Elections 2010 Usalama wa Taifa wakanusha tuhuma za Dr. Slaa

Elections 2010 Usalama wa Taifa wakanusha tuhuma za Dr. Slaa

Status
Not open for further replies.
kwani wao ni usalama wa taifa upi, kwa kuwa madai ya dr slaa ni mazito na anasema anao ushahidi kwani kama sehemu ya usalama wa taifa wasilichunguze hilo?
Sidhani kama itakuwa busara kwa wao kuchunguza hili kwa sababu nao ni watuhumiwa.

Can we have an independent body, even from oputside the country, kuchunguza na kuleta ukweli wa mambo?

Madai ya Slaa sidhani kama ni ya kupuuzwa hivihivi hasa ukizingatia kauli ya jaji Makame kuwa huwa 'wanarekebisha' matokeo ya uchaguzi wanayoyapokea kutoka kwa wasimamizi pale wanapobaini kuwa yana makosa
 
Wameitisha Press Conference imehutubiwa na Naibu Mkurugenzi bwana Jacky Mugenzi kuwa hawahusiki kwa namna yoyote na uchakacghuaji wa kura za urais.

Source: Mimi mwenyewe

tupe habari kamili wamejibu wapi na saa ngapi?

Katika dunia ya leo si makosa kutoa habari kwa wananchi ikibidi. Kumbuka katika siasa jambo la uongo lisipokanishwa hugeuka kuwa la kweli.

Kukaa kimya kwa chombo nyeti kama hicho si kosa na kutoa maelezo naona ni sawa.
 
Mkuu wa idara ya usalama wataifa amejitokeza leo na kukanusha tuhuma zilizotolewa jana na Dr.Slaa kuhusiana na tuhuma za idara hiyo kushiriki katika zowezi la wizi wa kura za urais. Akizungumza na TBC leo Mchana kwenye taarifa ya habari Mkuu wa idara hiyo amesema

"Dr.Slaa ameingizwa mjini na na watu waliyo jifanya ni usalama wataifa,hakuna kitu kama hicho, sisi hatuna chama, tupo kwajili ya taifa na siyo chama chochote. Na mtuka kama anaushaidi ajitokeze na auweke wazi.. Najua ameingizwa mjini na na watu waliyo jifanya ni usalama wa taifa ambao sisi hatuwatambui."


Style hii aliyo tumia mkuu wa idara hii ni style inayotumiwa na Russia kuwakana watu waliyo tumwa kufanya kazi na atimaye kuboronga na kukamatwa au kugundulika, Njia hii inatumika kujisafisha...

Nakumbuka mwaka 1978 Mzee wangu alitumwa kwenda kufanya upelelezi nchini Uganda akiwa na wenzie 8, waligundulika na kukamatwa Na serikali iliwakana na kusema haiwatambui na haijawatuma bali walikuwa na mambo yao binafsi...


Na muomba Dr.Slaa asikatishwe tamaa na majibu haya bali akusanye ushaidi na kuutoa hadharani ili kuwaumbua hawa wote..
 
Ili kupata muafaka ni bora malinganisho ya madai ya Dr.SLAA dhidi ya uchakachuaji yakafanyiwa kazi kuliko kukanusha tu.Hapa inabidi wawe objective zaidi ya kuwa subjective. SLAA amesema nazo takwimu basi zifanyiwe kazi kuliko kuendelea kurumbana.Time is running out you know!!!!!
I strongly agree with you brother.
 
Wameitisha Press Conference imehutubiwa na Naibu Mkurugenzi bwana Jacky Mugenzi kuwa hawahusiki kwa namna yoyote na uchakacghuaji wa kura za urais.

Source: Mimi mwenyewe

Mtuhumiwa huwa hakubali kosa. Mtakumbuka hata Mgonja alipotuhumiwa na Dr. Slaa pale Mwembeyanga aliitisha Press conference kupinga.

Nemo iudex in causa sua (No one can be a judge on his own cause).
 
Tusibiri Takwimu za Dr Slaa na majibu ya Tume ya Taifa ndipo tutakuwa na mengi ya kusema. Hawa Tiss tutakuwa tunawaonea kwa kuwa kazi yao haiwaruhusu kusemasema kama jeshi la polisi tutakuwa hatuwatendei haki. Na kwa kweli kama wamefikia kukanusha nawapongeza sana ni hatua kubwa kuelekea demokrasia ya kweli.

Sheria iko wazi chombo cha kuratibu na kusimamia uchaguzi ni Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) si TISS hivyo tuwabane hao hao NEC watakuwa na maelezo kama hizo ni tuhuma za kweli au ni za uongo.
 
Kama kuna idara ya serikali inatakiwa kuwajibika kwa uhalifu dhidi ya wananchi ni hii ya usalaama wa Taifa ambayo kutokana na utendaji kizembe nchi imepata hasara kubwa kabisa. Hapa kuna moja kati ya facts hizi mbili:

Ya kwanza ni labda hawaelewi kwamba wajibu wao si kumlinda Rais na viongozi wa serikali tu bali kulinda hujuma dhidi ya taifa kama zile za kufuru ya wizi uliofanyika Benki Kuu wa EPA, Benki Kuu ndiyo kidundio (Apex) cha moyo wa taifa lolote ambapo hujuma yoyote dhidi yake ni sawa na angamizo la uchumi. Zipo pia hujuma za Mikataba ya rushwa, Richmond, Meremeta, Kiwira n.k. zimetendeka wakiwa busy "kuwalinda " wahujumu hawa wa uchumi wetu ambao kwa kweli ndiyo maadui wa kweli wa nchi yetu. Na sasa ndiyo tunapata kichefuchefu kabisa kusikia wamehusika na vote rigging zinazolenga kuharibu utashi wa wananchi!

Pili ni kwamba huenda wanadhani wanapaswa kuwajibika kwa viongozi wanaowateua, lakini sijui kama wanajishughulisha kuelewa mishahara wanayolipwa inagharimiwa na nani.

Usalama wa taifa wa kwetu wanafanya kazi ki-primitive kwelikweli, hebu angalia; wenzetu kule Marekani walikuwa usalama wa Taifa wao waliogundua hila alizotumia Rais Nixon kushinda uchaguzi walimpeleleza, wakawakabidhi Polisi ambao waliwasilisha tuhuma Bungeni ambapo baada ya kuzithibitisha wengi walichukuliwa hatua na Rais kulazimishwa kuachia ngazi. Mambo ni hivyohivyo kule Uingereza ambako kina Chenge waligunduliwa kugawana rushwa ya ununuzi wa Rada na Ndege. Hapa hakuna cha Usalama wa Taifa wala kitengo cha upelelezi chenye ubavu wa kufanya hivyo, labda ni kwa sababu ya kulipwa fadhila ya kupewa ulaji na Rais ambaye anayo pia madaraka ya kuwaondoa hata kwa kuwaonyeshea kidole tu.

Kwa mtaji huu Usalama wa taifa wataendelea kuwa mzigo wa taifa na aibu kubwa kwa nchi yetu.

 
TISS wangekaa kimya tungesema wameiba ndio maana hawana la kutueleza na sasa wamejitokeza kutuhabarisha tunasema wanajichanganya. Ni lipi jema?

Binafsi naona dunia ya sasa ni ya uwazi zaidi si vibaya kwa TISS kujitokeza kuwaeleza wananchi jambo linaloweza kuhatarisha usalama wa Taifa hasa kama itaaminika miongoni mwetu na wale wasipenda kutafiti kabla ya kusema kwamba TISS wamechachua kura za SLAA.

Good show
 
Mwenye macho haambiwi Tazama,hapa ndo hata wale waliokua wamepuuza hizo habari watataka kuzijua zaidi.Kwanini aseme hawajui kama anauhakika hawakuhuusika?Tutafakari na tuchukue hatua.
 
vifupisho vingine havifai........uwt pia ni umoja wa wanawake tanzania
 
ni wazi kuwa, wizi tena mkubwa umefanywa!haiwezekani watu wakukimbize kwa mawe alafu wakupe kura,
lengo ni kutoa meseji ya udanganyifu kwa wananchi kuwa wanakubalika wakati tumeona wazi mwitiko wa nchi nzima!

Sisi sio watoto!

Makame naona astaafu make kwa umri alionao si mtu wa kusiamia chombo kama hicho alafu msitegemee kama uchakachuaji utaisha ikiwa hatutaamka na kushinikiza katiba mpya amabyo inampa rais mamlaka machache kwani kama makame kapewa kazi na kiwete untegemea nini???

TUNATAKA KATIBA MPYA ILI DHURMA NA UDHARIMU WAO UKOMESHWE!
 
Mkuu wa Idara hiyo anasema Slaa ameingia kichwa kichwa, mtu mwenye akili timamu anaweza kuongea maneno ya namna hii kweli kwa mtu mzima kama Dr. Slaa? kuwa ameingia kichwa kichwa? Siku zao zimetimia na sasa wanatapa tapa
 

Kama kuna idara ya serikali inatakiwa kuwajibika kwa uhalifu dhidi ya wananchi ni hii ya usalaama wa Taifa ambayo kutokana na utendaji kizembe nchi imepata hasara kubwa kabisa. Hapa kuna moja kati ya facts hizi mbili:

Ya kwanza ni labda hawaelewi kwamba wajibu wao si kumlinda Rais na viongozi wa serikali tu bali kulinda hujuma dhidi ya taifa kama zile za kufuru ya wizi uliofanyika Benki Kuu wa EPA, Benki Kuu ndiyo kidundio (Apex) cha moyo wa taifa lolote ambapo hujuma yoyote dhidi yake ni sawa na angamizo la uchumi. Zipo pia hujuma za Mikataba ya rushwa, Richmond, Meremeta, Kiwira n.k. zimetendeka wakiwa busy "kuwalinda " wahujumu hawa wa uchumi wetu ambao kwa kweli ndiyo maadui wa kweli wa nchi yetu. Na sasa ndiyo tunapata kichefuchefu kabisa kusikia wamehusika na vote rigging zinazolenga kuharibu utashi wa wananchi!

Pili ni kwamba huenda wanadhani wanapaswa kuwajibika kwa viongozi wanaowateua, lakini sijui kama wanajishughulisha kuelewa mishahara wanayolipwa inagharimiwa na nani.

Usalama wa taifa wa kwetu wanafanya kazi ki-primitive kwelikweli, hebu angalia; wenzetu kule Marekani walikuwa usalama wa Taifa wao waliogundua hila alizotumia Rais Nixon kushinda uchaguzi walimpeleleza, wakawakabidhi Polisi ambao waliwasilisha tuhuma Bungeni ambapo baada ya kuzithibitisha wengi walichukuliwa hatua na Rais kulazimishwa kuachia ngazi. Mambo ni hivyohivyo kule Uingereza ambako kina Chenge waligunduliwa kugawana rushwa ya ununuzi wa Rada na Ndege. Hapa hakuna cha Usalama wa Taifa wala kitengo cha upelelezi chenye ubavu wa kufanya hivyo, labda ni kwa sababu ya kulipwa fadhila ya kupewa ulaji na Rais ambaye anayo pia madaraka ya kuwaondoa hata kwa kuwaonyeshea kidole tu.

Kwa mtaji huu Usalama wa taifa wataendelea kuwa mzigo wa taifa na aibu kubwa kwa nchi yetu.


Mimi nadhani kushindwa kugundua uhalifu wa jambo fulani si kosa katika mambo ya ujasusi kwani hata marekani walipovamia Irak walituambia Sadam Hussein ana silaha za maangamizi.

Naona ni Kosa kwa majasusi kujua kwamba mahali fulani kuna uhalifu na kutouzuia. Dunia yote ya vyombo ya upepelezi kuna mapungufu ambayo hujitokeza kama sehemu ya kazi hiyo halikadhalika katika taasisi za kawaida za binafsi na umma.

si nia yangu kuwatetea hawa jamaa kama wanasitahili kulaumiwa ila naamini ni Mungu peke yake ambaye hakosei. Daima kwa sisi binadamu tunaangalia kama kulikuwa na uzembe katika kushindwa kuzuia tukio na si kushindwa kutambua tukio. Kumbuka Majasusi ni binadamu wanaotafuta habari za binadamu wenzao ambao pia wana akili kama hao majasusi na mbinu za uhalifu za kimataifa zinapenya kutoka taifa moja kwenda kwingine.

Kumkamata mhalifu ni kazi nguvu kama ilivyo kumfumania mwenzi wako wa ndoa ingawa jamii inayotuzunguka itatubeza kwamba ni ujinga kwa mke au mume kushindwa kufahamu kuwa mwenzi wako anatembea nje lakini jamaa haoni. Lakini kumbe kwa hakika hujui kama mwandani wako anatembea nje ya ndoa hadi pale raia mwema atakapojitokeza na kukuambia.

Hii ina maana gani, Usalama wa Taifa ni sisi sote. Mtanzania wenye nia njema na nchi hii anatakiwa kuwa karibu na taasisi hii na kutoa taarifa kwao katika ofisi zao zilizotapakaa nchi nzima. Baada ya kuwapa taarifa tunasitahili kupima uwezo wao. Wapo Watanzania wenzetu wanafanya kazi BOT walikaa kimya bila kutoa taarifa za EPA naamini na wao sio wazalendo wana sehemu ya lawama hizi, haiwezekani kwamba BOT wote hawakujua jambo hili na kulipeleka katika vyombo husika ikiwemo Usalama wa Taifa. Kamwe Watanzania tusitegemee maajabu kama tutaendelea kukalia taarifa zenye kukinzana na maslahi ya Taifa letu na kusubiri mpaka Usalama wa Taifa wapeleleze na kuzuia.
 
Kama kuna idara ya serikali inatakiwa kuwajibika kwa uhalifu dhidi ya wananchi ni hii ya usalaama wa Taifa ambayo kutokana na utendaji kizembe nchi imepata hasara kubwa kabisa. Hapa kuna moja kati ya facts hizi mbili:

Ya kwanza ni labda hawaelewi kwamba wajibu wao si kumlinda Rais na viongozi wa serikali tu bali kulinda hujuma dhidi ya taifa kama zile za kufuru ya wizi uliofanyika Benki Kuu wa EPA, Benki Kuu ndiyo kidundio (Apex) cha moyo wa taifa lolote ambapo hujuma yoyote dhidi yake ni sawa na angamizo la uchumi. Zipo pia hujuma za Mikataba ya rushwa, Richmond, Meremeta, Kiwira n.k. zimetendeka wakiwa busy "kuwalinda " wahujumu hawa wa uchumi wetu ambao kwa kweli ndiyo maadui wa kweli wa nchi yetu. Na sasa ndiyo tunapata kichefuchefu kabisa kusikia wamehusika na vote rigging zinazolenga kuharibu utashi wa wananchi!

Pili ni kwamba huenda wanadhani wanapaswa kuwajibika kwa viongozi wanaowateua, lakini sijui kama wanajishughulisha kuelewa mishahara wanayolipwa inagharimiwa na nani.

Usalama wa taifa wa kwetu wanafanya kazi ki-primitive kwelikweli, hebu angalia; wenzetu kule Marekani walikuwa usalama wa Taifa wao waliogundua hila alizotumia Rais Nixon kushinda uchaguzi walimpeleleza, wakawakabidhi Polisi ambao waliwasilisha tuhuma Bungeni ambapo baada ya kuzithibitisha wengi walichukuliwa hatua na Rais kulazimishwa kuachia ngazi. Mambo ni hivyohivyo kule Uingereza ambako kina Chenge waligunduliwa kugawana rushwa ya ununuzi wa Rada na Ndege. Hapa hakuna cha Usalama wa Taifa wala kitengo cha upelelezi chenye ubavu wa kufanya hivyo, labda ni kwa sababu ya kulipwa fadhila ya kupewa ulaji na Rais ambaye anayo pia madaraka ya kuwaondoa hata kwa kuwaonyeshea kidole tu.

Kwa mtaji huu Usalama wa taifa wataendelea kuwa mzigo wa taifa na aibu kubwa kwa nchi yetu.

Angalai accountability za CIA, KGB, MI6, MOSSAD na zingine halafu linganisha na hii ya kwetu............nadhani utapata jibu
 
Huyu bwana Nzoka hakupaswa kusema chochote so far, kajidhalilisha sana, kama kuna watu wamemshauri basi si washauri wazuri, hizi njaa na kiherehere ndio vinawafanya watu wafanye vitu wasivyovijua bila kujua athari zake ni nini,yeye kaona sifa sana kwenda kukanusha bila kufikiria akifanya hivyo jamii itamchukuliaje.

Tunaamini usalama wa taifa ni serikali na haina chama na wala haitakiwi kufungamana na chama chochote lakini sisi tunawaangalia tu mnavyojikomba na kushindwa kufanya kile mnachotakiwa kufanya,hii ni fedheha na ni mpya sijawahi kusikia.
 
Wameitisha Press Conference imehutubiwa na Naibu Mkurugenzi bwana Jacky Mugenzi kuwa hawahusiki kwa namna yoyote na uchakacghuaji wa kura za urais.

Source: Mimi mwenyewe

Duu?? nina wasi wasi kama hawa watu wanafahamu wajibu wao!
Kwani swala ni wao kukanusha kwamba hawajahusika? kwa maana hiyo wanatwambia uchakachuaji upo ila si wao walo ufanya?

Nilidhani wao walivo mashushu wa taifa ni wajibu wao kuhakikisha hamna uchakachuaji kwa kufahamu mbinu zote za wachakachuaji na kuwazuia ili wasihatarishe amani na usalama wa nchi yetu, lakini pia demokrasia ya nchi yetu isibakwe!
 
hwakupaswa kujibu

TISS hawana maana mambo ya siasa haya
 
Mida hii kuna newz bar zinapita ITV kwamba usalama wa Taifa wamejibu tuhuma zilizoelekezwa kwao na DR Slaa kwamba wamemsaidia JK kushinda kwa kupunguza kura zake na kumuongezea JK, cha ajabu badala ya kujibu tuhuma in reference to evidence anazotoa Dr. Slaa ,wao wanatoa jibu la jumla kwamba Dr. Slaa anapotoshwa na wanausalama wa Taifa ambao ni feki.

Hii ndiyo Usalama wa Taifa tulionayo, badala ya kulinda masilahi ya Nchi wao wako bize kulinda watawala,shame on them.
 
Wameitisha Press Conference imehutubiwa na Naibu Mkurugenzi bwana Jacky Mugenzi kuwa hawahusiki kwa namna yoyote na uchakacghuaji wa kura za urais.

Source: Mimi mwenyewe
Kwa hiyo bwana source wanakiri kuwa kura za uraisi zimechakachuliwa ..............ila wao hawakuhusika??
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom