Ushauri Kutoka kwa Grand Legend

Ushauri Kutoka kwa Grand Legend

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20241115_134437_Google.jpg


Watu muhimu katika maisha yako ni wale ambao wameamua kushea maisha na wewe hivyo uwajali sana

Unaweza kuishi maisha marefu au mafupi,ila jali sana ujana wako

Vitu ni vitu tu,usiwekeze sana sana katika vitu ila katika mda na uzoefu

Wivu unaharibu mahusiano,jifunze kumwamini mwenzako,je ni nani mwingine unapaswa kumuamini?

Watu siku zote wanasema hakikisha unafanya kazi unayoipenda,ila hilo sio wazo au ushauri mzuri,kazi nzuri ni ile ambayo unaweza kuipenda baadhi ya siku,kuivumilia baadhi ya siku na ukakidhi mahitaji yako,kwani hakuna mtu ambaye anaipenda kazi yake kila siku.

Usichukulie maisha kwa umakini sana hata pale mambo yanapokuwa magumu na hayaeleweki,jaribu kucheka kwani maisha ndivyo yalivyo

Watoto wanakuwa haraka sana,kwahiyo hakikisha unakuwa na mda wa kufurahi nao

Usichukue mawazo ya mtu kama Ufunuo,unaweza kuomba ushauri kwa mtu mnaye heshimiana halafu linganisha na mazingira yako kisha fanya uamuzi

Lipa madeni yako na uwe huru

Unapokuwa na ndoto ya kufanya jambo gumu wewe jaribu kufanya tu

Unapokutana na mtu kwa mara ya kwanza,jua kwamba hujui kuhusu yeye,unachoona mbele yako ni jinsia yake,mavazi yake na mwonekano wake.

Ijumaa Mubarak

Ni hayo tu!
 
Back
Top Bottom