Hizi timu mbili Simba na yanga ni Kama wanakaa meza moja kufanya mambo .
Nina wasiwasi Wana makubaliano yao kuwa wewe tawala misimu kadhaa na Mimi ntakupokea misimu kadhaa ni kama biashara fulani ivi, maana haiwezekani timu km ya Simba ambayo imefika mbali ianze kuporomoka gafla na kuja na mbinu zile zile ambazo ziliwaferisha watani zao yanga misimu kadhaaa.
Mtu lazima upate mashaka kidogo ,inawezekana vipi kwenye usajir ukaacha kusajir wachezaji wa maana na kusajir mchezaji mmoja chama na huku ukiwategemea akina nyoni ,bocco, Gadiel ,mhilu,mwanuke ,kagere ,mugalu eti wakufikishe nusu final shirikisho!!
Why makosa Yale Yale yaendelee kujirudia msimu na msimu .
Ivi hapo Simba kitengo Cha kusajir kipoje au kila kiongozi analeta mchezaji wake.
Za chini chini inasemekana matola anapambana Sana Wawa na bocco na mugalu wabakie msimu ujao maana Ana kamisheni zake toka kwa hao jamaa ,je huu ndio mpira wa kufika mbali?
Niwe mkweli tu hata msimu ujao naiona Simba ikikosa ubingwa na kufanya vibaya club bingwa maana uswahili na ubahili plus upigaji vimetawala hapo msimbazi.
Tunakosa hata nguvu za kwenda viwanjan sabab ya huu ujinga wa wazwaz.pia Simba haijifunz tu kuwa safar hii timu ni za Moto Sana Hakuna urahis hata kidogo ,Ila acha iwe hivyo nadhan viongozi wanatamani siku moja waje washikiwe mabango au kupigwa mayai viza na mashabik ndipo wataelewa uchungu na maumivu wanayopata mashabiki.
Hamna pesa semeni mashabiki wachangie ,lengo timu iwe imara tu acheni blabla
Hizi 10percent zikikomeshwa nadhani tutaenda sawa kabisa ,Kuna viongozi hapo Simba wanapaswa kuchungwa kwa jicho Kali Sana .