Ushauri: Biashara ya butchery vs salon ya kike

Joined
Apr 4, 2019
Posts
81
Reaction score
90
Wakuu nawasalimu,

Ama baada ya salaam naombeni ushauri wenu.

Kuna frem ipo maeneo ninayoishi nataka kuilipia. Bado niko dilemma ni biashara gani niweke hapo kati ya butchery (Bucha) au salon ya kike.

Kodi ya frem ni 50,000 kwa mwezi.

Biashara gani itanifaa hasa ukizingatia eneo ninaloishi kuna Bucha moja tu na saluni pia sio nyingi kivile.

Natanguliza shukrani.
 
miss personal cook,

Wewe ni mtaalamu wa kusuka?Kama ww unaiweza hyo kazi ya kusuka nakushauri ufungue saluni.
Lakini Kama hujui kusuka achana navyo vyote.

Siku hizi naona sehem nyingi nikipita nyama zinadoda sana. Labda Kama hyo sehem Kuna vibanda vingi vya mama ntilie.
 
biashara zote nzuri ila biashara inayo muhusu mwanamke ni nzuri zaidi.

MUHIMU: uwe mfanyabiashara kweli.
 
Edit sehem ya kodi

Hv kwa bucha, nyama utakuwa unatoa WAP mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…