Pamoja na kwamba Bunge la Kenya limemuondoa Madarakani Naibu wa Rais aitwaye Gachagua, Na kufikia hata kumpitisha Naibu Mpya aliyeteuliwa na Rais William Ruto, Lakini shughuli yote hiyo imezimwa na Mahakama ya Nchi hiyo.
Hii ni Baada ya Bwana Gachagua kuwasilisha pingamizi Mahakamani, Akipinga kuondolewa kwake kwa alichodai hakukufuata Utaratibu, Mchakato huo utaendelea baada ya Mahakama kusikiliza kesi hii iliyofunguliwa kwa hati ya dharula, na kama Mahakama hiyo itakubaliana na madai ya Gachagua aweza kurejeshwa Madarakani.
Jambo hili haliwezi kufanyika Nchini Tanzania, Haingewezekana kwa namna yoyote ile hata ikibidi kwa gharama ya Majaji na Gachagua mwenyewe kupotea ama kutekwa, Kwa Tanzania kauli ya Viongozi ina nguvu kuliko Amri Kuu za Mungu (Mifano ya Jambo hili tukiiweka hapa basi JF itajaa)
Soma Pia:
Kwa kadri ya Maono yangu Kenya haikupaswa kuwemo kwenye Jumuiya ya Africa Mashariki, kulikojaa viongozi Madikteta wasioheshimu Katiba walizoapa kuzilinda tena kwa kushika vitabu vya dini zao kwenye mkono wa Kulia.
Nitajaribu kuishawishi Kenya ijiondoe kwenye Jumuiya ya Africa Mashariki ili kulinda Heshima yake
Mungu Ibariki Jamhuri ya Watu wa Kenya