Ushauri kwa Rais atakaeshinda: Uza Dreamliner zote, nunua ndege ndogo hata 30 na achana na route za nje

Ushauri kwa Rais atakaeshinda: Uza Dreamliner zote, nunua ndege ndogo hata 30 na achana na route za nje

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Ni wazi suala la kununua Dreamliner limetupiga sana, kwa kuwa tulitegemea zingepiga route za nje na kuingiza faida lakini mambo hayajawa hivyo. Na Corona imeharibu hata zaidi.

Ushauri wangu kwa raisi ajae, Tundu Lissu au Magufuli - uza hizo Dreamliner tuweke kipaombele kwenye flights za ndani tu. Achana na mambo ya kwenda Bombay au China, wakati muafaka ukifika tutafanya hivyo lakini kwa sasa ushindani ni mkubwa hata mashirika makubwa yanashindwa.

Lengo iwe kuifanya airport ya Dar kama stand ya mabasi ya mikoani inapofika asubuhi. Ndege zetu saizi ndogo ya Bombardier ziwe zimejipanga kwenda Arusha, Mwanza, Mbeya, Kigoma, Bukoba, Tabora, Mtwara Lindi nk, kila siku asubuhi, zikifanya ruti moja au mbili.

Na nauli lazima ishuke sana kiasi kwamba hata mwananchi wa kawaida aweze kumudu ili ndege ziwe zinaenda zimejaa abiria. Achana na mambo ya biskuti kwenye ndege, ndege ziwe zinafanya kazi katika mpangilio wa low cost airline. Weka baadhi ya nauli karibu sawa na nauli ya basi au juu kidigo ili ku-promote abiria kusafiri kwa ndege. Yaani tufanye kwa namna ya kupunguza kabisa mabasi barabarani.

Kama ukitaka route za nje sana sana weka route za East Afrika Community. Hata Joburg bondeni kule hamna haja ya kwenda.

Nawaambia tukifanya hivi tutafanikiwa sana!
 
Mabasi kituo cha Ubungo asubuhi. Fikiria hizi zingekuwa ni ndege zimejipanga airport asubuhi zinasubiri kwenda mikoani.

1603192946837.png
 
Mabasi kituo cha Ubungo asubuhi. Fikiria hizi zingekuwa ni ndege zimejipanga airport asubuhi zinasubiri kwenda mikoani.

View attachment 1606067
Hayo mabasi ya mchina zidisha Mara mikoa Mara wilaya utapata jumla ya mabasi kisha zudisha Mara idadi ya nchi za Afrika utapata idadi ya mabasi Afrika nzima halafu zidisha Mara miliini 200 -300 Hizo ndizo hela alizoingiza mchina.Baada ya miaka mitano yanakufa, halafi kuna vipuri hapo.Mchina lazima aew tajiri.Mshauri Magu aanzishe kiwanda cha mabasi atapiga hela.
 
wazo zuri sana maana sidhani kam faida ya kurusha boeing 787 mikoani wakati ni kwaajili ya safari ndefu inarudisha faida
ushindani ni mkubwa sana sidhani kama KQ,Ethiopia,EK,na mashirika mengine yatakuwa tayari kutuachia route
 
Una uhakika gani? Akishinda bwana yule ana mpango wa kuongeza nyingine takribani tano.
Hizi Dreamliner mbili kuzitumia tunashindwa, tumebaki kuzipiga safari za ndani na kuzibebesha mizigo na kuzikodi kwa ajili ya chama - sijui hata kama huwa wanalipa
 
Hayo mabasi ya mchina zidisha Mara mikoa Mara wilaya utapata jumla ya mabasi kisha zudisha Mara idadi ya nchi za Afrika utapata idadi ya mabasi Afrika nzima halafu zidisha Mara miliini 200 -300 Hizo ndizo hela alizoingiza mchina.Baada ya miaka mitano yanakufa, halafi kuna vipuri hapo.Mchina lazima aew tajiri.Mshauri Magu aanzishe kiwanda cha mabasi atapiga hela.
I say Mchina tumemfaidisha sana. Achilia mabasi, njoo kwenye boda boda na bajaji, yaani anachuma mno kwenye shamba letu.

Ndio maana nasema tubadilishe ATCL kuwa shirikala ndege la bei poa lihudumie hapa hapa Tanzania kwenda mikoani
 
Mimi naona wazo lako ni zuri. Kuliko ndege iende tupu. Ni bora wakapunguza ukali wa nauli ili ziende zimejaa kama ilivyokua kwa fastjet.
 
Yule baada ya kura tunamsindikiza Chato

Kazi mnayo, sijui mmejipanga vipi. HUko nyuma watu hawakuona aibu kutangaza mpinzani ameshindwa japo alikuwa ameshinda. Hata Zanzibar ilishatokea. Safari hii tofauti ni nini?

Nilishasema kumbuka kwamba wakuu wa taasisi zote nyeti wanajua watapoteza kazi zao, kuanzia jeshini, usalama, polisi, wakuu wa mikoa, wa wilaya, mwanasheria mkuu, mwendesha mashitaka, msemaji wa serikali, wakurugenzi nk. Hawa wote wana dhambi ya kufanya kazi kisiasa na wanajua kwa dhambi hiyo CCM wakishindwa hawatastahili kukaa kwenye nafasi zao. Sasa niambie, nani atakataa kupindua matokeo pale ambapo wanaona wanaelekea kukosa maslahi yao, Mkurugenzi wa NEC? Tanzania haiwezi kuwa na mapinduzi ya serikali, lakini ya uchaguzi yatakuwepo.
 
Afu unataka akose ya kwenda walingishia wananchi wa chattle kwamba anamiliki Dreamliner “ ndege ni zangu sipangiwi”
 
Back
Top Bottom