Ushauri kuhusu wazo la huu mfumo

Ushauri kuhusu wazo la huu mfumo

Habari wanabodi,

Shida ya hii forum unaweza kuomba ushauti mijitu inakutazama tu[emoji706]

Twende kwenye Mada
TZ na dunia nzima wafanyabiashara na wanunuzi wanakutana na barrier ya uaminifu.Hasa wanunuzi waliombali na muuzaji lets say mikoa tofauti.

Kwa kuona hiyo.Ndipo zinakuta technology ya Ecommerce.Zipo site nyingi za Ecommerce kama ebay,Amazom,Alibaba,kikuu, na nyingine nyingi.

Kupitia hizi ecommerce maarufu mnunuzi anaweza kununua kitu chochote akiwa sehemu yoyote ile duniani.

TOFAUTI na hizo ecommerce kubwa yani International kuna hizi za local kama Jiji, jumia, Kupatana.com hizi site na App zinatofauti kidogo kwani hutaweza kufanya malipo ya bidhaa moja kwa moja badala yake utawekewa namba ya muuzaji.

SASA WAZO NDIO LINAKUJA HAPO
Nini kinakwamisha ecommerce za bongo kutokuwa na payment gateway?

Na uzuri wake ni kwamba kwa kila bidhaa itayouzwa unakata % kadhaa.Mfano bidhaa inauzwa 10,000 tsh/ wewe unakata 500/ na mteja atakapo fanya malipo unaweka malipo PENDING..mteja atakapothibitisha kapokea malipo ndio nawewe unaruhusu malipo kwa muuzaji ndivyo wengine kina Amazon hufanya hivyo kuepusha wizi!!?

Sasa kwa uelewa wako hapa bongo ugumu utakuja wapi kwenye kutengeneza mfumo kama huu wa kuuza na kununua.Wewe unakuwa kama mtu wa kati tu unaemuunganisha mnunuzi na muuzaji

Sidhani kama nimeeleweka kwakua nimeandika kwa spidi ya jet bila kufanya marejeo ya bandiko ila kama umepata concept karibu tujadili.
IPO taasisi inaweza tumika kama msambazaji wa vitu unavyouza.na kupokea pesa wakati mteja anapoenda kupokea alichonunua mkoani popote Tanzania.hii taasisis yenyewe kufanya E Commerce,Sheria zake zinakinzana,ila mtu/Kampuni binafsi inaweza tumia miundo mbinu yake kusambaza na kupokea malipo kuktumia miundombinu yake.System ya E Commerce ni $35,000.
Karibu
 
Kwa jinsi ambavyo watanzania uaminifu wetu unatiliwa mashaka, ni heri kwenda na Escrow, kuwe na "mtu kati", it being airtel, voda or tigopesa au hata mifumo ya benki. Then mnunuzi akihitaji service anaweka kiasi kama ni 10,000 then mtu kati anazuia muamala hadi muuzaji atume mzigo, mnunuzi akishafanya confirmation ya kupata bidhaa hapo muuzaji anapewa pesa yake.
Technology inavyokimbia tutafika tu huku
 
Technology inavyokimbia tutafika tu huku
True, technology inatufikisha huko, kwa vile hatuna uaminifu wa viwango vya amazon, ebay nk, lazima biashara zifanyike namna hiyo.
 
Nadhani wanaoendesha hizo e-commerce ama wanakosa ubunifu au sheria na taratibu haziruhusu/hazipo au zina complication sana au changamoto ya kimfumo

Kuna vitu vitatu muhimu ili kukamilisha biashara hii

1. Online platform
2. Malipo
3. Usafiri

Online platform; MayuBey
Malipo; Azam Pesa
Usafiri; Posta/mabasi

Sasa hapa itategemea biashara yako unauza vitu vyako tu au watu mbalimbali watakua wanatumia platform yako kuuza vitu vyao pia

Juma Mtwara akinunua Asali kutoka kwa Lisu Singida kupitia Mayubey atafanya malipo Azam Pesa baada ya kupata reference no kutoka Mayubey

Malipo ataya hold Azam Pesa hadi mzigo umfikie Juma Mtwara ndio Lisu Singida atalipwa

Itategemea usafiri utakua umepangwa vipi
Ama Lisu Singida atalipia na atarudishiwa hela yake ya usafiri atakapolipwa au kutakuwa na mkataba maalum na makampuni, Lisu atapewa ref No atapeleka post na posta watapokea mzigo na kuusafirisha na watalipwa na Mayubey(changamoto ni miundombinu ya namna ya usafiri labda yupo kijijini nk)

Azam Pesa atafanya malipo kwa Lisu Singida baada ya mzigo kufika kwa Juma Mtwara na akaridhika na Mayubey kutoa go ahead alipwe

Then Azam Pesa atakata asilimia yake labda na kodi kisha iliobaki ataingiza Mayubey

Changamoto hapo ni namna ya ku sync kati ya Mayubet app/seller/buyer, Azam Pesa na msafirishaji(hapo vitu vinafanyika online)
Mchakato wote huu anayetakiwa ku initiate ni Mayubey

Halafu sasa baada ya hayo kukamilika inakuja issue ya UAMINIFU
Je Lisu atatuma asali aliyoiyaka Juma?
Je juma atakua mkweli bidhaa aliyopata ipo ok au ataleta usumbufu tu?

Kwa mfano Ebay na Amazon seller wengi huwa hawataki ku ship nchi za dunia ya tatu kama Tz kwasababu ya usumbufu wa buyers wa huku
Mtu hasomi vizuri descriptions za bidhaa anaagiza tu halafu ukifika ana complain

Naamini hawa Jiji wangekuwa serious wakawafuata Azam au mpesa wakayajenga naamini inawezekana kabisa
Kisha wakayajenga na mabasi au posta.... mambo yangekuwa si haba
Aisee umefafanua vizuri kabisaa sasa nikujibu ili uongeze nyama na madini

1.Nia yangu ecommerce hii sio kuuza vitu vyangu kabisaa labda itokee kwa bahati mbaya.Ila nia ni User kupost vitu vyake selller na bayer wakutane

Mpango kazi:
Kutokana na changamoto ya kununua vitu huko IG,whatsapp au kokote kuonekana na wizi mwingi.Ndio sasa linapokuja hili wazo la kuanzisha ecommerce ambapo seller atakutana na Buyer atakua na uwezo wa kuchat nae vizuri kabisa na hata kumpigia.

Changamoto:
Njia ya Malipo ambayo seller atapokea pesa moja kwa moja bila kupitia kwa mtu ILA tu kwenye hayo malipo kuna asilimia kadhaa inakwatwa na kampuni(ecommerce)

Pili,Kutokana na kutoaminiana Naona App hii kuwe na feature ambayo kabla ya seller kupost bidhaa zake.Awe amepitia vetting ikiwemo verification ya kitambulisho cha Nida,TIN n.k hapo ndio mfumo utaapprove kama seller ni genuine au LA.

Tatu,Kutakuwa na feature ya REVIEW kwa seller kama kawaida.seller mwenye review nyingi nzuri atajiweka nafasi nzuri ya kuuza zaidi bidhaa zake.Seller mwenye review ndogo atawekwa kikaangoni.Ikiwemo kumfutia ID(account) yake kwenye database ikibainnika utapeli wa aina yoyote.

Nne,Feature nyingine ni Seller ataweza kulipia Blue tick na kampuni ikiapprove ni genuine itampatia Bluetick na kumuongezea premium features kama vile bidhaa yake kuwa promoted as top ads

Tano:Technology nayopanga kutumia ni Flutter,sqlite,php,js,react,next js n.k ila itakuwa App based tu kwa kuanzia.Halafu badae ndio tutaweka na website.

Mwenye chochote cha kuchangia karibu tukamilishe ndoto hizi wakuu..KARIBUNI
 
Habari wanabodi,

Shida ya hii forum unaweza kuomba ushauti mijitu inakutazama tu[emoji706]

Twende kwenye Mada
TZ na dunia nzima wafanyabiashara na wanunuzi wanakutana na barrier ya uaminifu.Hasa wanunuzi waliombali na muuzaji lets say mikoa tofauti.

Kwa kuona hiyo.Ndipo zinakuta technology ya Ecommerce.Zipo site nyingi za Ecommerce kama ebay,Amazom,Alibaba,kikuu, na nyingine nyingi.

Kupitia hizi ecommerce maarufu mnunuzi anaweza kununua kitu chochote akiwa sehemu yoyote ile duniani.

TOFAUTI na hizo ecommerce kubwa yani International kuna hizi za local kama Jiji, jumia, Kupatana.com hizi site na App zinatofauti kidogo kwani hutaweza kufanya malipo ya bidhaa moja kwa moja badala yake utawekewa namba ya muuzaji.

SASA WAZO NDIO LINAKUJA HAPO
Nini kinakwamisha ecommerce za bongo kutokuwa na payment gateway?

Na uzuri wake ni kwamba kwa kila bidhaa itayouzwa unakata % kadhaa.Mfano bidhaa inauzwa 10,000 tsh/ wewe unakata 500/ na mteja atakapo fanya malipo unaweka malipo PENDING..mteja atakapothibitisha kapokea malipo ndio nawewe unaruhusu malipo kwa muuzaji ndivyo wengine kina Amazon hufanya hivyo kuepusha wizi!!?

Sasa kwa uelewa wako hapa bongo ugumu utakuja wapi kwenye kutengeneza mfumo kama huu wa kuuza na kununua.Wewe unakuwa kama mtu wa kati tu unaemuunganisha mnunuzi na muuzaji

Sidhani kama nimeeleweka kwakua nimeandika kwa spidi ya jet bila kufanya marejeo ya bandiko ila kama umepata concept karibu tujadili.
Ukitaka kujua kikwazo ni nini nenda kwenye hizo kampuni za simu waambie unataka api ,

Watakupa list ya vitu wanavyo taka kisha uanze kuvifatilia ,

Hapo ndio utaelewa why! Kwaniniiii!
 
Ukitaka kujua kikwazo ni nini nenda kwenye hizo kampuni za simu waambie unataka api ,

Watakupa list ya vitu wanavyo taka kisha uanze kuvifatilia ,

Hapo ndio utaelewa why! Kwaniniiii!
Nasikia wanamasharti kama yote?kwa harakaharaka mambo gani ni magumu kupata Api zao?
 
Back
Top Bottom