Ushauri: Anzisheni utaratibu wa wahitimu wa elimu za juu kufundisha kwa mwaka mmoja

Ushauri: Anzisheni utaratibu wa wahitimu wa elimu za juu kufundisha kwa mwaka mmoja

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Tanzania kuna watoto wengi sana wanaingia shule kwa kasi kuliko uwezo wa serikali kuajiri walimu wa kutosha. Huu ni wakati mzuri wa kufikiria programu ya wahitimu wa elimu za juu ambao wengi nao ni vijana kufundisha kwenye shule mbalimbali kwa mwaka.

Serikali iweke utaratibu mzuri hili linawezekana kukabiliana na tatizo kubwa la walimu. Mpango huu uwe wa mpito na uwe wa kujitolea kwa masharti mazuri. Haya ni mambo ambayo napendekeza:
  1. Wanavyuo akijitolea kufundishwa asemehewe mkopo wake wa elimu kwa asilimia 30% kwa mwaka. Mfano kama deni lako ni Tsh 12M basi msamaha kwa mwaka ni Tsh 4M.
  2. Kuwe na program za kuwaandaa kwa muda wa miezi miwili kabla ya kuondoka chuo.
  3. Kwa wale watakaofanya vizuri kwenye hii program na kuonyesha matokeo, mkataba unaweza kuongezwa kwa mwaka mmoja. Lakini hii program isizidi miaka miwili.
  4. Wahitimu wa sayansi na teknolojia wapewe kipaumbele.
  5. Hii program iwe ya kizalendo zaidi kama ilivyo JKT
  6. Shule za vijijini zipewe kipaumbele zaidi
 
Kama watafanya hivyo basi wafute kabisa kozi ya ualimu maana hawatoajiri tena

Mkuu unapokuwa kiongozi inatakiwa uwe na maono sio kutumia nguvu kuliko akili

Nawapa pole saana watu wote walio chini yako kimaamuzi
Mkeo (nampa pole)
Watoto zako (nawapa pole)
Wadogo zako (nawapa pole)
Wafanyakazi wenzio wafikishie pia salamu zangu za pole kwao
 
Kama una madaraka sehemu yoyote ile ni vyema ukajiudhuru kwa maslahi mapana ya taifa HUFAI
 
Alafu wakishamaliza huo mwaka mmoja wa kufundisha wanaenda wap ?
 
Kama mm ndio ningekuwa nimetoa wazo la kijinga namna hii hakika ningekimbia mafichoni miezi 9 kukwepa aibu
 
Wewe ni hasara kwa familia yako
Wewe ni tatizo kwa ukoo wako
Wewe ni problem kwa Jamii yako
Wewe ni shida kwa wilaya yako
Wewe ni tatizo kwa mkoa wako
Wewe ni janga kwa taifa lako
 
Wewe ni hasara kwa familia yako
Wewe ni tatizo kwa ukoo wako
Wewe ni problem kwa Jamii yako
Wewe ni shida kwa wilaya yako
Wewe ni tatizo kwa mkoa wako
Wewe ni janga kwa taifa lako
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 mkuu, msamehe huyu jamaa bana. Utamuua
 
Serekali fanyie kazi ongezeko la ajira kwa vijana, vijana wengi wako kitaa
 
Kuna rundo kubwa la walimu wa Science ambao hawana ajira na wamemaliza vyuo kuanzia 2019 na mpaka sasa bado wapo kitaaa

Mm sio mwalimu am mechanical engineer

Hizo shule za vijijini ambazo hazina walimu waajiri walimu mazima sio kushauri waajiriwe walimu wa bure kufanya hivyo ni kuuwa soko la WALIMU
Jamaa upuuzi sana kukosa ajira uingilie sector za watu hakuna mwalimu atakubali huu upuuzi ni mawazo ya kipuuzi

Heshima kwenye taaluma za watu
 
Hoja yako inapwaya sana yaani bado aujaangalia vitu vingi kwa mfano je wahitimu ambao awakukopeshwa wao wananufaikaje na huo mpango wako ujaelezea. Alafu mbona kwa nn usiishauri serikali waajiri walimu mambo ya kujitolea ni utumwa uliopitiliza na mimi huwa nawadharau sana walimu wanaojitolea nawaona vichaa uho mdah wanaupata wapi wanaendeshaje maisha yao? Nashaangaa sana serikali iache janja janja jobless wenzangu tuwe toxic kwa serikali ituajiri tusijitoleee tunasababisha serikali hata isifikilie kuajiri akuna cha uzalendo wa kipuuzi wakati wao hata mishahara yao aikatwi kodi wengine waanze wao kuonesha uzalendo kwanza
 
Back
Top Bottom