious kwenda Brazili meli za kuzamia ni meli ambazo huleta sukari, mahindi au ngano.

Hizi ni meli za kubeba shehena(Bulk carrier) na hazina ratiba maalumu. Inabidi uwe unatembelea ratiba ya meli zinazoingia bandarini kwa njia ya mtandao hapo utaziona za mwezi mzima.

Ukikuta meli ni Bulk Carrier moja kwa moja utaona na sehemu ya gati itapopangiwa kushusha mzigo muda itaotumia kushusha.

Baada ya hapo utaitafuta iyo meli kwenye application inaitwa Vessel finder hapa utapata kuijua vizuri wapi iliposajiliwa ,uwezo wake na ipo au inaelekea wapi.

Unatakiwa kujua inaenda wapi sije ikawa bado inatakiwa iende Mombasa, kama next port of call ni za Msumbiji au South hapo umeula bingo hiyo inafaa. Na ujue muda itaofika hizo bandari Estimated Time of Arrival (ETA).

Kuna vitu kama usajili wa meli ukikuta imesajiliwa Panama, Liberia au Hong Kong hizo hazina shida tena ukikuta wafanyakazi ni wafilipino hao njaa kali uhakika wa kutoboa mkubwa.
 
Chamoto,

Huyo aliyefanikiwa alipambana haswa kuzamia zamani walitumia njia ngumu ukisimuliwa kama una roho ndogo uwezi kukubali uzamie.

Meli zilikuwa zinatumia muda mwingi safarini na mzamiaji anajificha kwenye chumba cha mizigo mtu anakula biskuti na maji. Sehemu za hewa safi zilikuwa finyu kwao.[/QUOTE]
 
Huyo aliyefanikiwa alipambana haswa kuzamia zamani walitumia njia ngumu ukisimuliwa kama una roho ndogo uwezi kukubali uzamie.

Meli zilikuwa zinatumia muda mwingi safarini na mzamiaji anajificha kwenye chumba cha mizigo mtu anakula biskuti na maji. Sehemu za hewa safi zilikuwa finyu kwao.
kweli, tulikuwa tunasimulia habari za kufungiwa kwenye pipa na kutupwa baharini, hasa meli za wagiriki.
 
Napenda sana maisha ya kuzamia kwani nahisi nilizaliwa niwe mzamiaji

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna vijana wa kizanzibar wao mazoezi ya kuzamia meli wanachukua kwenye Sea Link 1 na 2. Wanasafiri Dar-Zanzibar bure ila wakikamatwa kwa kuzamia meli inakuwa imetoka hapo wanajitetea na kusamehewa.

Pia nina jamaa yangu kwenda Zanzibar yeye anategea meli za kuondoka jioni lazima azamie, na anaijua kila kona.
 
Mkuu kumbe umewahi zamia meli.
Saizi raha sana ukizamiha ukakamatwa na mmetoka nje ya nchi yako. Wafanyakazi was meli hawarusiwi kukusumbua utahudumiwa vizuri mpaka utaposhushwa bandari inayofatwa na kupelekwa ubaloz wa nchi yako.

Na huo ndio muongozo wa international Ship and Port Facility Security Code (ISPS CODE) kwenye kipengele cha stow away.

Kuna kifungu cha kuhusu utu ukikamatwa wakati wa kurudishwa nchini mwako unapewa pesa kiasi kama dola 1000 ya kujikimu ukirudi mtaani.
Mtaji huo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom