Ushabiki wa Simba na Yanga wageuka uadui

Mwl Philemon

Member
Joined
Nov 29, 2018
Posts
63
Reaction score
70
Kwa yanayoendelea sasa kwenye mpira wetu ni ujinga na upumbavu mkubwa kuoneshwa na wapenda maendeleo ya michezo hususan huu mchezo pendwa wa mpira wa miguu.

Ndani ya siku tatu kumekuwa na matukio yasiyo ya kuvutia kwa wanamichezo wa kweli. Lilianza la Ali kamwe kumshambulia kwa maneno ya kejeli Kocha Juma Mgunda jambo ambalo si la kimchezo. Kama Ali ana chuki binafsi na Mzee yule angetafuta namna nyingine kumtusi au kufikisha ujumbe wake si Timu yetu pendwa.

Na pili ni hili la Mashabiki wa soka kushangilia kwa furaha kifo cha shabiki mwingine kisa ni shabiki wa timu nyingine huu si mchezo wala utani wa jadi bali ni uadui na chuki inayoendelea kujengeka ndani yetu. Lisipokemewa litakuja kuleta maafa makubwa baadaye.

Tubadilike huu ni ushamba katika michezo. Kama huna cha kufurahia kwenye mechi fulani achana nayo. Kama huna cha kujifunza kwa mwingine achana nae.

Haya majibizano ni upuuzi mtupu.
 
Shida ni unafki Kwa hiz timu mbili me Bora nijitoe tu maana hata huku mtaan ishakua vita hakuna utan ule wa asilia watu Wananuna had Kaz haziend huku makazin ,mtu ananuna et kisa yanga na Simba ,ushamba huu.
Ntasimama na Mbeya city timu ya home ,hawa yanga na Simba hapana Kwa sasa
 
Shida iko ktk mamlaka tulizo nazo ( si TFF, wizara, waziri, etc..etc) uwezo wa kuangalia mambo kwa jicho la mballi.

Hizi mbegu za chuki zimepandwa na zinaendelea kuota tangu enzi za Manara...Muro...na sasa Kamwe.

makosa kama haya mamlaka zichukue hatua serious kulinda afya ya mchezo ni starehe.

Usiogope kuwafungia miezi hata kama utawaudhi fulani.
 
Dawa ILITAKIWA Azam awe anafanya vizuri. Msipo Huu mgawanyiko wa u Simba na U yanga utakufa.

Mfano south Africa .
Kaiiser CHEEF
Na orando pirates ndio watani WA jadi.


Ameibuka MAMelody miaka 10 yote hawana UBINGWA psl
 
Hicho ni kipimo Cha IQ, unashindwa kuelewa kuwa ni Tz imecheza na sio Yanga. Uzalendo uko wapi?
 
Dawa ILITAKIWA Azam awe anafanya vizuri. Msipo Huu mgawanyiko wa u Simba na U yanga utakufa.

Mfano south Africa .
Kaiiser CHEEF
Na orando pirates ndio watani WA jadi.


Ameibuka MAMelody miaka 10 yote hawana UBINGWA psl
hii ndio dawa yao lakini Azam nao wajinga sana
 
.
 
Mtajuana na matimu yenu ndio maana Huwa sishabikii ila tuu kwenye michezo ya Kimataifa..

Kwa huo ujuha wenu acheni msiende kuzikana..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…