Ushauri kwa TFF, bodi ya ligi na ligi kuu Tanzania

Ushauri kwa TFF, bodi ya ligi na ligi kuu Tanzania

isajorsergio

Platinum Member
Joined
Apr 22, 2018
Posts
4,143
Reaction score
6,560
Habari 👋

Siku ya leo nimeona vyema nizikumbushe mamlaka za soka nchini Tanzania katika masuala kadhaa, nitumaini langu baada ya ushauri huu utekelezaji utaanza na msimu mpya 2021/2022 tutashuhudia makubwa na yaliyokuwa bora. Nimekuwa mfuatiliaji wa masuala mbalimbali lakini mpira wa miguu umekuwa kama sehemu ya maisha yangu. Nikiri wazi nazitambua jitihada na maboresho yanayofanywa na TFF, Bodi ya Ligi na Ligi Kuu japo naona kuna nguvu ya ziada inahitajika kuboresha mchezo wa soka na ligi zake.

1. Kutengeneza na kusimimia chapa ya Ligi Kuu

TFF, Bodi ya Ligi na ushirika wa Wizara ya Michezo zihakikishe zinatengeneza chapa ya Ligi Kuu, kuiendesha na kuisimimia kuleta tija katika kuinua mchezo husika ndani ya taifa, kuingiza mapato, kutangaza taifa na kutoa burudani. Ligi Kuu ni vyema isimame yenyewe huku ikiwa na wadhamini katika mlengo wake. Ligi Kuu kama chapa itambulishwe, itambulike na ifahamike kwa wepesi kwa kila rika, jamii na hali tofauti.

Kupitia chapa ya Ligi Kuu kama taasisi zitengenezwe taasisi ndogo chini yake ambazo zitakuwa katika mlengo wa soka kama ifuatavyo:-

i/. Uwepo wa ligi kuu itakayosimama kawaida katika mpira wa miguu unaohusisha timu za wanaume (Ligi Kuu).​
ii/. Uwepo wa ligi kuu ya wanawake ambayo itapewa nguvu, kusimamiwa na kuendeshwa katika mfumo sawa na unaondesha ligi ya wanaume hii itambulike (Ligi Kuu ya Wanawake au Ligi Kuu Women).​
iii/. Uwepo wa ligi kuu ya vijana chini ya miaka 23 itakayofahamika kama (Ligi Kuu ya Vijana au Ligi Kuu U23).​
iii/. Kuanzisha ligi kuu ya vijana chini miaka 18 itakayofahamika kama (Ligi Kuu ya Vijana au Ligi Kuu U18).​
iv/. Uanzishwaji wa ligi kuu ya watoto chini ya miaka 13 itakayofahamika kama (Ligi Kuu ya Watoto au Ligi Kuu U13).​
v/. Uanzishwaji wa ligi kuu ya mpira wa ndani au Fútsal ambayo itapewa nguvu kuwezesha kuinua, kuonesha na kutengeneza ajira na mapato kwa vijana, taaisi na taifa.​
vi/. Kuanzisha ligi kuu ya mpira wa fukwe maarufu kama Beach Soccer, ligi hii ipewe nguvu na isimamiwe vilivyo kuwezesha kuleta tija kwa vijana na taifa.​
vii/. Uanzishwaji wa ligi kuu ya michezo kimtandao eSport au eGames, ligi kuu hii itahusisha mfumo wa ligi tajwa hapa juu utofauti wake yenyewe ni michezo ya kimtandao au games ambayo itahusisha zaidi wapenzi na wafuatiliaji mchezo wa soka.​
Mfano wa haya ni kama picha ambatanishwa zinazoonesha ligi kuu ya soka nchini Chile.​
Chile 1.png
Ligi Kuu​
Chile 4.png
Ligi Kuu ya Wnawake​
Chile 2.jpg
Ligi Daraja la Kwanza​
Chile 3.png
Ligi Daraja la Pili​
Chile 7.png
Ligi ya Vijana​
Chile 5.png
Kombe la Ligi​
Chile 9.jpg
Kombe la Shirikisho​
Chile 8.png
Ligu Kuu ya Mpira wa ndani | Futsal​
Chile 6.jpg
Ligi Kuu ya Michezo | eFootbal/ eGames​

2. Kupitia na kuweka taratibu mpya za muenekano wa vilabu ndani na nje ya uwanja

Ligi Kuu na Bodi ya Ligi zitatakiwa kuandaa mfumo utakaosimamia vilabu viwapo uwanjani na nje ya uwanja kimuenekano na katika chapa husika. Chapa za vilabu, wadhamini na ligi kuu kama ifuatavyo:-

i/. Timu zote shiriki zitatakiwa kutumia mwandiko 'font' rasmi katika jezi zao utakaotumika kuwatambulisha wachezaji na namba zao mgongoni, benchi la ufundi na wahusika wa timu ziwapo uwanjani au katika sare za timu. Katika hatua ya awali naambatanisha mfano na mwandiko pendekezwa.​

Ligi Kuu.png


Hii ni font ya GONTSERRAT ambayo inaweza kusomeka na kuonekana katika jezi kwa uzuri.

Ligi Kuu 1.png


Ligi Kuu 3.png


Ligi Kuu 2.png


Muonekano wa majina katika jezi.
ii/. Jezi za vilabu zitatakiwa kuambatanisha nembo au matangazo ya wadhamini kama ifuatavyo:- Mdhamini mkuu atatakiwa kuchukua nafasi eneo la kifuani, mdhamini mkuu wa pili atatakiwa kuchukua nafasi mkono wa kushoto, nembo ya Ligi Kuu itatakiwa kuwa mkono wa kulia na nafasi ya chini ya mgongo itumike tuu kuweka tangazo linalohusisha jamii au kuigusa jamii (Inaweza kuwa taasisi, shirika au kauli mbiu) mfano, JamiiForums Foundation au Vijana na Ajira, Zuia Rushwa, Tokomeza Uviko na Ajali Basi. Sehemu ya ziwa la kulia ni nembo ya mtayarishaji jezi na sehemu ya kushoto ni nembo ya timu husika basi.​
iii/. Vilabu vyote shiriki vyatakiwa kuwa na bao za matangazo na mahojiano kwa kila timu na iv/. Kila timu ni lazima ifanye mahojiano kabla na baada ya mchezo (Pre Match Conference na After Match Conference) na mahojiano na waandishi wa habari kabla na baada ya mchezo. Bao hizo ni mfano wa picha ambatanishwa hapa​
Ligi Kuu SYNGE.png

3. Ligi Kuu na vilabu kidijitali na mawasiliano yake

i/. Ligi Kuu ihakikishe inaanda mawasiliano yake kama Ligi Kuu katika mitandao ya Facebook, Twitter, Instagram, YouTube, Spotify na LinkedIn mitandao hii isimamiwe ipasavyo siku hadi siku kuwezesha kufikisha taarifa na maendeleo ya mchezo wa soka na ligi yenyewe.​
ii/. Iwe ni lazima kwa vilabu kuwa na majukwa katika mitandao hasa Facebook, Twitter na Instagram kupita mitandao hiyo itatakiwa vilabu vyote viwe hai 'active' na kuendesha akaunti hizo katika misingi ya soka, nidhamu na uungwana.​
iii/. Ligi Kuu inatakiwa kuwa na tovuti rasmi ambayo itakuwa sehemu rasmi ya taarifa, ratiba, sheria, muongozo na masuala yote yanayohusisha ligi kuu. mfano Campeonatos Chilenos 2021 au Premier League Football News, Fixtures, Scores & Results
iv/. Vilabu vyote ni lazima kuwa na tovuti rasmi katika shughuli zake za utendaji wa kila siku.​
4. Ligi Kuu, washirika na wadhamini

TFF, Bodi ya Ligi na Ligi Kuu ihakikishe kuna wadhamini wafuatao ndani yao:- i/. Mshirika mkuu wa ligi kuu (Lead Partner/s) ii/. Mshirika mkuu katika utoaji vifaa kwa ajili ya ligi kuu mpira na jezi maalumu za waamuzi (Official Ball Partener) iii/. Mshirika mkuu katika masuala ya kifedha (Official Bank) iv/. Mshirika mkuu katika masuala ya vinywaji (Official Drink Partner) v/. mshirika muu katika masuala ya muda amabaye atatoa bao za muda na vifaa vya muda kwa waamuzi (Official Timekeeper) vi/. Mshirika mkuu katika masuala ya usafirishaji (Official Travel Partener).​

5. Ligu Kuu na taratibu za afya na usalama wa wachezaji na mashabiki

Ligi Kuu ihakikishe inasamimia na kupigania afya za washiriki katika mchezo na mashabiki ikiwa kwa kufuata taratibu za kujikinga na kupambana na UVIKO, maradhi ya moyo, magonjwa ya upumuaji, maradhi ya ngozi na usalama wa jumla kwa kufuata yafuatayo:-​
i/. Ligi Kuu itatakiwa kuwa na madaktari rasmi kama taasisi katika kila mchezo ambao watasaidia katika dharura na msaada wa nyongeza, hii iambatane na ulazima wa vilabu kuwa na madaktari idhinishwa na vyama na taasisi zinazosimamia madaktari na kila timu na gari la kubebea wagonjwa.​
ii/. Timu zote zitatakiwa kuchukua tahadhari kabla, wakati na baada ya mchezo dhidi ya magonjwa tajwa hapo juu.​
iii/. Vilabu vyote vitatakiwa kuwa na hati za afya ya jumla kutoka kwa Hospitali za kitaifa/mikoa na kuidhinishwa jopo la madaktari wa ligi kuu.​
iv/. Mashabiki watatakiwa kuchukua tahadhari wawapo viwanjani kwa kuacha nafasi ya kiti au mtu mmoja baina yao kujikinga na kupambana na UVIKO.​
v/. Ligi Kuu inatakiwa kuajiri walinzi binafsi maarufu 'stewards' ambao watakuwa chini yao katika kulinda usalama wa wachezaji, timu, viongozi na mashabiki, ligi kuu chini ya TFF itatakiwa kuomba msaada wa askari polisi wachache sana kuwepo uwanjani kwa hali za dharura. Hii ni kuondoa mkanganyiko wa mpira na siasa na hali zisizo za kiungwana kama zilivyoshuhudiwa katika vipindi tofauti waandishi na mashabiki wakipigwa na askari.​

6. Chombo huru ndani ya Ligi Kuu kitakacho husika na urushaji wa matangazo kwa washirika

Ligi Kuu inatakiwa kuanzisha chombo chini yake kitachokuwa na majukumu ya:-​
i/. Uandaaji, uchakataji na urushaji matangazo ya mchezo wa soka.​
II/. Ujenzi wa makao makuu hayo.​
iii/. Ununuaji wa vifaa husika.​
iv/. kuajiri watendaji husika.​
v/. Kuzalisha na kusimamia shughuli za kila siku.​
7. Ligi Kuu, waamuzi na usaidizi wa video (Video Assistant Referee

Ligi Kuu ihakikishe inapitisha sheria na kuanza kutumika kwa usaidizi wa video (Video Assistant Referee) ikiwa ni pamoja na:-​
i/. Kuagiza au kushirikisha chombo cha Ligi Kuu Productions kufanikisha hilo.​
ii/. Kutoa mafunzo kwa waamuzi au wataalamu wa teknolojia ya habari na mawasiliano kufanikisha hilo.​
iii/. Kutafiti mbinu wezeshi zitakazo wezesha uwepo wa mfumo wa maamuzi ya video.​
Haya ni machache natumai kupitia hapa wadau mbalimbali watatoa maoni mengi zaidi kuhakikisha tunakuza soka na ligi ya Tanzania.

Sergio
 
Kwa ninavyojua Ligi ya Wanawake ipo. Ligi ya wanawake kupuuzwa ni tatizo kwa nchi nyingi kwa sisi ambao hata ligi kuu ni tatizo ni dhahiri ligi ya wanawake itakua tatizo zaidi.
Pia TFF iliwahi kuelekeza kila kilabu kiwe na timu ya U18 lakini nafikiri ni agizo ambalo halina ufuatiliaji.

Nakiri kwamba sifuatilii mpira wa Tanzania, hivyo sijawahi kujua kama kuna juhudi zozote TFF imewahi kuzifanya ili kuuinua mchezo wa soka nchini. Kwa kidogo ninachokijua naamini mabadiliko yanahitajika kuanzia vilabuni haswa kwenye swala la umiliki wa vilabu.

Umiliki wa timu wa 'Wanachama' na 'Mmiliki' huu ni uongo TFF iangalie hili swala, timu imilikiwe kwa hisa kila anayetaka kuimiliki KMC akanunue hisa. Anayetaka kuimiliki Sayari Queens akanunue hisa n.k.

Kwa sasa tunaweza zaidi kukabiliana na swala la umiliki kuliko haya mengine hivyo hilo lianze, likitengemaa vitu vingine vitakaa mahala pake tu. Ninaamini umiliki ndiyo jibu la vitendawili vingi. Vilabu hata 7 tu vikitatua hili swala TFF itabidi ibadilike iwe kwa kutaka ama la.

Mmiliki ambaye atakua na maono zaidi ya ubingwa wa ndani na kuifunga Simba na Yanga atalazimisha mashabiki waone na waamini picha kubwa zaidi. TFF itafuatia nyuma.

Mapendekezo yote ya kwenye huu uzi yangekuja na hakuna ambaye angepinga kwakua ni faida kwa ajili ya mpira wa Tanzania kwa wamiliki wa sasa ni ngumu kuliona hili.

Anyway, natamani viongozi wa TFF wangesoma huu uzi.
 
Shukrani Castr kwa hint! Kubwa, naona mfungo na structure zibadilike sasa kuwezesha mageuzi.

Ni kweli Ligi ya Wanawake ipo lakini haieleweki ni Ligi au bonanza. Katika hili ni lazima kwa vilabu kuwa na timu za wanawake, vijana na watoto.
 
Shukrani Castr kwa hint! Kubwa, naona mfungo na structure zibadilike sasa kuwezesha mageuzi.

Ni kweli Ligi ya Wanawake ipo lakini haieleweki ni Ligi au bonanza. Katika hili ni lazima kwa vilabu kuwa na timu za wanawake, vijana na watoto.
Ni kweli unakuta Timu A imeifunga Timu B magoli 11 na mchezaji mmoja kafunga magoli 9.
 
Kwa ninavyojua Ligi ya Wanawake ipo. Ligi ya wanawake kupuuzwa ni tatizo kwa nchi nyingi kwa sisi ambao hata ligi kuu ni tatizo ni dhahiri ligi ya wanawake itakua tatizo zaidi.
Pia TFF iliwahi kuelekeza kila kilabu kiwe na timu ya U18 lakini nafikiri ni agizo ambalo halina ufuatiliaji.

Nakiri kwamba sifuatilii mpira wa Tanzania, hivyo sijawahi kujua kama kuna juhudi zozote TFF imewahi kuzifanya ili kuuinua mchezo wa soka nchini. Kwa kidogo ninachokijua naamini mabadiliko yanahitajika kuanzia vilabuni haswa kwenye swala la umiliki wa vilabu.

Umiliki wa timu wa 'Wanachama' na 'Mmiliki' huu ni uongo TFF iangalie hili swala, timu imilikiwe kwa hisa kila anayetaka kuimiliki KMC akanunue hisa. Anayetaka kuimiliki Sayari Queens akanunue hisa n.k.

Kwa sasa tunaweza zaidi kukabiliana na swala la umiliki kuliko haya mengine hivyo hilo lianze, likitengemaa vitu vingine vitakaa mahala pake tu. Ninaamini umiliki ndiyo jibu la vitendawili vingi. Vilabu hata 7 tu vikitatua hili swala TFF itabidi ibadilike iwe kwa kutaka ama la.

Mmiliki ambaye atakua na maono zaidi ya ubingwa wa ndani na kuifunga Simba na Yanga atalazimisha mashabiki waone na waamini picha kubwa zaidi. TFF itafuatia nyuma.

Mapendekezo yote ya kwenye huu uzi yangekuja na hakuna ambaye angepinga kwakua ni faida kwa ajili ya mpira wa Tanzania kwa wamiliki wa sasa ni ngumu kuliona hili.

Anyway, natamani viongozi wa TFF wangesoma huu uzi.
Umechangia katika eneo ambalo kiukweli litasaidia kubadilisha soka la nchi hii.

Watu wamejimilikisha na wakafanya vilabu vya nchi hii kama vyao na familia zao na magenge yao. Yaani sisi tunaotokea huko wapi sijui hatuwezi sema lolote au kukaribishwa na yoyoyte kusema chochote. Wapo watu wazuri wenye maono chanya ya soka ambao kwa sababu tu kuna wazee wa yanga asili basi watu hao hawana nafasi ya kusema chochote juu ya klabu yao.

Hongera mkuu.
 
Mimi mchango wangu mkubwa utakuwa kwa TFF kuangalia namna gani misingi ya soka na kuendelezwa kwa vipaji kuna ratibiwa bila kuathiri shughuli nyengine za kawaida kwa watoto.

Uwekezaji wa kweli ni lazima uanzie kwa watoto. Kama wafanyavyo wenzetu Ulaya na mataifa mengine.

Soka isiwe mchezo wa watu waliokosa nafasi ki-elimu. Hapa mtaona kwamba wachezaji karibia wote ambao hufikia hivyo vinavyoitwa viwango vya juu hapa nchini ni wale ambalo shule yao sio kubwa, yaani watoto wa mtaani. Binafsi nilikuwa mchezaji mzuri sana wa mpira wa miguu, lakini mara tu baada ya kumaliza darasa la saba familia ilinitaka nichague kati ya mpira au elimu na hatimae nikachagua elimu.

Mipanngo ifanywe, wazazi washajihishwe na waaminishwe kwamba kucheza mpira hakutomfanya mtoto akose elimu, na sio waaminishwe tu bali vividly waone hivyo.

Ni nani anamjua kijana alipata kuitwa Ibra Messi?? alichezea Coastal Union halafu akaenda Simba kipindi cha Julio??

Yule kijana yuko wapi kwa sasa??
 
Mimi mchango wangu mkubwa utakuwa kwa TFF kuangalia namna gani misingi ya soka na kuendelezwa kwa vipaji kuna ratibiwa bila kuathiri shughuli nyengine za kawaida kwa watoto.

Uwekezaji wa kweli ni lazima uanzie kwa watoto. Kama wafanyavyo wenzetu Ulaya na mataifa mengine.

Soka isiwe mchezo wa watu waliokosa nafasi ki-elimu. Hapa mtaona kwamba wachezaji karibia wote ambao hufikia hivyo vinavyoitwa viwango vya juu hapa nchini ni wale ambalo shule yao sio kubwa, yaani watoto wa mtaani. Binafsi nilikuwa mchezaji mzuri sana wa mpira wa miguu, lakini mara tu baada ya kumaliza darasa la saba familia ilinitaka nichague kati ya mpira au elimu na hatimae nikachagua elimu.

Mipanngo ifanywe, wazazi washajihishwe na waaminishwe kwamba kucheza mpira hakutomfanya mtoto akose elimu, na sio waaminishwe tu bali vividly waone hivyo.

Ni nani anamjua kijana alipata kuitwa Ibra Messi?? alichezea Coastal Union halafu akaenda Simba kipindi cha Julio??

Yule kijana yuko wapi kwa sasa??
Miaka hiyo kulikua na Makongo kama sehemu ambayo michezo na elimu vinaweza kukaa sehemu moja.

Kulea vipaji ni mwanzo mzuri. Ila inahitajika uwekezaji ambao kama TFF kwa kushirikiana na vilabu na washikadau wengine sioni kama ni gumu.

Ni mchakato wa muda mrefu lakini malipo yake ni ya uhakika.
 
Miaka hiyo kulikua na Makongo kama sehemu ambayo michezo na elimu vinaweza kukaa sehemu moja.

Kulea vipaji ni mwanzo mzuri. Ila inahitajika uwekezaji ambao kama TFF kwa kushirikiana na vilabu na washikadau wengine sioni kama ni gumu.

Ni mchakato wa muda mrefu lakini malipo yake ni ya uhakika.
Ni kweli lakini wazee wakiamini kwamba ukishika masomo na mpira basi utayumba tu.

Ndio maana nkasema wazazi waelimishwe na waonyeshwe vividly kwamba mtoto anaweza kushiriki michezo na shule akafanya vizuri.

Na ndio nkauliza kuhusu Ibra Messi, unadhani wazazi wa Ibra Messi wanaweza mruhusu mtoto wao mwengine aache shule akacheze mpira??
 
Mimi mchango wangu mkubwa utakuwa kwa TFF kuangalia namna gani misingi ya soka na kuendelezwa kwa vipaji kuna ratibiwa bila kuathiri shughuli nyengine za kawaida kwa watoto.

Uwekezaji wa kweli ni lazima uanzie kwa watoto. Kama wafanyavyo wenzetu Ulaya na mataifa mengine.

Soka isiwe mchezo wa watu waliokosa nafasi ki-elimu. Hapa mtaona kwamba wachezaji karibia wote ambao hufikia hivyo vinavyoitwa viwango vya juu hapa nchini ni wale ambalo shule yao sio kubwa, yaani watoto wa mtaani. Binafsi nilikuwa mchezaji mzuri sana wa mpira wa miguu, lakini mara tu baada ya kumaliza darasa la saba familia ilinitaka nichague kati ya mpira au elimu na hatimae nikachagua elimu.

Mipanngo ifanywe, wazazi washajihishwe na waaminishwe kwamba kucheza mpira hakutomfanya mtoto akose elimu, na sio waaminishwe tu bali vividly waone hivyo.

Ni nani anamjua kijana alipata kuitwa Ibra Messi?? alichezea Coastal Union halafu akaenda Simba kipindi cha Julio??

Yule kijana yuko wapi kwa sasa??

Vizuri sana kugusia suala la kipawa, elimu na ajira kwa wakati. Ni wazi ziwekwe taratibu ambazo haziathiri kipaji na elimu kwa mtoto au kijana na itambulike wazi mpira na michezo ni sehemu ya ajira tena yenye ukwasi mkubwa.

Hata mimi nilikuwa mchezaji kwa bahati nzuri au mbaya nimewahi kucheza Walvis Bay City na FC Ulster ya watoto na nimewahi kutrain na Kagera Sugar nikiwa kinda kabisa. Nadhani baba angekubali niendeleze elimu na mpira leo hii ningekuwa Arsenal. 😅

Tunahitaji mabadiliko!
 
Vizuri sana kugusia suala la kipawa, elimu na ajira kwa wakati. Ni wazi ziwekwe taratibu ambazo haziathiri kipaji na elimu kwa mtoto au kijana na itambulike wazi mpira na michezo ni sehemu ya ajira tena yenye ukwasi mkubwa.

Hata mimi nilikuwa mchezaji kwa bahati nzuri au mbaya nimewahi kucheza Walvis Bay City na FC Ulster ya watoto na nimewahi kutrain na Kagera Sugar nikiwa kinda kabisa. Nadhani baba angekubali niendeleze elimu na mpira leo hii ningekuwa Arsenal. 😅

Tunahitaji mabadiliko!
Nimependa ulivyomalizia.

"Tunahitaji mabadiliko"
 
Nadhani baba angekubali niendeleze elimu na mpira leo hii ningekuwa Arsenal. 😅

Bora hukwenda huko, ungeishusha timu daraja (joke).

Naomba niongeze kitu:
Castr ameitaja Makongo, kipindi kile Kipingu alikuwa anawapata wachezaji kutoka kwenye mashindano ya Umitashumta na Umiseta ambaya Mungai aliyafuta.

Baada ya kufuta yale mashindano, hata mkazo wa michezo mashuleni ulikufa. Ambacho ilikuwa ni chanzo kikubwa cha kuona vipaji vikiwa bado vichanga.

Nini kifanyike?

Kwa kila wilaya, serikali kwa kushirikiana na TFF ijitahidi kuboresha miundombinu ya viwanja na irudishe mashindano yale, walau kuwe na shule ambazo ni affiliated na sports kwa kila wilaya, ambazo watoto wenye vipaji wanaweza kupata kama scholarships (hizi zinakuwa shule za kawaida ila zina mkazo wa michezo).

Hapo wenye academies za sports wanapata feeders, hata hizi timu za Ligi ambazo zitakuwa na youth teams hazitasumbuka sana kupata talents.
 
Bora hukwenda huko, ungeishusha timu daraja (joke).

Naomba niongeze kitu:
Castr ameitaja Makongo, kipindi kile kipingu alikuwa anawapata wachezaji kutoka kwenye mashindano ya Umitashumta na Umiseta ambaya Mungai aliyafuta.

Baada ya kufuta yale mashindano, hata mkazo wa michezo mashuleni ulikufa. Ambacho ilikuwa ni chanzo kikubwa cha kuona vipaji vikiwa bado vichanga.

Nini kifanyike?

Kwa kila wilaya, serikali kwa kushirikiana na TFF ijitahidi kuboresha miundombinu ya viwanja na irudishe mashindano yale, walau kuwe na shule ambazo ni affiliated na sports kwa kila wilaya, ambazo watoto wenye vipaji wanaweza kupata kama scholarships (hizi zinakuwa shule za kawaida ila zina mkazo wa michezo).

Hapo wenye academies za sports wanapata feeders, hata hizi timu za Ligi ambazo zitakuwa na youth teams hazitasumbuka sana kupata talents.
You nailed it! 👊 Kila wilaya ipate shule affiliated to sports. Hapa tutaona talanta za aina yake.
 
Ligi Kuu ihakikishe kila kiwanja tumika kinafungwa skrini kubwa yenye kuwezesha kuonesha mchezo moja kwa moja.

Pamoja na hayo, Ligi Kuu kwa ushirika na TFF, bodi ya Ligi, wizara ya michezo na vilabu husika wahakikishe wanafunga LCD Screens, bao za kuonesha matangazo pembezoni katika uwanja.
 
Kitengo anzishwa cha Ligi Kuu Productions chini ya Ligi Kuu kifanye uuzwaji wa haki za matangazo ya televisheni na redio kwa vituo mbalimbali ndani na nje ya taifa.

Katika hili Ligi Kuu na Ligi Kuu Productions ziandae packages za matangazo zikiwa katika vipengele vifuatavyo:-

i/. Matangazo ya moja kwa moja | Live Coverages (Kwa televisheni na redio).

ii/. Matangazo ya Mapitio | Replay's (Kwa televisheni).

iii/. Matangazo ya Mapitio | Highlights (Kwa televisheni).

Vituo vya runinga na redio vinunue haki za matangazo kwa Ligi Kuu Productions, pamoja na Ligi Kuu Productions kuuza haki tajwa katika mataifa yanayofuatilia Ligi Kuu. Baadhi ya mataifa haya ni Rwanda, Zambia, Kenya, Uganda na Burundi.
 
Dah..wadau mmeandika mengi as if ukiyasema yanatokea tu...guys hakuna kinachowezekana hapo Kama hakuna pesa..narudia tena hakuna kinachowezekana hapo Kama hakuna pesa..pesa pesa..pesa..aka.fedhaaa...

Maligi yote hayo hayataanzishwa kwa tamko la TFF ama Serikali..lazima pesa awepo...

Ambacho nafikiria kwanzA tuangalie namna ya kutatua changamoto ya pesa ambayo ndio itafanikisha haya yote..pesa ikishapatikana hii mipango mizirui itatekelezeka tu.

Mtazamo wangu ni hivi..Serikali iweke sheria kwa makampuni na taaisisi kwa kila mkoa,walaya kuhakikisha wanatumia pesa zao za SRF ( Social Responsibility Fund) kutenga nusu na kuzitekeleza kwenye shughuli za kimichezo aidha kwa kudhamini timu katika maeneo hayo ama kujenga miundombinu ya kimichezo ama kuikarabati..hii policy iko Sana Afrika kusin , Namibia na baadhi ya nchi nyingine za kusin huko.

Hii itasaidia kwanzA, kuboresha Hali za timu, kuzipa timu Hali ya ushindani na kukuza ajira .

Emu fikiria now ligi kuu iko na timu 16 what if kila timu inapotoka ikawa inapata hii support..ni wazi ushindani ungeongezeka..ushindani ukiongezeka..mashabiki wanajitokeza..mashabiki wakijitokeza..ligi inakuwa na mvuto na kuvutia kampuni nyingi zaidi kuwekeza kwenye soka..matokeo yAke tunakuwa na ligi yenye ushindani na inayouzika ..

Kule uingereza pia wanatumia policy hii..unakuta katimu ka daraja la sita huko..kifuani mwa jezi zao kumepachikwa mdhamini..

Kingine..naungana na mtoa hoja..TFF wanafaa waiache ligi kuu iwe ni project inayojitegemea waipe nafasi ya kuwa Kama kampuni ama taasisi binafsi ..yenye kujitosheleza..ikiwezekana iwe na wataalamu na wajuzi wa mambo ya marketing katika football Ili lengo litimie.

TFF ibaki kwenye kusimamaia maendelo ya mpira wa miguu na kuandaa sera za muda mrefu ,wakati na mfupi kwa timu za Taifa.
 
Kitengo anzishwa cha Ligi Kuu Productions chini ya Ligi Kuu kifanye uuzwaji wa haki za matangazo ya televisheni na redio kwa vituo mbalimbali ndani na nje ya taifa.

Katika hili Ligi Kuu na Ligi Kuu Productions ziandae packages za matangazo zikiwa katika vipengele vifuatavyo:-

i/. Matangazo ya moja kwa moja | Live Coverages (Kwa televisheni na redio).

ii/. Matangazo ya Mapitio | Replay's (Kwa televisheni).

iii/. Matangazo ya Mapitio | Highlights (Kwa televisheni).

Vituo vya runinga na redio vinunue haki za matangazo kwa Ligi Kuu Productions, pamoja na Ligi Kuu Productions kuuza haki tajwa katika mataifa yanayofuatilia Ligi Kuu. Baadhi ya mataifa haya ni Rwanda, Zambia, Kenya, Uganda na Burundi.
Sawa..je ligi yetu inauzika kiasi hiko...!? Kama hapa ndani tu Kuna baadhi ya timu zikivheza watazamaji hawafiki hata 10 sembuse kuuza haki za matangazo kwenye nchi zingine!?

Nadhan hoja iwe kwanzA kwenye kuboresha ligi yetu na kuifanya iwe na mvuto kwanzA kwetu sisi ..na hili litawesekana Kama lila timu itajengewa uwezo wa kushindana...

Mfano tazama Mbeya city ile ya Kocha Mwambusi. Wakati ule ilikuwa na full support ya mkoa..hamasa ilikuwa kubwa Sana Mbeya..timu yao ikicheza hata na timu ndogo watu walikuwa wanajitokeza kuwashangilia ..sasa ingaliea sasa..Mbeya city imeshuka hamasa..watu uwanjan wameisusa..

So tuzipe hamasa timu zetu kwanzA.kwa khziwezesha kiuchumi..zisajili vizuri. Kisha zishindane kwa uhalali wa kiuwezo ..na kuzingatia sheria za soka..timu ishinde kwa uweoz na sio kubebana..tukifanikiwa kwenye hiki..Hao EPL watakuja kuomba kozi hapa ...watanzania wanapenda soka..Ila soka halijafanyiwa mikakati ya kuwa la.kisasa
 
Ligi Kuu ihakikishe kila kiwanja tumika kinafungwa skrini kubwa yenye kuwezesha kuonesha mchezo moja kwa moja.

Pamoja na hayo, Ligi Kuu kwa ushirika na TFF, bodi ya Ligi, wizara ya michezo na vilabu husika wahakikishe wanafunga LCD Screens, bao za kuonesha matangazo pembezoni katika uwanja.
Pesa za kufunga hizo screen waziokote wapi!!? Ligi yetu inavalue ya hivyo..wafunge LCD screen za matangazo hayo kwenye miundombinu ipi!? Je gharama za kurun hizo screen zitakuwa kwa TFF ama timu za ligi kuu ama wamailiki wa viwanjan!?
 
Mimi mchango wangu mkubwa utakuwa kwa TFF kuangalia namna gani misingi ya soka na kuendelezwa kwa vipaji kuna ratibiwa bila kuathiri shughuli nyengine za kawaida kwa watoto.

Uwekezaji wa kweli ni lazima uanzie kwa watoto. Kama wafanyavyo wenzetu Ulaya na mataifa mengine.

Soka isiwe mchezo wa watu waliokosa nafasi ki-elimu. Hapa mtaona kwamba wachezaji karibia wote ambao hufikia hivyo vinavyoitwa viwango vya juu hapa nchini ni wale ambalo shule yao sio kubwa, yaani watoto wa mtaani. Binafsi nilikuwa mchezaji mzuri sana wa mpira wa miguu, lakini mara tu baada ya kumaliza darasa la saba familia ilinitaka nichague kati ya mpira au elimu na hatimae nikachagua elimu.

Mipanngo ifanywe, wazazi washajihishwe na waaminishwe kwamba kucheza mpira hakutomfanya mtoto akose elimu, na sio waaminishwe tu bali vividly waone hivyo.

Ni nani anamjua kijana alipata kuitwa Ibra Messi?? alichezea Coastal Union halafu akaenda Simba kipindi cha Julio??

Yule kijana yuko wapi kwa sasa??
Tuzalishe vijana alafu waende wapi..manara Kama kuzalishwa wapo wengi lakini Hawna ending nzuri..umemtolea mfano huyo ibra messi..je unauhakika kilichomfanya shindwe kuendelea ama kuachana na soka kimetatuliwa..!?

Hoja ibaki kuwa timu zijengewe uwezo wa kiuchumi Ili kuweza kumudu kuwahudumia wachezaji pamoja na kuzifanya ziwe na ushindani miongoni mwao..hii itawafanya wachezaji wengi kupata nafasi ya kutulia na kucheza...wakijua wanacheza kwa ajili ya ajira zao na sio kucheza riadha...

Gape lililopo baina ya timu za Simba, Yanga na Azam kinafaa kupunguzwa Kama si kulifuta kabisa..haswa katika eneo la ushindani ..na huwezi kulipinguza ama kuliondoa Kama timu hazijiwezi kiuchumi..matokeo yAke Hizo timu zitaendelea kusajili tena in free mode wachezaji wa hizo timu ndogo na hivyo kubakisha ushindani miongoni mwao...so ligi inakuwa na msisimko kwa timu tatu tu zinapocheza ...
 
Back
Top Bottom