Ushauri kwa Serikali: Ajira za mkataba ndiyo suluhisho pekee la uhaba wa ajira nchini

Realistic kivipi sasa mkuu! Kwani watu wanaoajiriwa kwenye ma NGO wanaishije baada ya mikataba?

Potelea pote hata serikalini tu itakuwa na impact kubwa sababu watu watakuwa wanabadilika badilika chap! Fikiria serikali imeajiri around watu laki 4 wakiwa wanajitwist kila baada ya miaka 5 inamaana watu laki 3 watakuwa wanaingia ajirani kupishana na wanaokuwa wamemaliza mikataba, which is almost 50% ya graduates wote kwa kipindi cha hio miaka watakuwa wanapata kazi!

Wale wanaorudi mtaani wanakuja kusisimua uchumi kupitia miradi mbali mbali watayoanzisha! Watawa boost 50% ya graduates waliokosa ajira, uchumi utaendelea kukua huku hali za maisha zikiwa nzuri!
 
Anakua na mtaji wa kuanzisha ujasiria mali wowote ule sio sawa na kukosa ajira kabisa!!
Una Uhakika gani Atajiajiri !? Wengine watajiua Kwa Kukosa Mashahara. Kumbuka Nchi Yetu Inapitia Wakati ambao Nchi za Wenzetu kama Nigeria na South Afrika zilishapitia
 
Nani kaajiriwa Serikalini wewe? Wacha kujifanya unanijua!!!
Usitukane basi mzee, usiite upuuzi sababu una ahueni ya maisha kuna graduates wamemaliza chuo mda mrefu mwangaza hawauoni, mitaji hakuna!
 
Miaka Mitano Inflation Ya Pesa Yako Itakuwaje. Umesave Mil 1 kila Mwezi je Hiyo Mil 1 itakuwa na Thamani sawa baada ya Miaka 5. Mil 1 ingenunua Bundle 3 za Bati tuseme leo 2021 je 2026 itaweza Kununua Bati Bundle 3 au Zitakuwa Mbili na Nusu au Mbili
 
Hapo Itabidi hata Miaka ya Masomo Ipungue Pia. Maana Mtu anamaliza Masomo Wengine 30+ ishagonga
 
Tanzania kuna watu wengi ukiwaambia katiba mpya ni kitu muhimu sana watasema siyo muhimu lakini akigeuka analalamikia mambo yanasababishwa na katiba mbovu. Kwa kifupi wengi hawaoni correlation kati ya vitu kama ulivyoandika na katiba.
Ni kweli kabisa, kazi zingekuwa na mikataba hio hata hao viongozi wasingeshindana kufanya anasa! Wangejikita kufanya ya msingi sababu miaka michache ijayo wanatupwa mtaani na system.
 
Miaka Mitano Inflation Ya Pesa Yako Itakuwaje. Umesave Mil 1 kila Mwezi je Hiyo Mil 1 itakuwa na Thamani sawa baada ya Miaka 5. Mil 1 ingenunua Bundle 3 za Bati tuseme leo 2021 je 2026 itaweza Kununua Bati Bundle 3 au Zitakuwa Mbili na Nusu au Mbili
Utajiongeza sasa kama unanunua bundle za bati au una save pesa ikufae baadae! Sababu hata wa mikataba ya miaka 60 inflation iko pale pale!
 
Hii haina tija. Unawaajiri watu ná kuwapa training yenye gharama kubwa katika utendaji wa kazi zao za kila siku. Baada ya miaka mitatu wakati tayari wana experience ya kutosha katika utendaji wa kazi zao unawaondoa na kuwaleta wapya ambao hawajui chochote na zoezi la kutoa training upya linaanza tena!!!. Kuna wizi, ufisadi na ubadhirifu mkubwa sana Serikalini kama mianya hii ikiondolewa basi Serikali inaweza ikatoa ajira nyingine kati ya laki 5 mpaka milioni bila matatizo yoyote yale.

RAISI AJAE
 
Wakijiua ni mipango binafsi! Kama una 60m una uwezo wa kuizalisha kama huna jiunge na wanaoweza! This is how we create wealth
Katika Pesa Mzee kuna Kitu kinaitwa Greed(Tamaa). Omba Usipatwe na Hiki kitu hasa kwa Sisi Ambao Nchi Yetu ni Masikini hiki Kitu Kinatusumbua Sana. Hatuna Nidhamu katika Pesa

Huyo Mtu unayemzania Ataiwekeza Hiyo Pesa Utakutana Naye Siku Moja Anakuomba Pesa Ya Kula, Maana Alipoipata Aliona itaendelea Kuwepo Tu Haitoisha atanunua Vitu Alivyokuwa Hana Gari,Kuonga na Starehe Zinazokula Pesa Hatokumbuka Kuwekeza

Mfano Mzuri waangalie Wastaafu wa TZ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…