Ushauri kwa Diamond: Unatia aibu, achana na Makonda anakuharibia sana

Diamond kwa kweli pale ali kera kweli, hivi zile akili alizo zionesha kwenye kuizima bifu yake na Kiba zilimfanya aonekane ana maana, halafu akaja kuharibu kabisaaaa kwa kuonekana na Bashite.
Kwanza yeye ina muongezeaa nini aki kaa jirani na Bashite?, angekaa home ingempungua nini?, hajui kuwa RC alikuwa ana mtumia kwa aijili tu ya kutaka vijisifa vyake mwenyewe.
Namkubali sana Domo ila kwa Bashite kaonesha u pompompo wa hali ya juu.
 
Diamind mlimshutumu sana alivyoipigia kampeni ccm kuwa atapoteza mashabiki lkn matokeo yake kaongeza mashabiki maradufu zikiwemo tuzo.
Kwenda kwenye party ya makonda hakutampunguzia chochote.
Halafu makonda hatumii cheti cha mtu mpk itakapothibitika mahakamani.
Mnafungua kesi jumanne kwa mujibu wa mstahiki meya wa ubungo..ngojeni kesi iishe uamuzi utoke hapo ndipo makonda atajua fate yake kama atafungwa ama la lkn mpk sasa bado ni 100 percent innocent.
 
Bob Marley alipogundua kila Mwanasiasa kule Jamaica anataka kumtumia kisiasa kwa sababu ya nyota yake ya Ustaa, hakumuunga mkono yeyote waziwazi!

Hawa wanamuziki wa sasa waachane na wanasiasa, ni bora kama wanataka kuwa wanasiasa basi wasimame wao kama wao!
 
Diamond ni Punda so anajua kabisa kitanuka muda si Mrefu no wonder anajaribu kujificha Nyuma ya Mgongo wa Bashite
Kimsingi Wasanii wote ambao ni ma punda au wanaojihusisha na Ngada wote wamefunga ndoa na ma Gamba kwa minajili ya kujificha wasistukiwe.
Wasanii wote ambao wako stand bila Magumashi na Mziki wao uko Juu hutokaa uwasikie wanajipendekeza kwa Ma Magamba
Ona Msanii kama King Kiba,Joe Makini (Mwamba wa Kaskazin),Fid Q ,Darasa,Lady Jay Dee etc hutakaa uwaone wanajipendekeza kwa watu kama Daud Bashite
 
Watanzania sijui tutapona lini, huku JF nako tunajiita GT lakini mambo tunayoshabikia hayaendani na sifa yenyewe.

GT kwa kipi hasa??.

Jaribu kuwa msomaji wa mada na maoni ya watu humu JF kwa wiki nzima bila kuchangia chochote, utapata majibu kwanini nasema hivi..
 
Mchafu ni yeye au wewe?

Anajuana nae miaka mingi, ulikuwa wapi kumshauri au umeona nini kibaya kimemtokea Diamond. Jembe la Taifa Mh. Makonda yupo juuuuuuuuuu

Acha wivu, uvivu na tamaa

Yaani unamfikiria Makonda hadi kuingilia maisha yake kila upande. Embu ishi kivyako wewe na wenzako wote


Mnamchafua mnashindwa, unakuja kuanza kuingilia maisha ya watu.

Umeandika upupwu haswa, fikiria maisha yako yasonge acha wivu.


Na bado


Makonda oyeeeeee
 
Labda na yeye amebanwa na kitu fulani au analipa fadhila ya kufanyiwa mpango wa kuongea na Rais 360
 
Mi nadhani nafasi aliyonayo makonda ndio iliyomfanya mond akakubali kuitika wito wa mkuu wa mkoa na sio kama mnavyodhani
Hivi unafikiri makonda aniondolewa kile cheo nani atamwita ataitika wito wake?
Hata hizo media na gsm watampuuza.

Makonda anatumia cheo chake na mahusiano yake na mkuu kufanya anachotaka

Kabla ya kuanza kulaumu mtu angalia kwanza mazingira ya tukio
 
diamond wa miaka ya 2015 kurudi nyuma sio huyu wa Leo, amepukutika,
 
Ni upuuzi kutaka Diamond aishi kwa kukuridhisha wewe na bavicha, ni upuuzi wa kiwango cha juu, kwenye sherehe kaenda na atarndelea kupeta kwa raha zake sio za mwingine!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…