Ushauri kwa Serikali kuhusu uzalishaji mkubwa wa zao la mpunga msimu huu

Ushauri kwa Serikali kuhusu uzalishaji mkubwa wa zao la mpunga msimu huu

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
948
Reaction score
1,627
Kwanza tunamshukuru Mungu kwa uzalishaji mkubwa wa zao la mpunga kwa msimu huu. Kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha wananchi wamepata mavuno makubwa ya mpunga. Kwa sasa bei ya mchele inazidi kuteremka na ninaambiwa kuwa maeneo ya Katavi kilo moja ya mchele umefika Tshs. 600.

Pia wafanyabiashara wageni kutoka Uganda, Kenya wameanza kuingia maeneo ya Mkoa wa Mara, Simiyu, Shinyanga na Mwanza wakiwarubuni wakulima kuuza mpunga wao kwa bei ya kutupa. Ushauri wangu kwa Serikali, ni vema Serikali ikachukua uamuzi wa busara kununua mpunga wote toka kwa wananchi kwa bei rafiki kama Tshs. 80,000 kwa gunia la kilo 100 kuliko kurubuniwa na walanguzi wanaowarubuni kuuza gunia moja kwa Tshs.30,000.

Ninajua kuna dhana ya supply and demand lakini kwa Serikali inayojali wananchi wake ni vema ikaingilia kati. Tumeona Serikali ikinunua mazao kama mahindi vivyo hivyo wafanye kwa mpunga. Mpunga watakaonunua unaweza kuuzwa kwa dola ya Marekani kwa faida kubwa. Mhe. Bashe wasaidie wakulima wa mpunga.
 
Kwanza tunamshukuru Mungu kwa uzalishaji mkubwa wa zao la mpungu kwa msimu huu. Kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha wananchi wamepata mavuno makubwa ya mpunga. Kwa sasa bei ya mchele unazidi kuteremka na ninaambiwa kuwa maeneo ya Katavi kilo moja ya mchele umefika Tshs.600. Pia wafanyabiashara wagenii kutoka Uganda, Kenya wameanza kuingia maeneo ya Mkoa wa Mara, Simiyu, Shinyanga na Mwanza wakiwarubuni wakulima kuuza mpuunga wao kwa bei ya kutupa. Ushauri wangu kwa Serikali, ni vema Serikali ikachukua uamuzi wa busara kununua mpunga wote toka kwa wananchi kwa bei rafiki kama Tshs.80,000 kwa gunia la kilo 100 kuliko kurubuniwa na walanguzi wanaowarubuni kuuza gunia moja kwa Tshs.30,000. Ninajua kuna dhana ya suppy and demand lakini kwa Serikali inayojali wananchi wake ni vema ikaingilia kati. Tumeona Serikali ikinunua mazao kama mahindi vivyo hivyo wafanye kwa mpunga. Mpunga watakaonunua unaweza kuuzwa kwa dola ya Marekani kwa faida kubwa. Mhe. Bashe wasaidie wakulima wa mpunga.
Comments reserved
 
Kwanini wakulima wanakubali kuuza gunia bei ndogo namna hiyo?

Anyway, wakulima ndio watakaoamua wapi wauze magunia yao kutokana na mahitaji yao kimaisha kwa wakati husika.
 
Mwenye taarifa ya bei ya mpunga Kwa mikoa ya Tabora na Shinyanga naomba atupatie taarifa hiyo, natanguliza shukrani.
 
Back
Top Bottom