Uchaguzi 2020 Ushauri: CCM jiwekeni kando, wapo wenye uwezo zaidi

Uchaguzi 2020 Ushauri: CCM jiwekeni kando, wapo wenye uwezo zaidi

Vyote hivyo hakuna mwingine alievianzisha ni CCM na mpaka kesho ataendelea kuboresha kila sekta.
Ni CCM tu mwenye hiyo dhamana. Wengine msubiri kidogo mpaka 2045


ccm itakuepo mpaka 2100 according to polepole himself, hio 45 umewapendelea sana
 
Salama.

Kiukweli nawaonea huruma CCM chama cha siasa kwa namna wanavyohangaika huku na huko kutafuta mapenzi kwa wapiga kura kwa gharama kubwa sana na wananchi kuwashawishi pasipo maana.

CCM jichunguzeni kupitia mifano na kazi zilizopita. Fanyeni mchanganuo sahihi na bora kuhusu wananchi kwa ujumla wanawazungumziaje matendo yenu na siasa mnayoitumia kuhudumia na kutatua changamoto zao.

Changamoto kubwa inayowasumbua CCM kwasasa na haiwezi kukwepeka ni ongezeko kubwa la wasomi nchini linalopelekea siasa zenu za ahadi uongo, sera za kufirika, tambo, umaarufu na mambo yanayoendana na hayo kuwa kikwazo kwa CCM kujitetea kwa wananchi na wapiga kura halisi.

1. Nchi hii ilikuwa na viwanda lukuki karibia kila mkoa na mazao ya kimkakati, CCM kwa uzembe wenu mkaua kila kitu.

2. Nchi hii wasomi mbalimbali walipata ajira ya moja kwa moja kutoka vyuo walivyosoma kwenda idara na taasisi mbalimbali nchini, CCM mkavuruga utaratibu wote na kuwaweka watoto wenu, ndugu na jamaa zenu mkaharibu kila kitu na kusababisha tatizo la ajira nchini.

3. Nchi hii ilikuwa na vyuo vya kuandaa viongozi na watawala, CCM mkavurugavuruga kila kitu na kuanza kuchaguana chaguana kwa uchama na uswahiba.

4. Nchi hii sera ya biashara na uwekezaji wakati huo ilikuwa rafiki, CCM mkaanza kukwepa kodi na kufungua biashara zisizo halali yaani walio wengi wenu wenye mamlaka mkavuruga vuruga ovyo ovyo ndio chanzo cha ninyi CCM kuwa na mrundikano wa kodi na ushuru usio maana.

NB

CCM brothers & sisters, it's too late to apologize royal voters.

Tanzania nchi tamu sana.
Ni ngumu sana kuilewa ccm, jitahidi kutuliza akili yako utailewa tu.
 
Mtaji wa CCM ni ujinga wawananchi, hivyo basi kadri ujinga unavyopungua ndivyo na umaarufu wa CCM unapungua.

ushawahi kutana na mtu ameenda shule vizuri anaishabikia hio saccos? we angalia tu viongozi wenu kuanzia mbowe mpaka leo wote shule walikimbia na ndo chama chenu kilivo, tafuta mtu ambae akili zmemkaa timam utaona kama anashabikia hio saccoss yenu!
 
Subiri kipenga kipigwe ndiyo utawajua ccm kama chama cha ukombozi. Je mnajua kuwa mmeanza kampeni kabla ya muda official. Msije kuja mkulialia.Fuateni instruction za mtihani, subirini supplementary zinawafuata mgongoni

Hakika wagombea wote waliisha anza kampeni kabla ya muda
 
Umenikumbusha walivyo ianzisha ile SUKITA jamaa walipiga pesa vibaya hawa hawa ccm.
Kuna wakati mjumbe wa mkutano alimuuliza katibu mkuu wa CCM Mzee Rashid Kawawa Report ya mapato na matumizi ya CCM,Mwenyekiti Mwl.Nyerere akamwamlisha mjumbe akae chini,na wajumbe wengi wakashangilia nakusema CHAMA KIMLINDE.
Maana yake CCM kutokea TANU hawakujali kudhibiti mali za Chama.Kwao ni utiifu kwa Mwenyekiti wa chama na chama chenyewe.
 
Back
Top Bottom