Usajili wa Usajili wa Simba umewaingiza choo cha kike wanahabari uchwara

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Hii ni heshima kubwa kwa club yangu Simba SC. Simba sio club ya vichochoroni mpaka mipango yake ivuje kwenye vijiwe vya kahawa.

Sajili zote maingizo mapya hakuna uliovuja. Beki wa Singida United hata tetesi tu hazikuwahi kupatikana achilia mbali wale maproo kutoka Brazil na Sudan.

Imefikia kipindi media zimekubali yaishe nazo zinasubiri saa 7 mchana,na sio kuvujisha sajili kama kipindi kilichopita. Kifupi wamekuwa wapole.

Simba ni taasisi kubwa.
 
Katika miaka ya karibuni uandishi hasa wa magazeti ya michezo ni kama magazeti ya udaku.

habari ni uongo mtupu na kupambatu ili kuvutia wanunuzi lakini ukinunu kusoma habari nitofauti kabisa na kichwa cha habari.

hapa nadhani wizara ya habari inatakiwa itoe darasa kwa waandishi pamoja na wahariri wa magazeti maana huku ni ujambazi wa kuwaibia wasomaji kwa habari za udaku.
 
Sinunuagi magazeti ya michezo mana habari nyingi ni uwongo na tetesi,mengi ukweli ni msimamo wa ligi tu mengi uwongo
 
Katika Sekta zote kuazia kwenye Siasa(Utawala na menejimenti) Tunaendesha na kuishi kwa propaganda ili kupata mkate wa kila siku/kufanya mambo yaonekane yanaenda! Hivi vyombo vya habari navyo vinasaka mkate! Suala la kujiuliza hivi wanapateje wateja....jibu lake ndio Watanzania tulivyo! Kama kuna Watanzania Hawajui wanapoumwa waende wapi; kuna wengine wanatembea kilomita 10 kupanga foleni ya kuchota maji ya kunywa,na bado wanaona wanastahili na wanawapigia makofi viongozi unashangaa nini Mhariri kupamba gazeti lake kwa Rangi Nyekundu au kijani ..SIMBA YAJIBU MAPIGO au YANGA YAIMALIZA SIMBA!
 
Kwa iyo biashara ya magazeti imeingiliwa na wataalam wa propaganda?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…