USAHIHI: Aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali amepangiwa Majukumu mengine na siyo kutumbuliwa. Anaweza kuwa na Majukumu makubwa kuliko ya Awali

USAHIHI: Aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali amepangiwa Majukumu mengine na siyo kutumbuliwa. Anaweza kuwa na Majukumu makubwa kuliko ya Awali

..maana yake yuko benchi.
Hivi unaelewa kiswahili kweli wewe? Benchi ni mtu ambaye hana majukumu ya kufanya.sasa ni wapi umeambiwa kuwa Matinyi ameachwa bila majukumu ya kufanya? Huoni katika taarifa kuwa kupangiwa MAJUKUMU MENGINE? Kweli CHADEMA akili zenu mnazijuwa wenyewe tu.
 
Ndugu zangu watanzania,

Nimeona ni kama kiswahili kimekuwa kigumu kidogo kwetu watanzania japo ndio lugha yetu ya Taifa au huwa tunasoma taarifa kwa juu juu tu,kama kawaida yetu ya baadhi yetu watanzania ya uvivu wa kusoma habari au taarifa kwa umakini na utulivu.

Nimepita baadhi ya maeneo na kwenye kurasa mbalimbali za Mitandao za baadhi ya watu,nimeshangaa wakitumia maneno kuwa aliyekuwa msemaji mkuu wa serikali ametumbuliwa,jambo ambalo siyo kweli .

Ukweli na usahihi ni kuwa taarifa ya ikulu inasema kuwa AMEPANGIWA MAJUKUMU MENGINE,ambapo majukumu hayo bila shaka yatatangazwa muda wowote ule kwa umma, ili umma ujuwe mtumishi wao ni nani katika nafasi fulani.

Na unaweza kuta majukumu hayo mengine mapya yanaweza kuwa makubwa sana kuliko majukumu aliyokuwa nayo Awali. Kwa hiyo tuendelee kuwa na subira na utulivu kusubiri majukumu hayo mapya.

Japo ningependa pia kuwaambia ya kuwa siyo kila nafasi ya uteuzi huwa inatangazwa.yaani namaanisha zipo nafasi nyeti ambazo Rais anaweza mteua mtu au kumpangia mtu Majukumu na isitangazwe kwa watu,kutokana na unyeti wake. Ndio maana ukiwa kiongozi sehemu fulani unapaswa kuwa mtulivu na mwenye kudhibiti na kuchunga Ulimi wako. Siyo kuwa roporopo tu ,kwa kuwa ulimi wako unaweza kukukosesha baadhi ya nafasi kufikiriwa kupewa.hasa zinazohitaji usiri mkubwa wa taarifa na kila kitu ukionacho na kukifanya.

Kuelewa hiki nilichokizungumza basi angalia katika orodha hii ya majina hapo chini uende mpaka namba (IV )uone lugha iliyotumiwa katika taarifa ya Ikulu .View attachment 3018479View attachment 3018479

Kazi iendelee Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kuna mtu amekuuliza?
 
Kwanza sisi hatuna shida na Matinya hatuhuusu, tunacholalamika ni hizi teuzi, tengua hamisha za hovyo na gharama kubwa kwa walipa kodi
Yes ni kweli mkuu, maana mtu akipata teuzi tu hata mshahara unapanda tena wengine hata mara 4 alafu akitenguliwa mshahara huwa unabaki ule ule na kuja mwingine tena.....kuna Kuna Kuna ma-senior govt official kibao wengine wanazunguuka zunguuka tu
 
Hivi unaelewa kiswahili kweli wewe? Benchi ni mtu ambaye hana majukumu ya kufanya.sasa ni wapi umeambiwa kuwa Matinyi ameachwa bila majukumu ya kufanya? Huoni katika taarifa kuwa kupangiwa MAJUKUMU MENGINE? Kweli CHADEMA akili zenu mnazijuwa wenyewe tu.

..yuko benchi mpaka nafasi yake mpya itakapotajwa, na atakapoapishwa ktk nafasi hiyo.
 
Wewe kapuku utaendelea kufukuza upepo sana kwa mwaka wa 2 mwingine.

Hizo buku 7 ndio zitakuwa kifuta jasho chako.
 
Hili linatusaidia nini sisi? Na yakiwa madogo linatusaidia nini?
 
Back
Top Bottom