Ushauri: Idris Sultan biashara itakutoa achana na uchekeshaji

pambana sultan!! una improve kila siku..komaa komaa
 
Kuimba na kuchana. Kuna tofauti gani?
 
Unamjua Indris Sultan? Aliwahi kua na $300,000 YA BBA Dec 2014 , hii ni million 650. leo hii 2017 ameajiriwa na Clouds afanye Stand Comedy huyu mtu hovyo sana anaitaji watu wakumshauri kila hatua ya mambo yake asiachwe akafanya maamuzi peke yake, kwa pesa alizo zipata afanani na maisha anayo ishi-sasa hivi
 
Chalii ni mpuuzi sana yani kwa ile bingo angeweza fungua biahara hata 10 tofauti na still akabaki na mtaji wa kutosha. Ila kwa kuwa kiande hata ile hela haijulikani imeishaje. 650 millions then niishie kuwa mtangazaji, hell no!!!

Nilichokiona jamaa anataka ku maintain publicity ila angekuwa na akili angefungua hata consultancy firm akawa anatoa counsellation kwa raia kuhusu mambo ya biashara au hata maswala ya mahusiano kisha anawacharge fees. Kwa influence aliokuwa nayo ingemlipa tu kibongo bongo watu wa psychology wapo kibao angeajiri vichwa kadha vikawa vinampigia pesa tu.

Angeweza kuwa na goli la spear parts za magari kubwa tu mjini kati awe anafata mzigo china au japan akawa anapiga pesa ndefu tu. Accessories za magari kama rims, miziki maybe akawa hata anatoa service kama dick sound vile. Hela angepata biashara ikienda poa unatia na carwash yako kabisa. Kwa kutumia nguvu ya jina angepata wateja kibao tu uhakika.

Kwa mwaka aliopata mipunga (2014) angeweza kuanza na coaster hata 4 ambazo hazifiki hata 200m mjini biashara ya usafirishaji inalipa sana kwa jiji kama Dar. Pesa ipo kwa kweli hasa ukianza na gari mpya ndani ya miezi sita unakuwa na uwezo wa kuleta gari mpya kama kwa day kila gari inaleta sio chini ya laki moja.

Biashara ya maji pia inalipa mjini kwa ile mipunga angefanya co-branding na kampuni mfano bhakresa group akaomba kufanyia kwa maji ya uhai yakawa kama version mpya edition ya idris sultan angeweza piga pesa because ana influence tayari. Ingelipa na wangefaidika wote. Huo mfano tu ila kuna products nyingi za ku co-brand. Kile kimefanyika na Diamond karanga kika boost sales it also an instance of co-branding. Mjini akili tu wazee tatizo vijana wanajisahau sana.

Bado kuna investment za risk free kama muoga wa biashara angenunua eneo la kiwanja kikubwa linalofikika mjini kirahisi hata kama ni 50m then akatoa viji apartment vya vyumba viwili vyenye jiko na choo na kasebule ndani walau kwa 25m unatoa kenye finishing kali.Kwa budget ya 250m akiwekeza kwa hata vijumba 8 eneo potential ma bachelor watakaa tu angekuwa anavuta 150 kila mwezi kwa nyumba 8.

Upele humuota mtu asie na kucha mazee. Tuishie hapa kwa leo mambo ni mengi.
 
Anayemkubali sultani ujue anawakubali na futuhi.
 

Just encourage him. It costs you nothing. Nothing! Hata wewe kuna waliokudharau wakakubali huwezi kufanikiwa kwenye malengo yako. Lakini kuna waliokupa hamasa! Yes, sultan anaweza kuwa na mapungufu katika hiyo vocation aliyoichagua. Lakini akikomaa atafanikiwa. Yeye si wa kwanza wala wa mwisho. Mfano kipindi tunasoma kuna wengine baada ya kufeli lasaba wazazi waliwatosa wakaambiwa wachunge mifugo shule hawawezi tena. BAADHI walipata wasamaria wakasonga mbele. Leo in maprofesa na wanategemewa na familia zao. Kikubwa in kutokata tamaa.

Just a word of encouragement will do. Ingependeza sana ungeanzisha uzi huu kumpatia encouragement hata michango humu ingekuwa na tofauti.

Maisha ndivyo yalivyo. Mafanikio yana sura nyingi.
 
Kweli mwenyewe sijamkubali kwenye tasnia ya comedy, nimeaangalia zaidi ya mara mbili bila kuambulia kicheko
 
Umengia kwenye siasa,mtoa mada amaendika uzi kutoka na uhalisia wa mambo yalivyo kukumbuka alikuwa mashidi wa Big brother Afrika na akapata 650.milion kama angekuwa mtu wa maaana angefanya jambo kubwa now tungekuwa tunaongea mambo mengine jamaa kwenye comedy amefell ashike jembe akalime
 
Apo kwenye kujenga nyumba tuko pamoja mkuuu

Kwa mpunga alio-upata ungetosha kabisa kuanzisha company yake Real Estate akajenga nyumba akapangisha like now angekuwa mbali hii biashara ni-low lisk na ingekuwa brand kubwa sana na wangepanga watu wakubwa katika nnchi yetu hata wasanii, kutokana na jina lake





Wema Sepetu amelamba mpunga wote
 
Jamani Idrisa sio kama hachekeshi
.. tatizo awamu hii kucheka imekuwa ni mtihani.. mabandama yote yameathirika na ukata.
 
Ki ukweli naangaliaga kipindi chake lakini sioni kama kina elements za comedy sioni kwa kweli na ninafikiri hiyo aitime amepewa either atakuwa analipa mkwanja mzito au amepewa tu kwa kuwa ni celebrity
 
Tena usikute bado anaishi nyumba ya kupanga
 
Kwa hiyo usipocheka wewe unadhani na wengine hawacheki??Inawezekana una stress zako hata Mr Bean hawezi kukuchekesha
Unaonekana una msongo wa mawazo wewe..huyo jamaa analazimisha fani tu...anajitahidi abakie relevant.....
Ndo tatizo.la watu wa mkoa wakiingia mjini wanakuaga na ka ulimbukeni fulani hivii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…