broken ages
JF-Expert Member
- Mar 23, 2012
- 235
- 84
Nimeona kitu kinachofanyika ama sijui ni tanesco ama ni jiji ila kwa namna nilivyoona ni uharibifu
ni kweli inawezekana kwamba miti hii inazuia ama inaleta madhara kwenye nyaya na njia za umeme na hivyo inapaswa kukatwa ili kupisha nyaya za umeme Hili siwezi kupingana nalo ila ambacho mimi hakijaniridhisha ni namna kazi hii inavyofanyika ndani yake kukiwepo uharibifu mkuwa mno wa mazingira na hata miundombinu ya barabara na taa za barabarani kama utakavyoona kwenye baadhi ya picha ambazo zimepigwa kwenye barabara inayotoka Impala hotel kwenda Philips ndani ya jiji la arusha
Wakataji wanakata miti hovyo na kuliacha eneo husika likiwa kama jangwa eneo ambalo lilikuwa na mandhari nzuri na ya kuvutia mno kabla ya ukataji huu usiozingatia ubora wa mazingira na hata namna ya ukataji wao ni kizamani mno miti inaanguka na kuzivunja taa zote za barabarani na wao wanaendelea na ukataji tu bila kujali (heri ingekuwa imevunjika taa moja ama mbili)
USHAURI WANGU ni bora wangeyaparua matawi yanayoelekea kwenye nyaya ama wakaipunguza urefu miti hiyo ikabaki kuwa mifupi kiasi kwamba haitofikia nyaya ili ikichanua ingependezesha bado eneo husika ama mazingira kuwa mazuri na umeme usipate madhara pia
na wakati wa kukata watumie wataalam na mashine kama misumeno ya kukatia miti(chainsaw) badala ya kutumia mashoka ambayo ni mtindo wa zamani mno na uliopitwa na wakati ili pia waweze kuimudu wapi ianguke na hivyo kuepuka uharibifu wa miundo mbinu nyingine
naomba kama mpango huo ni endelevu wazingatie ubora wa miti na mazingira ili yote yawe na nafasi yake.
ni kweli inawezekana kwamba miti hii inazuia ama inaleta madhara kwenye nyaya na njia za umeme na hivyo inapaswa kukatwa ili kupisha nyaya za umeme Hili siwezi kupingana nalo ila ambacho mimi hakijaniridhisha ni namna kazi hii inavyofanyika ndani yake kukiwepo uharibifu mkuwa mno wa mazingira na hata miundombinu ya barabara na taa za barabarani kama utakavyoona kwenye baadhi ya picha ambazo zimepigwa kwenye barabara inayotoka Impala hotel kwenda Philips ndani ya jiji la arusha
Wakataji wanakata miti hovyo na kuliacha eneo husika likiwa kama jangwa eneo ambalo lilikuwa na mandhari nzuri na ya kuvutia mno kabla ya ukataji huu usiozingatia ubora wa mazingira na hata namna ya ukataji wao ni kizamani mno miti inaanguka na kuzivunja taa zote za barabarani na wao wanaendelea na ukataji tu bila kujali (heri ingekuwa imevunjika taa moja ama mbili)
USHAURI WANGU ni bora wangeyaparua matawi yanayoelekea kwenye nyaya ama wakaipunguza urefu miti hiyo ikabaki kuwa mifupi kiasi kwamba haitofikia nyaya ili ikichanua ingependezesha bado eneo husika ama mazingira kuwa mazuri na umeme usipate madhara pia
na wakati wa kukata watumie wataalam na mashine kama misumeno ya kukatia miti(chainsaw) badala ya kutumia mashoka ambayo ni mtindo wa zamani mno na uliopitwa na wakati ili pia waweze kuimudu wapi ianguke na hivyo kuepuka uharibifu wa miundo mbinu nyingine
naomba kama mpango huo ni endelevu wazingatie ubora wa miti na mazingira ili yote yawe na nafasi yake.