Ushauri kuhusu leseni ya biashara

Ushauri kuhusu leseni ya biashara

ufumawicha

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2014
Posts
504
Reaction score
209
Ndugu wanajf wiki moja iliyopita nilikuja hapa na kuwashukuru kuwa baada ya kunishauri kuwa nifungue genge kwa kamtaji kangu kale ka sh.350,000/=.Nimefanikiwa kufungua genge kwa sh.100000/=na iliyobaki nimeweka kaduka kadogo nyuma ya genge.Nilienda TRA wanikadirie kodi kwa miezi 6 kwani nina mpango wa kuwa wakala wa MPESA,TIGO PESA ikibidi na AIRTEL MONEY.TRA waliniambia kwa miezi sita nitalipia sh.318,000/=ili nipewe tin number na kuanza kuitumia nilipe kwa pamoja nusu ya kodi hiyo,sh.159,000/=Kwa kuwa mauzo ni mazuri kwani kwa siku nauza kati ya sh.23000 na sh.35000 kwangu hiyo ni pesa kubwa kwani ndo naanza na niko kati ya watu wenye mitaji mikubwa mithili ya mlima kilimanjaro.Nimejipigapiga na jana nimelipia hiyo nusu TRA.Sasa wamenipa TAX CLEARENCE FORM eti nipeleke manispaa wanipe leseni,jamani mwenye uzoefu anielimishe kwani mimi ni muumini mzuri wa kulipa kodi ingawa lengo langu kubwa ni kufanya kabiashara kangu kiuhalali mbona naona kama mambo ni mengi mno?Je,huko manispaa watahitaji nini tena?Leseni ya biashara ni shilingi ngapi?Halafu Tra wameniandikia kwenye fomu yangu RETAIL SHOP,Hicho ni nini wadau?Halafu,kwa kuwa Tin number nimepewa je,naweza kuwaona Tigo,Vodacom na Airtel ili waweze kunisajili na kuwa wakala wao ili nianze kufanya miamala ya pesa?Maana hilo ni miongoni mwa malengo yangu!
 
Da mkuu pole ndio nchi yetu kodi nyingi sana kuliko income zetu lesene around 80000 mkuu
 
Hongera. Tin number hyo utaitumia ktk biashara zaidi ya 1 hata tgo,aitel na mpesa,genge n.k. ila leseni halmashauri au manispaa kuna afsa biashara atakupa leseni kulingana na aina ya biashara. Hapa tofauti na tra hawakadilii bali kila biashara inajulikana gharama zake. Kwa sasa lesen ni rahisi maana hao jamaa wamepewa masharti ili eafikie kiwango(target)
 
Hongera. Tin number hyo utaitumia ktk biashara zaidi ya 1 hata tgo,aitel na mpesa,genge n.k. ila leseni halmashauri au manispaa kuna afsa biashara atakupa leseni kulingana na aina ya biashara. Hapa tofauti na tra hawakadilii bali kila biashara inajulikana gharama zake. Kwa sasa lesen ni rahisi maana hao jamaa wamepewa masharti ili eafikie kiwango(target)
Umenitoa tongotongo mkuu kumbe ndio maana wamepunguza mikwara, acha kesho na mie niende
 
Lesen ya biashara manispaa haijalishi kama umelipa tax clearance au la. Cha msingi ni uwe na TIN ya biashara.
Leseni ya Vyakula na biashara ndogo ndogo ni jumla ya Tshs. 71,000 Hii utaweza fanyia vyote ulivyovisema.
Uende manispaa na
  1. Copy ya kadi ya mpiga kura/NIDA/cheti cha kuzaliwa
  2. Copy ya TIN
  3. Copy ya mkataba wa chumba/fremu ya biashara
Kama mkataba. Nimeambatanisha copy ya huo hapo utumie vizuri.
 

Attachments

Ndugu wanajf wiki moja iliyopita nilikuja hapa na kuwashukuru kuwa baada ya kunishauri kuwa nifungue genge kwa kamtaji kangu kale ka sh.350,000/=.Nimefanikiwa kufungua genge kwa sh.100000/=na iliyobaki nimeweka kaduka kadogo nyuma ya genge.Nilienda TRA wanikadirie kodi kwa miezi 6 kwani nina mpango wa kuwa wakala wa MPESA,TIGO PESA ikibidi na AIRTEL MONEY.TRA waliniambia kwa miezi sita nitalipia sh.318,000/=ili nipewe tin number na kuanza kuitumia nilipe kwa pamoja nusu ya kodi hiyo,sh.159,000/=Kwa kuwa mauzo ni mazuri kwani kwa siku nauza kati ya sh.23000 na sh.35000 kwangu hiyo ni pesa kubwa kwani ndo naanza na niko kati ya watu wenye mitaji mikubwa mithili ya mlima kilimanjaro.Nimejipigapiga na jana nimelipia hiyo nusu TRA.Sasa wamenipa TAX CLEARENCE FORM eti nipeleke manispaa wanipe leseni,jamani mwenye uzoefu anielimishe kwani mimi ni muumini mzuri wa kulipa kodi ingawa lengo langu kubwa ni kufanya kabiashara kangu kiuhalali mbona naona kama mambo ni mengi mno?Je,huko manispaa watahitaji nini tena?Leseni ya biashara ni shilingi ngapi?Halafu Tra wameniandikia kwenye fomu yangu RETAIL SHOP,Hicho ni nini wadau?Halafu,kwa kuwa Tin number nimepewa je,naweza kuwaona Tigo,Vodacom na Airtel ili waweze kunisajili na kuwa wakala wao ili nianze kufanya miamala ya pesa?Maana hilo ni miongoni mwa malengo yangu!
Hivi hata ukishalipia na kupata leseni bado kuna kodi tena ya kulipia TRA?? Mbona sielewei mwenzenu??!!
 
Manispaa unalipa kodi mara mbili
Kwanza unalipia leseni
Pili utalipia ten parsent ya kodi ya pango

Kisha Tra utalipa kodi ya mapato
Na stemp duty
 
kwa mtaji huo kachukue kitambulisho cha machinga elfu ishirini , halafu nyie watu acheni ujinga ukienda tra wakikuuliza mapato yako kwa siku usiwaambie zaidi ya elfu tano ili wakukadirie kodi ndogo
 
kwa mtaji huo kachukue kitambulisho cha machinga elfu ishirini , halafu nyie watu acheni ujinga ukienda tra wakikuuliza mapato yako kwa siku usiwaambie zaidi ya elfu tano ili wakukadirie kodi ndogo
Kama mapato hayazidi sh5000 kwa siku maana yake hutakiwi kulipa kodi, kodi unaanza kulipa pale unapofikisha mauzo ya sh 4million kwa mwaka
 
Yan we hapo ndio ulipokosea sasa ungefanya biashara kwanza ili ujue faida na hasara mpango wa kwenda kulipa kodi mapema kiasi hicho utaijutia nafsi yako so kula mwaka utalipa hyo 315000
Kulipa Kodi in vyema ila sio kwa biashara kama hyo yako
Ungepambana kwanza mtaji ukae sawia TRA wakikuvaa unawahonga mchezo unaendelea
 
Kama mapato hayazidi sh5000 kwa siku maana yake hutakiwi kulipa kodi, kodi unaanza kulipa pale unapofikisha mauzo ya sh 4million kwa mwaka
Kiwango cha chini cha kodi TRA ni Sh 150,000 ambapo pato la mlipaji la chini ni Sh 300,000 kwa mwezi.
Mauzo yako yakiwa chini ya Sh 300k kwa mwezi wao watakupigia hiyohiyo Sh 150k kwa miezi 6
 
Kiwango cha chini cha kodi TRA ni Sh 150,000 ambapo pato la mlipaji la chini ni Sh 300,000 kwa mwezi.
Mauzo yako yakiwa chini ya Sh 300k kwa mwezi wao watakupigia hiyohiyo Sh 150k kwa miezi 6
Nilisoma mahali humuhumu wakasema kuanzia 4m to 7.5m kwa mwaka ndo unalipa 150k, chini ya 4m hulipi kitu
 
Nilisoma mahali humuhumu wakasema kuanzia 4m to 7.5m kwa mwaka ndo unalipa 150k, chini ya 4m hulipi kitu
Mimi nilipochukua TIN 2018 mwanzoni, waliniuliza mauzo yangu dukani kwa siku, nikawaambia Sh 10,000, wakanikadiria Sh 150k kwa miezi 6 na nilitakiwa kulipa katika awamu 2
 
Mimi nilipochukua TIN 2018 mwanzoni, waliniuliza mauzo yangu dukani kwa siku, nikawaambia Sh 10,000, wakanikadiria Sh 150k kwa miezi 6 na nilitakiwa kulipa katika awamu 2
[emoji15] [emoji15] hawa jamaa mi siwaelewi, mbona ukipiga hesabu kwa mwaka haizidi 4m na wamekulipisha!!! Na hiyo 150k nilijua ni kwa mwaka kumbe ni kwa miezi 6!!! Aaah siendi tena,nimeghairi
 
[emoji15] [emoji15] hawa jamaa mi siwaelewi, mbona ukipiga hesabu kwa mwaka haizidi 4m na wamekulipisha!!! Na hiyo 150k nilijua ni kwa mwaka kumbe ni kwa miezi 6!!! Aaah siendi tena,nimeghairi
Nenda tu ukaonane nao. Uzuri mnazungumza. Unaweza kuwa unauza Sh 50k kwa siku, ukawaambia Sh 10,000 kwa siku.
Mind you wataomba mkataba wako wa pango pia watakuuliza mtaji ulio anzia. Pango na mtaji vikiwa vikubwa itaashiria mauzo ya siku nayo ni makubwa. Hivyo inabidi uwe makini ili mzani ubalansi
 
Mkuu ulkosea kwenda TRA hasa biashara ikiwa mwanzon...mimi wakat naanza walinikadiria 350 kwa mwaka...ubaya ni kuwa alienda mzee maana mimi kitambulisho sina...!!nililipa mwaka wa kwanza but nilianza kuona mtaji na faida inakata....nkapiga hesabu nikagundua hela zote znaenda TRA....nmesitisha kulipa...na nmeshawaandikia barua ya kufunga biashara....nasubiri mpk sku nikieda niongee nao mwenyew...!!japo biashara bado nafanya
 
Back
Top Bottom