Ushauri: Ili kuimarisha upinzani, CHADEMA tusikiite "chama kikuu" cha upinzani

Ushauri: Ili kuimarisha upinzani, CHADEMA tusikiite "chama kikuu" cha upinzani

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kwa mtazamo wangu, tunapotaka kuimarisha umoja miongoni mwa vyama vya upinzani nchini, moja ya jambo tunalopaswa kuliepuka au kutoendelea nalo ni kuita CHADEMA chama kikuu cha upinzani.

Nasema hivi kwasababu, matmuzi ya jina hilo yanajenga inferiority complex miongoni mwa vyama vya upinzani na pia matumizi ya neno hilo yanachangia upinzani miongoni mwa vyama vya upinzani badala ya umoja.

Ni wazi matumizi ya maneno chama kikuu cha upinzani yametafsiriwa kutoka kwenye matumizi ya maneno: "main opposition party " yanayotumika katika lugha ya kingereza. Swali ni je, kwa lugha ya wenzetu, neno "main" linaleeta tafsiri kama inayoletwa na maneno chama kkuu? Na je, tunapaswa kuiga kila kitu?

Binafsi naona maneno sahihi ni kama chama kikubwa cha upinzani au chama chenye wafuasi wengi na si maneno chama kikuu.

Mimi ni mpenzi CHADEMA lakini huwa sipendezwi na matumizi ya hayo maneno kama ambavyo huwa sipendezwi na matumizi ya neno "mtukufu" unapotaka kum-address kiongozi na ni bora watu wengine ambao sio wana-CHADEMA au viongozi wa CHADEMA ndio wakatuita hivyo lakini sio sisi WANA-CHADEMA na viongozi wetu.

Let's be humble na tuachane na huu "ukuu" kwani nguvu ya chama chetu inajieleza yenyewe.

Nafarijika sana leo kuona vyama vingine vya upinzani vikitoa mawakili wao kuungana na wale wa CHADEMA kumpigania kamanda Mbowe ingawa vyama hivi sometimes huwa vinatupa wasiwasi ila adui yetu mkubwa ni CCM na si ACT, NCCR au chama kingine chochote cha upinzani.

Ni ushauri kwa nia njema.
 
Vyovyote hats tukiita chama Dume
 
Ni ushauri mzuri, lkn sidhani kama vijana hapa ufipa wapo tayari kushaurika ktk kipindi hiki. Sana sana watakwambia umeshanunuliwa, na hapo pia watakuwa wamekuheshimu kidogo.
 
Sasa hao chadema wenyewe mara zote huwatuhumu wenzao kuwa ni vyama vilivyoanzishwa na ccm au vinatumika na ccm, Lissu aliwahi kutamka kuwa vyama vya upinzani vya kweli ni Chadema na Cuf pekee. Wakati huo kabla Cuf hii ya Lipumba.

Kwahiyo issue sio kujiita bali hivyo ndivyo wanavyoamini wao kwamba upinzani Tanzania ni Chadema na Chadema ndio upinzani.
 
Sasa hao chadema wenyewe mara zote huwatuhumu wenzao kuwa ni vyama vilivyoanzishwa na ccm au vinatumika na ccm, Lissu aliwahi kutamka kuwa vyama vya upinzani vya kweli ni Chadema na Cuf pekee. Wakati huo kabla Cuf hii ya Lipumba.

Kwahiyo issue sio kujiita bali hivyo ndivyo wanavyoamini wao kwamba upinzani Tanzania ni Chadema na Chadema ndio upinzani.
Umeelewa mada lakini?
 
Kwa mtazamo wangu, tunapotaka kuimarisha umoja miongoni mwa vyama vya upinzani nchini, moja ya jambo tunalopaswa kuliepuka au kutoendelea nalo ni kuita CHADEMA chama kikuu cha upinzani.

Nasema hivi kwasababu, matmuzi ya jina hilo yanajenga inferiority complex miongoni mwa vyama vya upinzani na pia matumizi ya neno hilo yanachangia upinzani miongoni mwa vyama vya upinzani badala ya umoja.

Ni wazi matumizi ya maneno chama kikuu cha upinzani yametafsiriwa kutoka kwenye matumizi ya maneno: "main opposition party " yanayotumika katika lugha ya kingereza. Swali ni je, kwa lugha ya wenzetu, neno "main" linaleeta tafsiri kama inayoletwa na maneno chama kkuu? Na je, tunapaswa kuiga kila kitu?

Binafsi naona maneno sahihi ni kama chama kikubwa cha upinzani au chama chenye wafuasi wengi na si maneno chama kikuu.

Mimi ni mpenzi CHADEMA lakini huwa sipendezwi na matumizi ya hayo maneno kama ambavyo huwa sipendezwi na matumizi ya neno "mtukufu" unapotaka kum-address kiongozi na ni bora watu wengine ambao sio wana-CHADEMA au viongozi wa CHADEMA ndio wakatuita hivyo lakini sio sisi WANA-CHADEMA na viongozi wetu.

Let's be humble na tuachane na huu "ukuu" kwani nguvu ya chama chetu inajieleza yenyewe.

Nafarijika sana leo kuona vyama vingine vya upinzani vikitoa mawakili wao kuungana na wale wa CHADEMA kumpigania kamanda Mbowe ingawa vyama hivi sometimes huwa vinatupa wasiwasi ila adui yetu mkubwa ni CCM na si ACT, NCCR au chama kingine chochote cha upinzani.

Ni ushauri kwa nia njema.
Ushauri wangu kama mtu neutral. Hakuna shida na neno chama kikuu upinzani. Kama kuna chama cha siasa cha upinzani kinaumia kuona chadema ni chama kikuu cha upinzani hilo linadhihirisha jambo moja kubwa: kwamba vyama vyetu vya upinzani ni cocktail ya watu wabinafsi ambao kwao siasa za upinzani ni jukwaa jingine la kujitafutia maisha ya wao na watoto wao na wajukuu wao.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Binafsi naona maneno sahihi ni kama chama kikubwa cha upinzani au chama chenye wafuasi wengi
Mapendekezo yako bado hayataondoa inferiority complex kwa anayetaka ama aliyezoea kuijenga.

Maneno chama kikubwa na chama kikuu au main party yote yana maana sawa.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Umeelewa mada lakini?
Nimeilewa ndio maana nakwambia kwamba tatizo sio kujiita tu chama kikuu bali hivyo ndivyo wenyewe wanavyoamini na hilo ndio tatizo kubwa hapo na ndio maana nikakupa huo mfano wa Lissu.
 
Kwa mtazamo wangu, tunapotaka kuimarisha umoja miongoni mwa vyama vya upinzani nchini, moja ya jambo tunalopaswa kuliepuka au kutoendelea nalo ni kuita CHADEMA chama kikuu cha upinzani.

Nasema hivi kwasababu, matmuzi ya jina hilo yanajenga inferiority complex miongoni mwa vyama vya upinzani na pia matumizi ya neno hilo yanachangia upinzani miongoni mwa vyama vya upinzani badala ya umoja.

Ni wazi matumizi ya maneno chama kikuu cha upinzani yametafsiriwa kutoka kwenye matumizi ya maneno: "main opposition party " yanayotumika katika lugha ya kingereza. Swali ni je, kwa lugha ya wenzetu, neno "main" linaleeta tafsiri kama inayoletwa na maneno chama kkuu? Na je, tunapaswa kuiga kila kitu?

Binafsi naona maneno sahihi ni kama chama kikubwa cha upinzani au chama chenye wafuasi wengi na si maneno chama kikuu.

Mimi ni mpenzi CHADEMA lakini huwa sipendezwi na matumizi ya hayo maneno kama ambavyo huwa sipendezwi na matumizi ya neno "mtukufu" unapotaka kum-address kiongozi na ni bora watu wengine ambao sio wana-CHADEMA au viongozi wa CHADEMA ndio wakatuita hivyo lakini sio sisi WANA-CHADEMA na viongozi wetu.

Let's be humble na tuachane na huu "ukuu" kwani nguvu ya chama chetu inajieleza yenyewe.

Nafarijika sana leo kuona vyama vingine vya upinzani vikitoa mawakili wao kuungana na wale wa CHADEMA kumpigania kamanda Mbowe ingawa vyama hivi sometimes huwa vinatupa wasiwasi ila adui yetu mkubwa ni CCM na si ACT, NCCR au chama kingine chochote cha upinzani.

Ni ushauri kwa nia njema.
Kama chadema ndio chama chenye wafuasi wengi ndio chama kikuu cha upinzani hiyo haina shida wala mjadala.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Vyama vingine ni vyama lege lege ni vyama ambavyo maccm hawana wasiwasi navyo wanavitumia vyama hivyo vile watakavyo na ndiyo sababu viongozi na wanachama wa vyama hivyo hawafanyiwi udhalimu na dhuluma za kutisha kama wa Chadema kwa maoni yangu Chadema nadhani na ya Watanzania wengi ni chama kikuu cha upinzani na imekuwa hivyo kwa miaka mingi sasa pamoja na hujuma za maccm na baadhi ya vyama FEKI vya upinzani.
 
Back
Top Bottom