Ushahidi, Wazungu wana Akili kuliko sisi

Ushahidi, Wazungu wana Akili kuliko sisi

Kijakazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
7,093
Reaction score
10,469
Haya ni maonyesho yaliyoandaliwa na Wazungu (Umoja Wa Mataifa) kuhusu kile kilichotokea huko Ulaya wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia! Maonyesho hayo yalihusu hasa mauaji ya Wayahudi huko Ulaya!

Kilichonigusa hasa na kunifanya mpaka niandike hapa ni jinsi Wazungu walivyofanya haya maandalizi, kwanza aina ya wanafunzi waliokuja ni wa kutoka Shule za kawaida kabisa za Serikali za kata yaani Mtz wa kikawaida, lkn kama hii shughuli ingeandaliwa na Serikali yetu (sisi Watz weusi) basi Wanafunzi ambao wangepata fursa hii wangetoka Shule za binafsi kama Al Muntazir, International school, St Marys n.k yaani shule za Watoto wa kidosi!

Pili kilichonivutia zaidi kuhusu haya maandalizi yaliyofanywa ni Wazungu ni Lugha iliyotumika, Wazungu wameamua kutumia Lugha ya Kiswahili lkn kama hii ingefanywa na Mtz Mdiaspora kama John Mashaka basi lazima wangeandika kwa Kiingereza ingawaje mlengwa ni Mtz wa kawaida!

Hii imenifundisha moja ya kwamba Wazungu ni kweli kabisa wana akili sana kuliko sisi!

attachment.php
attachment.php
attachment.php
attachment.php
attachment.php

 
Basi sawa! maana umejustify conclusion yako based on what you think is correct.
 
Basi sawa! maana umejustify conclusion yako based on what you think is correct.

Angekuwa Mzungu ndiyo anajibu huyo ujumbe basi angeandika kwa kiswahili au hata angetafuta Mkalimani lakini kamwe asingeweza kuchanganya lugha kama ulivyofanya, Ushahidi mwingine wa kuwa na akili ndogo!
 
Angekuwa Mzungu ndiyo anajibu huyo ujumbe basi angeandika kwa kiswahili au hata angetafuta Mkalimani lakini kamwe asingeweza kuchanganya lugha kama ulivyofanya, Ushahidi mwingine wa kuwa na akili ndogo!

ungekuwa umesoma lugha usingetoa maoni ya kipumbavu.....mtu anaweza kuchanganya lugha mbili katika maongezi(code switching) ili kuonyesha msisitizo na sababu zingine pia...sasa wewe umekimbilia hitimisho angekuwa mzungu asingefanya hivyo..kama unaona wana akili sana tafuta mwanaume mwenzako/mwanamke mwenzako akuoe kama wanavyofanya wao
 
Nianze kwa kusema kwamba wewe ni Fisi Maji. Nina haki ya kukutukana sababu hujitambui. Nakuelewesha, Fisi maji ni TUSI. Upo hapo????!!!
Kwa mawazo yako, utaendelea kuwa mpumbavu milele na milele na nakuombea kwa Mungu usirithishe hii kwa watoto wako!! Ni laana!
 
we mleta uzi sio mzima,au labda utuambie kabla ya kupost kuna kitu ulitumia?
 
ungekuwa umesoma lugha usingetoa maoni ya kipumbavu.....mtu anaweza kuchanganya lugha mbili katika maongezi(code switching) ili kuonyesha msisitizo na sababu zingine pia...sasa wewe umekimbilia hitimisho angekuwa mzungu asingefanya hivyo..kama unaona wana akili sana tafuta mwanaume mwenzako/mwanamke mwenzako akuoe kama wanavyofanya wao

Ni Waafrika tu ndio hufanya hivyo!

Mzungu, Mchina au hata Mpersia na Mwarabu hata siku moja hawezi kuchanganya lugha, aidha ataongea kama ni Kiswahili basi ni Kiswahili TU, na kama hawezi Kiswahili basi atakwambia na ataongea Kiingereza TU! Watu wengine nje ya sisi waafrika hawana mambo ya kuchanganya Lugha!

Naangalia vyomba vya Habari vya nje kila siku kama Mzungu anaongea Kiingereza basi atongea Kiingereza tu na kama Mchina anaongea Kichina basi ataongea Kichina na SIYO Kichina na kuchanganya na Kingereza, au hata kama Muirani anaongea Kiirani basi ataongea Kiirani tu na siyo kuchanganya Kiirani na Lugha nyingine, hiyo ya kuchanganya ni Waafrika tu tena sisi weusi tu lakini Waafrika wa Kaskazini huwa hawafanyi hivyo atongea Kiarabu tu au Kiingereza tu kama kuna ulazima, hata Ethiopia nimefika huko Watu aidha wataongea kikwao tu au kiingereza kama ikibidi lkn kamwe hawachanganyi hivyo kuchanganya ni kwa kwa watu weusi tu wa Waafrika!
 

Ni Waafrika tu ndio hufanya hivyo!

Mzungu, Mchina au hata Mpersia na Mwarabu hata siku moja hawezi kuchanganya lugha, aidha ataongea kama ni Kiswahili basi ni Kiswahili TU, na kama hawezi Kiswahili basi atakwambia na ataongea Kiingereza TU! Watu wengine nje ya sisi waafrika hawana mambo ya kuchanganya Lugha!

Naangalia vyomba vya Habari vya nje kila siku kama Mzungu anaongea Kiingereza basi atongea Kiingereza tu na kama Mchina anaongea Kichina basi ataongea Kichina na SIYO Kichina na kuchanganya na Kingereza, au hata kama Muirani anaongea Kiirani basi ataongea Kiirani tu na siyo kuchanganya Kiirani na Lugha nyingine, hiyo ya kuchanganya ni Waafrika tu tena sisi weusi tu lakini Waafrika wa Kaskazini huwa hawafanyi hivyo atongea Kiarabu tu au Kiingereza tu kama kuna ulazima, hata Ethiopia nimefika huko Watu aidha wataongea kikwao tu au kiingereza kama ikibidi lkn kamwe hawachanganyi hivyo kuchanganya ni kwa kwa watu weusi tu wa Waafrika!

Sababu ni kwamba hao uliwataja hapo toka mashuleni kwao, yaani shule za msingi, secondary na chuoni hawatumii lugha nyingine kufundishia. Wanatumia lugha zao kama lugha kuu za kufundishia. Kiingereza wanakitumia kama lugha ya ziada.
 
Kama huna akili ni wewe sio uchanganye Waafrica wote kama ni maboga. Kwanza rangi ya mtu kwenye biologia haina tofauti na watu kuwa warefu au wafupi kibiologia rangi ya mtu ni sehemu ndogo tu watu wote ni sawa na mazingira ndiyo yanabadilisha tabia za watu hivyo huwezi kusema sisi tuna akili kwasababu hakuna watu wawili duniani wenye akili sawa hata mapacha!
 
Sababu ni kwamba hao uliwataja hapo toka mashuleni kwao, yaani shule za msingi, secondary na chuoni hawatumii lugha nyingine kufundishia. Wanatumia lugha zao kama lugha kuu za kufundishia. Kiingereza wanakitumia kama lugha ya ziada.

Kama hiyo ndiyo sababu, sasa ni kwanini mapadri wa Kizungu hapa Bongo huwa naongea nao sana lakini hata siku moja hawachanganyi Lugha? Huwa aidha mnaongea kwa Kiswahili na ni moja kwa moja Kiswahili au kama hajui Kiswahili basi Mtaongea kwa Kiingereza moja kwa moja lakini siyo nusu nusu hiyo sijawahi kuiona ila kwa sisi waafrika weusi tu! Hata kwenye mahubiri makanisani huwa (mapadri Wazungu) hawachanganyi Lugha ya Kiswahili na Kiingereza bali atahubiri kwa Kiswahili mwanzo mwisho na kama hawezi Kiswahili basi atachukua Mkalimani, lakini Padri wa Kiafrika mweusi ukiongea naye ni lazima atakuchanganyia Kiingereza na Kiswahili yaani uvugu vugu, huku hayuko na kule pia hayuko!
 
Kama huna akili ni wewe sio uchanganye Waafrica wote kama ni maboga. Kwanza rangi ya mtu kwenye biologia haina tofauti na watu kuwa warefu au wafupi kibiologia rangi ya mtu ni sehemu ndogo tu watu wote ni sawa na mazingira ndiyo yanabadilisha tabia za watu hivyo huwezi kusema sisi tuna akili kwasababu hakuna watu wawili duniani wenye akili sawa hata mapacha!

Hata mimi nilikuwa naamini hivyo siku zote lakini pia kuna UKWELI ambao sasa nashindwa kuulezea kwa mfano hili la Lugha, ni kwa nini Mtz anayetaka kufikisha Ujumbe kwa Watz wenzake anatumia lugha ya Kiingereza wakati Mzungu, Mchina, Muhindi wakitaka kufikisha Ujumbe kwa Watz hutumia Lugha ya Kiswahili?

Kwa hali ya kawaida ungetegemea ya kwamba huyu Mtz aweze kutumia Kiswahili zaidi kwa maana anaelewa ya kwamba watu wake wengi wanaelewa Kiswahili zaidi kuliko Kiingereza sasa hiyo tofauti ndiyo nashindwa kuilezea kwa ni sijawahi kuona Mzungu, Mchina Muirani, Mwarabu akifanya hivi isipokuwa sisi tu, tena Waafrika weusi hata Waafrika wenzetu wa Kaskazini hawafanyi hivi, sasa ni kwa nini?
 
Kama hiyo ndiyo sababu, sasa ni kwanini mapadri wa Kizungu hapa Bongo huwa naongea nao sana lakini hata siku moja hawachanganyi Lugha? Huwa aidha mnaongea kwa Kiswahili na ni moja kwa moja Kiswahili au kama hajui Kiswahili basi Mtaongea kwa Kiingereza moja kwa moja lakini siyo nusu nusu hiyo sijawahi kuiona ila kwa sisi waafrika weusi tu! Hata kwenye mahubiri makanisani huwa (mapadri Wazungu) hawachanganyi Lugha ya Kiswahili na Kiingereza bali atahubiri kwa Kiswahili mwanzo mwisho na kama hawezi Kiswahili basi atachukua Mkalimani, lakini Padri wa Kiafrika mweusi ukiongea naye ni lazima atakuchanganyia Kiingereza na Kiswahili yaani uvugu vugu, huku hayuko na kule pia hayuko!

Ni rahisi kwa wao sababu wanajifunza kiswahili ukubwani, waafika (Tz) tunatoka na huo mfumo toka udogoni!!
Pia binafsi sioni tatizo la kuchanganya lugha wakati wa kuongea.
Pia lugha yetu bado haijitoshelezi baadhi ya maneno, hivyo tunaazima maneno mengi kuongeza msisitizo!
 
Ni rahisi kwa wao sababu wanajifunza kiswahili ukubwani, waafika (Tz) tunatoka na huo mfumo toka udogoni!!
Pia binafsi sioni tatizo la kuchanganya lugha wakati wa kuongea.
Pia lugha yetu bado haijitoshelezi baadhi ya maneno, hivyo tunaazima maneno mengi kuongeza msisitizo!

Sasa ni kwanini wazungu wanaojua Kiswahili kama Mapadri huwa hawachanganyi Lugha yaani Kiswahili na Kiingereza? Lakini Padri wa Kiafrika Mweusi atachanganya Lugha Kiswahili na Kiingereza?
 
Sasa ni kwanini wazungu wanaojua Kiswahili kama Mapadri huwa hawachanganyi Lugha yaani Kiswahili na Kiingereza? Lakini Padri wa Kiafrika Mweusi atachanganya Lugha Kiswahili na Kiingereza?

Hao mapadri wanajifunza kuongea kiswahili ukubwani, ni rahisi kujizuia kwa kutamka maneno wanayotaka na mepesi bila ya kuchanganya na kizungu. Hawajajua Kiswahili kama lugha yao asilia, na hawajaanza kujifunza kiswahili ktk umri mdogo!
 
Hao mapadri wanajifunza kuongea kiswahili ukubwani, ni rahisi kujizuia kwa kutamka maneno wanayotaka na mepesi bila ya kuchanganya na kizungu. Hawajajua Kiswahili kama lugha yao asilia, na hawajaanza kujifunza kiswahili ktk umri mdogo!

Lakini, ni kwanini sisi Waafrika weusi tu ndiyo huchanganya Lugha?
 
Back
Top Bottom