Usalama wa Kununua Vitu Mtandaoni (Online Trade Assurance) Tanzania

Usalama wa Kununua Vitu Mtandaoni (Online Trade Assurance) Tanzania

Samedi Amba

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2018
Posts
227
Reaction score
178
Habari wanajamvi,

Natumaini wote tunaendelea vizuri.

Moja kwa moja kwenye mada...

Nimekuwa mdau wa kununua vitu mtandaoni kwa muda mrefu. Imenilazimu sana kumtuma mtu endapo nafanya biashara na "mgeni" nisiyemfahamu. Kwa mfano, mwaka jana nilinunua laptop kwa mdau mmoja Mwenge, DSM. Ilinibidi kumtuma rafiki yangu kukagua mashine, na kunipa jibu kabla sijafanya muamala.

Aliponihakikishia, nilituma pesa kwa namba ya jamaa (muuzaji). Mara simu ikawa haipatikani. Kiwewe hichooo! Sema nadhani mtandao ulicheza na baadaye akanihakikishia kuwa fedha alipata. Tukamaliza mchezo.

Huwa nawaza kwa sauti... Hivi haiwezi kufika siku kukawa na "mfumo kati", yaani mfumo unaoniruhusu kununua bidhaa kwa usalama?

Wanavyofanya alibaba:
1. unaenda mtandaoni,
2. unatafuta laptop inayouzwa,
3. unaweka fedha kwenye mfumo,
4. jamaa anatuma laptop
5. unahakikisha ndo yenyewe
6. "unaruhusu" fedha. Yaani inaingia kwenye account yake na anakuwa na uwezo wa kutoa.

Hofu yangu ni kwamba wafanyabiashara wengi ni watu wa "papo hapo". Nahisi huenda wasiwe na subira ya kusubiri uhakiki huu.

Hivi, tofauti na kumtuma unayemwamini, je kuna njia mbadala? Je, kuna kampuni wanaoweza kufanya ukaguzi wa mzigo kabla haujatumwa? Au tafanyaje kuongeza usalama wa biashara mtandaoni?
 
Habari wanajamvi,

Natumaini wote tunaendelea vizuri.

Moja kwa moja kwenye mada...

Nimekuwa mdau wa kununua vitu mtandaoni kwa muda mrefu. Imenilazimu sana kumtuma mtu endapo nafanya biashara na "mgeni" nisiyemfahamu. Kwa mfano, mwaka jana nilinunua laptop kwa mdau mmoja Mwenge, DSM. Ilinibidi kumtuma rafiki yangu kukagua mashine, na kunipa jibu kabla sijafanya muamala.

Aliponihakikishia, nilituma pesa kwa namba ya jamaa (muuzaji). Mara simu ikawa haipatikani. Kiwewe hichooo! Sema nadhani mtandao ulicheza na baadaye akanihakikishia kuwa fedha alipata. Tukamaliza mchezo.

Huwa nawaza kwa sauti... Hivi haiwezi kufika siku kukawa na "mfumo kati", yaani mfumo unaoniruhusu kununua bidhaa kwa usalama?

Wanavyofanya alibaba:
1. unaenda mtandaoni,
2. unatafuta laptop inayouzwa,
3. unaweka fedha kwenye mfumo,
4. jamaa anatuma laptop
5. unahakikisha ndo yenyewe
6. "unaruhusu" fedha. Yaani inaingia kwenye account yake na anakuwa na uwezo wa kutoa.

Hofu yangu ni kwamba wafanyabiashara wengi ni watu wa "papo hapo". Nahisi huenda wasiwe na subira ya kusubiri uhakiki huu.

Hivi, tofauti na kumtuma unayemwamini, je kuna njia mbadala? Je, kuna kampuni wanaoweza kufanya ukaguzi wa mzigo kabla haujatumwa? Au tafanyaje kuongeza usalama wa biashara mtandaoni?
Kwa uelewa mchache ni kwamba "Africa is a peculiar market". Sisi tunanamna yetu ya kufanya biashara mtandaoni ambazo e-commerce companies za Tanzania zinabidi zikae na wateja wao kueleweshwa somo hili. Mteja ndio anasiri ya jinsi angependa vitu viende hadi anapata bidhaa zake kwenye kila category ya bidhaa.
Kuna marketplace (e-commerce platform) inayokuwa hatua kwa hatua inayoitwa Sambazah.co wameweka mifumo ya kumlinda muuzaji na mteja kila wakati wa kufanya biashara. Kwa sasa wameanza na niche ya vitabu tu na wanatumai kuingia kwenye category zingine.
 
Back
Top Bottom