Ushauri: Kichanga wangu analia sana usiku

Hakikisheni wazazi wote wawili mnaoga vizuri kwa sabuni nzur zenye kuondoa jasho la mwili, vinyweleo makwapani mtoe maana harufu yake huenda ikawa inamdhuru mtoto jengeni utaratibu wa kupiga mswaki kila mnapotaka kulala, hakikisheni mtoto mnamuweka mbali kidogo na ninyi ili kumuepusha na audible lambling zenu(ushuzi) kama tatizo litakuwa bado endelevu mkamuone Dr. Haraka sana.
 
Umesema yote chief, Bravo [emoji122][emoji122][emoji122]

Nimependa ulivyomaliza kabisa kabisa wengi wangeanza kufikiri witchcraft manyuva [emoji23][emoji28][emoji23]
 
Watoto usiku huwa wanaona mengi mkuu , vitu vya kutisha hasa wakati wa kulala uwe unampakaa wanja katika nyuso zake " mi wa kwangu pia alikuwa hivo lakini nilvokuwa nampaka wanja hakuwa anasumbua tena .
[emoji15] [emoji15] [emoji15] kwq jinsia zote ?
 
Kawaone wabibi wa mambo ya watoto wachanga watakusiadia
 
uko sawa hata mimi wa kwangu alikuwa analia lakini wazee waliposema neno moja tu akawa analala mpaka anaamushwa
 
miezi 6 ya kwanza mtoto haitakiwi apewe chochote zaid ya ziwa la mama.
 
Watoto usiku huwa wanaona mengi mkuu , vitu vya kutisha hasa wakati wa kulala uwe unampakaa wanja katika nyuso zake " mi wa kwangu pia alikuwa hivo lakini nilvokuwa nampaka wanja hakuwa anasumbua tena .
Mmh!
 
Hongera sana baba.

Mie alikiuwa akilia nafanganya naumwa maana aio kazi rahisi.. First born alikuwa analia hadi na Mimi nalia, 2nd hajasimbua kwakweli.
Shukrani kwa pongezi


Kama ulivyosema kulea ni kazi kuliko kuzaa,kwa hili nawaheshimu sana wanawake waliokuza wanawe ,wengne hata bila wenzi wao
 
Duh! Jamani kazi kweli kweli
 
I had the same issue,
sasa hivi mwanangu ana miezi mitatu na siku 16 .mwezi wa pili ulikuwa changamoto tulikuwa tunapokezana kumbeleza . ni normal case kama mchangiaji mmoja hapo juu alivyoeleza. nunca de creer itakwisha cha msingi mama asiache kumnyonyesha na na nguo za kumvalisha usiku ziangalieni san zisije kuwa ni nzito sana au nyepesi sana kwani ni rahisi kusababisha pneumonia kwa mtoto joto husababisha pneumonia(high humidity)
 
Pole sana hii imenikuta tokea mtoto wangu akiwa na wiki mbili alikua analia na hivi ana sauti kubwa yani hadi majirani wanaamka wanadhani huwenda kuna tatizo limetukuta ndani, tunabembeleza usiku kucha na inapofika alfajiri analala na mchana wote analala, hivyo mchana wake ukawa usiku kwa miezi 7 mfululizo hakika tuliona rangi zote, analala mmoja unabembeleza ukichoka unampa mwenzako anapambana wewe unalala.

Ukienda hospital hana tatizo na ana afya njema kabisa na alianza kula akiwa na wezi mmoja tu.

Kwasasa ana miaka 4 na miezi kadhaa japo tabia yake ya kudeka bado anayo napambana nae.

Malezi sio mchezo.
 
Hii ilinikuta kwenye fungu moja japo sitaweka wazi yote, ila imani za kitamaduni hakika zipo, mtoto alimtesa sana mama yake, nilipofika na kumshika sikio tokea siku hiyo ikawa tiba hadi leo yupo shule
 
Kula mwezi mmoja? Mlikuwa mnamrisha chakula gani mkuu?? Maana kitaalamu mtoto chini ya miezi 6 inashauriwa anyonyeshwe maziwa ya mama tu,bila maji wala kitu chochote.

Mkuu pengine mwanao anaponyosha hashibi,au maziwa ya mama ni mepesi. Ale Mchele,mihogo,nazi vitu kama hivo vitasaidia katika upande wa maziwa ya mama.
Lakini pia kama mpo dar tazameni hali ya hewa hii,joto nyuzi 34 mkimvalisha nguo mingi kero kwake,kama mnalala na feni pia tatizo. Kama mpo kwenye baridi mkamvalisha nguo kiduchu akapigwa na baridi pia tatizo.
Wababa,msikimbilie kuwapa watoto wenu maji ya kunywa au maziwa ya kopo au vyakula when they are under 6 months kwa ushauri wa kitabibu.
 
Kama analia kwa kushtuka na sauti kali na ana mwili sana uwe unaponda kitunguu swaum unakifunga kwenye kitambaa unaweka jiran na kichwani akilala,... Mimi wangu pia ana miezi miwili wiki ilopita yote hatujalala ilikua timbwili hadi tulipoambiwa tufanye hivyo kwmb ni dalili ya degedege na huwakumba sana watoto wanene
 
Mkuu

Congratulations being dady to yr family,unaonesha unawajibika vyema kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…